Tafsiri ya Sizonje - Wimbo wa Mrisho Mpoto

Tafsiri ya Sizonje - Wimbo wa Mrisho Mpoto

Siku za hivi karibuni Msanii Mrisho mpoto katoa Wimbo wake ambao unaitwa SIZONJE na kasema Yakuwa Sizonje maana ake ni Ukombozi! Sasa mistari yake nimeona Niilete hapa tuijadiri nakuijua Vizuri nini Anamaanisha na nani Anazungumziwa hapa!

Najua ya kuwa wanasiasa na wachambuzi wa mambo ya kisiasa humu wapo wengi na watu wenye uelewa Mkubwa

Natambua ya kuwa mambo aliyo yazungumzia Mrisho mpoto ni yale current katika Nchi yetu! Tafadhari toa maana ya mstari utakao kuwa unajua maana yake,kama huwezi tuwe wavumilivu wengine watakuw wanatusaidia! Ila navyo jua kaimba mambo mengi na ya muhimu kujadiriwa hapa!

Anaanza kwa kusema
-Sizonje hii ndio nyumba yetu
Milango ipo wanapita madirishani
-Ingia uyaone, maajabu ya nyumba yetu
-Tulikaa barazani, tukasikia kelele,Kelele toka ndani, mtu anaruka dirishani,Sizonje, karibu nyumbani kwetu,Uone maajabu ya nyumbani kwetu

Mrisho anaendelea kwa kusema
-Karibu sana Sizonje, hii ndo nyumba yetu,Tulipoficha mundu za kupondea wezi
-Kwani, makaburi yaliofukuliwa lazima yazikwe upya?
-Nyumba hii Sizonje ina vyumba vinne,Vitatu havifunguki, kimoja hakina,mlango Japo kuwa kina watu ndani, na hawaongei kiswahili
-Wenyeji wanalala sebleni na walishazoea
-Sizonje kule tulipotoka panaitwa jikoni Huna haja ya kwenda kule, kumejaa mafundi wa kupika
-Sasa hivi wanakupikia wewe ili ule ulale Ukiamka muongee nini hasa ujio na dhima ya safari yako Wanashangaa mbona ghafla
-Samahani sana mgeni Wapishi wameniomba kwamba Nikuulize tena kwa kukuomba kwamba Eti unapenda vya mafuta au vya nazi?
-Wanataka kukuonyesha madoido katika mapishi yao Sizonje
-Sizonje chumba hiki naomba usiingie Ukimaliza nitakwambia kwanini
-Kuna sauti inajirudia mara kwa mara
-Na hapa mlangoni kulikuwa na picha mbili kubwa! Moja picha, nyingine mchoro wa picha wa kwanza
-Ninachokumbuka iliwahi kuandikwa “USIYEMTAKA KAJA”
-Hatukuwahi kuelewa maana yake Labda kwa sababu ya ujio wako unaweza kutusaidia
-Najua, wimbo mbaya haufai kubembelezea mtoto Na kamwe mtoto hawezi kuungua
Kwa kiazi kilichokuwa kwenye kiganja cha mama yake mzazi
-Njoo huku uone Sizonje Si unajua, harufu ya uzazi haiishi mpaka mtoto akue?
-Sawa, Sizonje, huu hapa ni ua Lile pale ni shimo la taka Na kile pale ni choo Kinachotutisha na kutuogopesha zaidi Wanaoishi humu ndani hawajawahi kutupa taka Wala kwenda chooni
-Kama ukiwa makini Kwa nje utasikia sauti za makundi ya
watu
-Wengi ni vijana, wana bahasha za khaki mikononi
-“KAMA HAMTUPI TAKA SHIMO HILI MLICHIMBA LA NINI?”
-Lakini pia kwenye sauti zao, Sizonje Kuna watoto, wazee na kina mama Ukiunganisha sauti zao ndio unapata hizo kelele
-Ninavyosikia, ila sina uhakika Waliambiwa kihistoria nyumba hii ni ya kwao Na wana haki ya kutupa taka na kutumia
choo hiki
-Sasa, njoo nikuonyeshe huku uchochoroni Uone maajabu mengine ya nyumba hii
-Sizonje, ukiona tembo anaringa Ujue mvua zinakaribia!
Hapo kamaliza!
Sinzonje ni magufuri nyumba ni tz, tulikaa balazani tukasikia kelele hichi ni kipindi cha lowassa kutangaza nia akiwa ccm makada wa ccm walipiga kelele walioaminishwa kuwa lowassa fisadi yaani kelele zilitoka ndani ya ccm, namtu aliyeruka dirishani ni huyohyo magufuri maana kwawaliotangaza nia ya urais magufuri hakuwemo akaja kuchomekwa tu ndo aliruka dirishani, na ndo anakalibishwa kuyaona matatizo ya nchi yetu, hii ndo myumba yetu tuliyoficha mundu za kupondea wezi yaani tz serekali yetu imeficha makucha dhidi ya mafisadi kwenye vyumba vitatu havifunguki sielewa ila kwenye kimoja hakina mlango japo kuwa kinawatu ndani hawaongei kiswahili hapo kaongelea wachina wamejazana na wanapata ajira ila wenyeji wanaolala sebuleni ni sisi watz hatuna ajira lakini wachina wanapata ajira na tunawaona ndo maana chumba chao kipo wazi, na wapishi hapo wametajwa ni akina kikwete mkapa na kundi lao ndo wanaopikia mpango mzima wa nchi, nawanasubilia tu dakika hizi za kwanza ziishe waanze kumwongoza njia zao zote za wizi apitie ndo wanamsubilia ale alale akiamka tu waanze kumwongoza,anaambiwa akiwa makini kwa nje atasikia kelele ni za vijana wa ukawa wamevalia gwanda za khaki✌✌✌, na ukiona tembo analinga hapo ujue mvua zimekalibia ni lowassaaa hashituki hatishwi anajiamini ukombozi umekalibia 2020 pipooooozzzzzzzz ✌✌✌✌✌ lowassaaa tena 2020 uelewa wangu umekomea hapo!!!
 
