Tahadhari kwa wakazi wa Arusha, ni kuhusiana na watendaji wasio waaminifu na wazembe kazini

Tahadhari kwa wakazi wa Arusha, ni kuhusiana na watendaji wasio waaminifu na wazembe kazini

ngaiwoye

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2014
Posts
2,150
Reaction score
3,225
Hivi karibuni vimeongezeka visa vingi vya uzembe, utovu wa nidhamu kazini, kunakofanywa na baadhi ya watendaji wa kata zilizopo Arusha.

KERO kuu ya kwanza kabisa, ni kuchelewa kufika ofisini bila sababu za msingi, jambo linalosababisha wananchi kushindwa kupata huduma kwa haraka na inavyopaswa.

KERO ya pili inahusu watendaji wa kata ambazo zipo pembezoni mwa miji, mfano kata ya Muriet na kata ya Terati, ambapo watendaji hawa wamegeuka kuwa madalali wa kuuza ardhi na viwanja. Hali hii imesababisha kutokuwepo kazini kwa muda sahihi na pia inachangia migogoro mikubwa ya ardhi.

Mara nyingi, watendaji wa mitaa haswa wa kata ya Terati muda wa kazi mara nyingi utawakuta mjini katika vijiwe vya madalali wakitafuta wateja wa kununua viwanja na mara kadhaa wamesababisha migogoro mikubwa sana ya ardhi.

Je serikali hufanya ufuatiliaji na kuhakiki ufanisi katika ofisi za watendaji zilizopo pembezoni mwa miji?? Mfano: yule anaevaa suti kila siku, hivi mtendaji wa kata na Mkurigenzi hua mnafatilia kwa karibu KERO za wananchi wenu na hii migogoro haswa ya ardhi inayosababishwa na ukanjanja wa watendaji dhaifu?

Rai yangu kwako mkurugenzi wa jiji PAMOJA na mkuu wa wilaya, hebu piteni mfanye ukaguzi na msikilize wananchi kwa sababu mpo hapo kuwatumikia wananchi.

Swala lingine ni uchafu uliokithiri kwenye baadhi ya maeneo mjini katikati. Kuna sehemu wamachinga wamerudi na ni sehemu hatarishi, kinachosikitisha ni wimbi la garage bubu pembezoni mwa barabara kuu, tena mjini katikati (kwa hili naomba Lobikoki ajitizame na ajitafakari kama anastahili hiyo nafasi).

Pia huko Muriet na Terati kuna madampo ya watu binafsi kwenye makazi ya watu, kwa kisingizio cha kurecycle chupa za plastics pamoja na vyuma chakavu. Haya maeneo ni machafu hatari, afya za wananchi zinahatarishwa na watendaji wapo wanaona (tetesi wanapewa mpunga) na bibi afya nao wapo.

Nakushauri mkurugenzi, haya madampo funga yote na yahamishiwe dampo kuu la jiji, mule ndani muwakodishie sehemu za kuchakata hayo mauchafu. Kwa kufanya hivyo mtaokoa afya za wananchi, mtaliongezea jiji mapato na pia mtadhibiti uchafu.

Haya ni kwa uchache sana.

Kataa watendaji dhaifu kwa ustawi wa jiji.

Kwa upendo mkubwa sana, habari hii iwafikie wizara ya Tamisemi, mkuu wa wilaya ( former tarafa) mh. Felician najua unafahamu Arusha vizuri, na ikufikie Mkurugenzi Chitukuro (wanangu wanakuitaga mzalendo)
 
Watendaji wa kata wamekua chanzo cha migogoro mingi ya ardhi na mbaya zaidi wakiharibu eneo moja wanahamishiwa eneo lingine ndiyo maana sio waoga kuendelea kufanya madudu.

Wananchi wasiojua haki zao wananyanyasika sana na watendaji wa namna hii especially kwenye migogoro ya ardhi.
 
Hivi hii kampuni ya Kambele ni ya mkubwa gani hapa mjini? Maana asee sio mara moja au mbili wanasababishaga migogoro ya ardhi, mf wanafoji nyaraka wanauza viwanja vya raia au kiwanja kimoja mara kadhaa, nasisitiza sio mara moja nimekutana nayo haya mamigogoro halafu viongozi wa kata hawana msaada rushwa rushwaaaaaaaa tupu siku hizi, Yaani mauozo yaliyopo Arusha asee ni noma, mama alisema kuwa uyaone Sasa na hili tukaliangalie nadhani
 
Ivi hii kampuni ya kambele ni ya mkubwa gan apa mjin? Maana asee sio mara moja au mbili wanasababishaga migogoro ya ardhi,mf wanafoji nyaraka wanauza viwanja vya raia au kiwanja kimoja mara kadhaa, nasisitiza sio mara moja nimekutana nayo haya mamigogoro alaf viongoz wa kata hawana msaada rushwa rushwaaaaaaaa tupu siku izi, Yaan mauozo yaliyopo arusha asee ni noma,mama alisema kuwa uyaone Sasa na hili tukaliangalie nadhani
Nimeshakutana sana na malalamiko ya huyu Kambele kwenye kuvamia ardhi za watu.
Huyu lazima anapewa jeuri na hawa watendaji njaa wanaoishi kwa kuuza ardhi za raiya.
Hapa dawa ni kushuhulika na mtendaji husika kwa kumreport kwa mkurugenzi aonyeshe anatua miongozo gani kufanya udalali tena wa kitapeli kwenye ardhi za watu.
 
