Tahadhari: Kwa hali ilivyo tusishangae kushuhudia kifo au vifo kwa wanagombania kupanda Mwendokasi

Tahadhari: Kwa hali ilivyo tusishangae kushuhudia kifo au vifo kwa wanagombania kupanda Mwendokasi

1. Utaratibu ule ulifanikiwa hapo awali wakati ulinzi ulikuwa ukisimamiwa na SUMA JKT, baada ya kubadilisha na kuweka kampuni binafsi ya ulinzi wanashindwa kudhibiti abiria kupanga foleni.

2. Utaratibu wa kupanga foleni unakuwa mgumu sababu unahitaji sana kuratibiwa na madereva wa mwendokasi ambaya anapaswa kudhibiti abiria kwa kuhakikisha mlango mmoja tu wa gari ndio unaofunguliwa, badala yake wakifika vituoni kama kivukoni wanafungua milango yote na kusababisha watu kugombania. Kwa kweli ni kero sana hakuna ustaarabu tena.
Upo sahihi watanzania usitaarabu ni zero si wanaume si wanawake si vijana Wala watu wazima wanaona kupanga foleni ni tatizo.
Pia watu wa ulinxi waondolewe itafutwe kampuni nyingine.
 
Shida hapo ni hayo mabasi yenyewe ni machache, kuna haja gani watu wapange foleni ikiwa gari linakuja kwa wakati na kuondoka kwa wakati? Unaweza ukakaa kituoni zaidi ya dk 45 na magari yapo pembeni madereva wanapiga story
 
Last week ndugu yangu aliumia mgongo kwa kusukumwa akipanda Mwendokasi Kariakoo. Nilitoka Mwanza kwenda kumsalimia kisha nikaenda kujionea mazingira yaliyopelekea yeye kuumia.

Naomba niseme tu kwamba kwa hali ilivyo kituo cha Msimbazi na Gerezani sitashangaa kukatokea kifo.

Kwa namna watoto wanavyosukumwa na jinsi abiria wanavyogombania magari tutapata maafa.

Niwaombe viongozi wa Mwendokasi na viongozi wa serikali, itasikitisha sana kujitokeza kuomboleza vifo vya wanafunzi katika kituo cha Msimbazi, Kivukoni,Gerezani, DIT,Fire, Korogwe na Kimara. Naandika just kutoa taadhari nikitambua sikio la kufa alisikii dawa
nadhani hata wanaichi wenyewe yafaa kutumia busara, na hekima iwaelekeze kutumia usafiri mbadala wakati jambo hilo likitaftiwa suluhu ya kudumu🐒

madhara na athari zitawapata wao hakuna haja ya kulazimisha kwamba lazima upande mwendokasi, japokua ni hali ya kipato inachochea yote hayo 🐒
 
Pale gerezani panafundisha ukomandoo na ukakamavu ukipazoea huwezi kuwa mtu wa kuendeshwa mpaka na kimbunga hidaya

Mi binafsi naona wapunguze mabus vurugu iongezeke tuwe maninja kabisa

Gerezan kimara
Sio lelemama
 
Pale gerezani panafundisha ukomandoo na ukakamavu ukipazoea huwezi kuwa mtu wa kuendeshwa mpaka na kimbunga hidaya

Mi binafsi naona wapunguze mabus vurugu iongezeke tuwe maninja kabisa

Gerezan kimara
Sio lelemama
Makomando wa nchi kavu 🤣🤣🤣🤣
 
Kwanini wananchi msipange foleni? Kuna kipindi pale kivukoni nilikuwa napanda kwa foleni, siku hizi imekuaje?
Mzee una subiri gari nusu saa nzima kituoni huoni hata dalili ni watu tu wanazidi kuongezeka unazani hiyo foleni ina kua na maana tena?
hawa wanao endesha mwendokasi walisha shindwa siku nyingi kuendesha huu mradi..
 