If you take time and listen... I think there are really wonderful jewel build inside this poetic song "sizonge"
 
Duh!wacha nami nitoe nilichoelewa vyumba vinne ni awamu zilizopita vitatu vinafunguka ina maana awamu ya kwanza mpaka ya tatu ya nne haina mlango ndo anasema usiingie mwisho nitakwambia kwa nini!kuhusu makaburi ni uozo wa uongozi uliopita so anasema yakifukuliwa kuna haja ya kuzika tena?
 
Fasihi huwa inamaana pana sana ila mi nilivyoelewa Sizonje ni kiongozi tulienae sasa na nyumba yetu ndo taifa letu milango ipo ila wanapitia madirishani yaani watu hawafuati utaratibu mfano kutoa mizigo bandarini kwa kutolipia kodi na kupitia dirishani nyumba ina vyumba 4 vitatu havifunguki na kimoja hakina mlango na watu wamo na hawaongei kiswahili hii ni kwamba awamu tatu za mwanzo zilikua zimefunga mianya ya unyonyaji na ufisadi ila awamu ya nne imekua wazi na kuwaacha wageni wafanye watakavyo na mengine mengi kama wimbo unaofaa humbembelezea mtoto na harufu ya uzazi haishi mpaka mtoto akue ni kuwa sera za Sizonje ni nzuri lakini taifa hili bado linanuka rushwa wizi na ufisadi wa hali ya juu na hali hiyo itakua sawa mpaka taifa litakapo kua
 
Duh!wacha nami nitoe nilichoelewa vyumba vinne ni awamu zilizopita vitatu vinafunguka ina maana awamu ya kwanza mpaka ya tatu ya nne haina mlango ndo anasema usiingie mwisho nitakwambia kwa nini!kuhusu makaburi ni uozo wa uongozi uliopita so anasema yakifukuliwa kuna haja ya kuzika tena?
At least nimepata mwanga.
 
Sizonje = Magufuli

Nyumba yetu = Nchi ya Tz

Wanapita madirishani = Rushwa

Makaburi yaliyofukiwa lazima yazikwe upya = Mambo ya zamani kwa nini uyafukue? (Wala rushwa kama akina Tiagi masamaki na HSC).

Chumba hiki usiingie = Usilijadili swala la HSC

Wenyeji wanalala sebuleni = Watanzania walalahoi hawana kazi na ofis nyeti wameshika wageni.

Kule tulikotoka wanaita jikoni = Hii ni awamu ya JK, full kujiachia na siri za nchi nje nje.

Chumba hakina mlango na waliomo hawazungumzi Kiswahili = Wageni wanaingia nchini bila vibali na kufanya kazi.

