sudirashid
New Member
- Feb 21, 2025
- 2
- 5
Habari ya mchana
Nimeamua niwaandikie wenzangu kwa kifupi kuhusu madhara rafiki zangu waliyoyapata baada ya kununua mboga za majani pale stendi ya daladala Mbezi Luis.
Siku chache zilizopita rafiki zangu Hawa walinunua mchicha pale stendi ya mbezi Luis na kwenda kuupika na kula. Madhara waliyoyapata ni pamoja na kuchubuka ngozi, kushindwa kupumua vizuri, kuharisha damu, kutapika damu, vidonda vya Tumbo na kichwa kuuma sana muda wote. Hawa rafiki zangu walikwenda hospitali na kupima vipimo na kugundulika wamekula mboga zenye vimelea sumu. Pia Kuna taarifa mgonjwa mkaka amefariki kwa kula mboga hizi alizonunua mbezi yeye alikuwa akiishi kinyerezi.
Uchunguzi wa haraka niliofanya baada ya kuuliza ni wapi wamezipata zile mboga za majani wakasema wamezichukua zinapolimwa kibaha kwa Matias na chache picha ya ndege huko huko kibaha.
Naombeni kuwataadharisha kuhusu Kununua mboga za majani mbezi Luis zilizoagizwa kutoka zinapolimwa kibaha kwa Matias. Naomba uusambaze ujumbe huu kwa wapendwa wako utakuwa umeokoa maisha yao. Pia taarifa hizi nimezipeleka mamlaka husika
Asanteni
Nimeamua niwaandikie wenzangu kwa kifupi kuhusu madhara rafiki zangu waliyoyapata baada ya kununua mboga za majani pale stendi ya daladala Mbezi Luis.
Siku chache zilizopita rafiki zangu Hawa walinunua mchicha pale stendi ya mbezi Luis na kwenda kuupika na kula. Madhara waliyoyapata ni pamoja na kuchubuka ngozi, kushindwa kupumua vizuri, kuharisha damu, kutapika damu, vidonda vya Tumbo na kichwa kuuma sana muda wote. Hawa rafiki zangu walikwenda hospitali na kupima vipimo na kugundulika wamekula mboga zenye vimelea sumu. Pia Kuna taarifa mgonjwa mkaka amefariki kwa kula mboga hizi alizonunua mbezi yeye alikuwa akiishi kinyerezi.
Uchunguzi wa haraka niliofanya baada ya kuuliza ni wapi wamezipata zile mboga za majani wakasema wamezichukua zinapolimwa kibaha kwa Matias na chache picha ya ndege huko huko kibaha.
Naombeni kuwataadharisha kuhusu Kununua mboga za majani mbezi Luis zilizoagizwa kutoka zinapolimwa kibaha kwa Matias. Naomba uusambaze ujumbe huu kwa wapendwa wako utakuwa umeokoa maisha yao. Pia taarifa hizi nimezipeleka mamlaka husika
Asanteni