Mabasi yanayo fanya kazi ni machache ukifika kimara saa12 na nusu basi ikipakia kuiona tena n baada ya nusu saa unao ni dereva yule yule alie ondoka muda ule ulio fika hii ina ashiria gari hizo chache zinapeleka abiria mjini zina rudi tena kimara kupakia
 
Siku kukiwa na kiongozi ana fanya ziara pale mf. Mkuu wa mkoa ama maboss wa mwendokas utashangaa mabasi yana miminika tu ila wakisha ondoka hmmm tunarudi kule kule kwenye matatizo ya siku zote
-Magari machache
-Abiri wengi vituoni
-Basi hazifiki kwa wakati
-Foleni ina kua haina maana tena abiria wanapo kua wengi na walio subiri kwa muda mrefu ayo magari
mwendokasi mjitathmini
 
Yaani waingize daladala kwenye mwendokasi? We are not serious!
Nadhani haujamuelewa..
Alimaanisha Kuweko na daladala zinazoruhusiwa tumia Morogoro road kutoka mbezi kwenda kivukoni, morocco na gerezani moja kwa moja...
Kumbuka hakuna daladala zilizosajiliwa kutumia hiyo njia. Sio kwenye njia ya mwendo kasi, ila njia za kawaida ila routes hizo ndo hakuna kwa daladala

Yaani Mwendo kasi wamejiweka wenyewe wa kutoa hiyo huduma. ni kama imewanyima watu haki ya kupata huduma nyingine ilihali wao hawana uwezo .
Ukitaka pata usafiri wa umma mfano gerezani to mbezi inabidi upakie bajaji na ni elfu 4 had 5 mtu mmoja
 
Pale gerezani panafundisha ukomandoo na ukakamavu ukipazoea huwezi kuwa mtu wa kuendeshwa mpaka na kimbunga hidaya

Mi binafsi naona wapunguze mabus vurugu iongezeke tuwe maninja kabisa

Gerezan kimara
Sio lelemama
Jamaa ukinywa ngedule ujiniasi unazidi maradufu
 
nadhani hata wanaichi wenyewe yafaa kutumia busara, na hekima iwaelekeze kutumia usafiri mbadala wakati jambo hilo likitaftiwa suluhu ya kudumu🐒

madhara na athari zitawapata wao hakuna haja ya kulazimisha kwamba lazima upande mwendokasi, japokua ni hali ya kipato inachochea yote hayo 🐒
Sio kipato ni kwamba hamna route ya daladala Gerezani to kimara mbezi
 
Niliona uziwao humu mkuu hii hoja ya msingi sana ungeiweka pia pale kwenye uziwao
 
Last week ndugu yangu aliumia mgongo kwa kusukumwa akipanda Mwendokasi Kariakoo. Nilitoka Mwanza kwenda kumsalimia kisha nikaenda kujionea mazingira yaliyopelekea yeye kuumia.

Naomba niseme tu kwamba kwa hali ilivyo kituo cha Msimbazi na Gerezani sitashangaa kukatokea kifo.

Kwa namna watoto wanavyosukumwa na jinsi abiria wanavyogombania magari tutapata maafa.

Niwaombe viongozi wa Mwendokasi na viongozi wa serikali, itasikitisha sana kujitokeza kuomboleza vifo vya wanafunzi katika kituo cha Msimbazi, Kivukoni,Gerezani, DIT,Fire, Korogwe na Kimara. Naandika just kutoa taadhari nikitambua sikio la kufa alisikii dawa
Safi sana. Raia tunapogeuka na kuwa na akili kama za nyumbu, wacha yatupate!
 
Balaa zito la mwendokasi lipo hapa kimara
Wahusika wenyewe wamekaa pembeni abiria wanasukumana
 
Utakua mtu wa 1000 kwenye hiyo foleni na kutoka pale itakua usiku wa manane 🤣🤣🤣🤣 hii nchi inahitaji kuforce kila idara
Nimegundua za Morocco huwa hazina misukosuko ndio huwa napanda hizo.
 
Back
Top Bottom