Usiyemtaka kaja = Wengi walikuwa hawamtaki Magufuli awe Rais sasa kawa.
Shukran kwa uchambuzi wako mkuu
 
Milango ipo wanapita madirishani.. = Sheria, taratibu na kanuni za kazi zipo lakini watu wanapindisha sheria na kufanya yao (wanapiga dili)
Hii je imekaaje ukiona tembo anaringa jua mvua zinakaribia
 
At least nimepata mwanga.
Shukran mtunzi kaficha tafsiri ili hadhira ishiriki kutafakari kwa namna mbalimbali.Nyumba yetu ni ikulu ndipo tulipoficha silaha zetu yaani nguvu ya kupambana na adui na jikoni ni wizara ya fedha shimo la taka ni ajira kwa vijana wetu wanawaambia zipo lakini hazipo au kwa mchongo ndo zinatoka.nawe unaweza kuleta uelewa wako.
 
sizonje ni raisi mpya as msanii anavyomwita kama mkombozi na kama watanzania wanavyoamini.

wimbo umejaa kwenye nyumba ambayo kwa mara ya kwanza binafsi nilidhani ni tanzania lakini vijana walioshika bahasha za khaki(wasaka ajira) wanaouliza KAMA HAMTUPI TAKA SHIMO HILI MLICHIMBA LA NINI? wanaonyezsha wazi kuwa nyumba ni serikali ya tanzania na wanachouliza ni KAMA HAMTUPI AJIRA MLITUSOMESHA KWA NINI?.
IDADI YA VYUMBA:kama ilivyosemwa kuwa nyumba ni serikali na kawaida ina mihili mi3 ila hii ya kina msanii ina vyumba vinne(mihimili mi4) mahakama,bunge,serikali ndio vile vyumba vi3 ambavyo havifunguki(havisikilizi wananchi) na cha nne ni watu toka ng'ambo ama mataifa makubwa ndio maana hakia mlango(hakihusiani na vyumba vingine wala wananchi) na hawaongei kiswahili kuonyesha ugeni wao

JIKO:jiko ni idara mbalimbali kama BANDARI,BENKI,TANESCO N.K...huko ndo kuna wizi sasa na wanahusiana sana na watu kama sizonje(raisi) ndo maana wanaulza anapenda vya aina gani????

CHUMBA KISOFUNGULIWA:sizonje mkkmbozi...chumba hiki kina picha(baba) na mchoro wa picha(huyu anaweza kuwa mwana wa baba) kwakuwa kulikuwa na picha na kisha ukaja mchooro.kulikuwa na baba na kisha mwana.pengine sizonje hatakiwi kufungua humu ndani maana kuna mabalaa yakutosha na yatazua makubwa.na maneno ya USOMTAKA KAJA kwani mwenye chumba alimtaka sizonje(baba)?

SHIMO NA CHOO:wachafu kutoka serikalini hatuwaoni mahakamani wala gerezani....

NB...MUONO HUU UNAWEZA KUWA TOFAUTI NA LENGO LA MSANII
 
kwenye kiitikio inaonyeshwa wazi kabisa pale msanii anapomkaribisha sizonje(raisi) kwenye nyumba(serikali)

kwenye kelele nadhani ni maswala ya chaguzi za vyama.kwani kuna mtu aliruka toka chama cha nyumbani kwa njia ya mazonge? ndo huyo wa dirishani labda AU kama mhakiki anatakiwa ayajue maswala yanayomtukia msanii na kumzunguka kilichotokea dirishani ni makonteni yaleeee...ya kule baharini na kulikuwa na kelele kweeeli...

maiti ilofukuliwa yaweza kuwa mafisadi wanaosafishwa sasa hivi.tushawafukua na kuuona uozo wao tunawazika ili iweje tunaficha nini?
 
Shukran mtunzi kaficha tafsiri ili hadhira ishiriki kutafakari kwa namna mbalimbali.Nyumba yetu ni ikulu ndipo tulipoficha silaha zetu yaani nguvu ya kupambana na adui na jikoni ni wizara ya fedha shimo la taka ni ajira kwa vijana wetu wanawaambia zipo lakini hazipo au kwa mchongo ndo zinatoka.nawe unaweza kuleta uelewa wako.
Sawasawa.
 
Mpoto mwenyewe kahojiwa kasema ye mwenyewe haelewi..Anaendelea kuusikiliza zaidi ili apate maana..
Duh hii kali; lakini inawezekana maana jamaa nyimbo zake nyingi anatungiwa.
 
NIMEMUELEWA ALIPOSEMA VIJANA WENYE BAHASHA ZA KAKI WANAOLALAMIKA KUTOTUMIWA KWA VYOO NA MASHIMO YA TAKA,KAMAANISHA VYAMA PINZANI HASA CHADEMA(GWANDA ZA KAKI)
 
Mpoto mwenyewe kahojiwa kasema ye mwenyewe haelewi..Anaendelea kuusikiliza zaidi ili apate maana..

Hahahahaahhhh....
Mkuu embu kuaa serious😀:lol:
 
Wachangiaji mmenisaidia sana at least nimeanza kuuelewa huu wimbo. Ama kweli penye wengi kuna mengi. Ngoja niendelee kuusikiliza tena.
Ila neno "sizonje" ni la kilugha ama ni kiswahili fasaha??
 
Back
Top Bottom