Watendaji wa kata wamekua chanzo cha migogoro mingi ya ardhi na mbaya zaidi wakiharibu eneo moja wanahamishiwa eneo lingine ndiyo maana sio waoga kuendelea kufanya madudu.

Wananchi wasiojua haki zao wananyanyasika sana na watendaji wa namna hii especially kwenye migogoro ya ardhi.
Mfano mzuri ni hiyo kata ya Terat, ambayo ipo Arusha. Mtendaji wa kata na watendaji wa mitaa wote ni wazembe. Wala rushwa za waziwazi. Madalali wa viwanja na mashamba ya watu hivyo husababisha migogoro. Kibaya zaidi wameliweka kiganjani baraza la ardhi la kata, hivyo baraza hilo hutumika kuwakatisha ama kuumiza wananchi kwa kutokutenda haki pindi shauri likiletwa mezani ambalo watendaji hao wana maslahi binafsi.

Mtendaji Tumain Nchimbi ameishindwa kabisa kata hiyo, na ni mchelewaji namba moja wa ofisini, Mtendaji aitwae Mkama yeye ndio disaster, saa za kazi yeye unamkuta kwenye vijiwe vya madalali wa mashamba na viwanja, Ina maana mkurugenzi hujui wala hufahamu matendo ya huyu mtendaji mkama? Mtendaji aitwae Shabani sijui mara ya mwisho kwenda kazini ni lini. Wananchi wanakosa huduma sababu watendaji wamechelewa kazini, ofisini unakuta wanafunzi wa field ndio wamejazana.
 
Nimeshakutana sana na malalamiko ya huyu Kambele kwenye kuvamia ardhi za watu.
Huyu lazima anapewa jeuri na hawa watendaji njaa wanaoishi kwa kuuza ardhi za raiya.
Hapa dawa ni kushuhulika na mtendaji husika kwa kumreport kwa mkurugenzi aonyeshe anatua miongozo gani kufanya udalali tena wa kitapeli kwenye ardhi za watu.
Kambele ni matapeli na wanashirikiana na hawa watendaji wa kata na mitaa. Mfano huko east Afrika ambapo ni kata ya Terat na Muriet. Lakini migogoro mingi ya ardhi ipo kata ya Terat ambapo Hawa watendaji wanawasaidia hii kampuni na matapeli wengine kuiba ardhi za watu.

Watendaji hawa wamehodhi baraza la ardhi la kata, hivyo baraza hilo hufanya jinsi watendaji WANAVYOTAKA.

Ili wananchi wapone, mkurugenzi Hana budi kuchukua HATUA stahiki haraka.
 
Kwa kiandika na kipost ni rahisi sana kama unataka kujua utamu wa Ngoma ingia ukaicheze, swala la usafi ni issue mtambuka sana,machinga waliondolewa mjini lakini siasa ziliingia katikati machinga wameanza kurudi.Lobikok anajitaidi kadri anavyoweza ila changamoto,ukimnyanganya mzigo machinga anakimbilia Kwa wakuu ngazi za mkoa na wilaya, kuhusu madampo ya re-cyling ni kweli zinaanzishwa mtaani ila Bado zoezi la kuwaondoa kinafanyika.
 
Kwa kiandika na kipost ni rahisi sana kama unataka kujua utamu wa Ngoma ingia ukaicheze, swala la usafi ni issue mtambuka sana,machinga waliondolewa mjini lakini siasa ziliingia katikati machinga wameanza kurudi.Lobikok anajitaidi kadri anavyoweza ila changamoto,ukimnyanganya mzigo machinga anakimbilia Kwa wakuu ngazi za mkoa na wilaya, kuhusu madampo ya re-cyling ni kweli zinaanzishwa mtaani ila Bado zoezi la kuwaondoa kinafanyika.
Tatizo ni yule mke wa Lobikoki ambae ni bibi afya alikuwa hapo levolosi, anapewa hela na machinga na watu wanaofanya biashara pembezoni mwa biashara za watu, kisha akifika kwa mume wake ambae ni Lobikoki anakuwa hana namna zaidi ya kulinda tozo za mama Lobikoki ambae ni mkewe. Sasa hivi huyo mama kahamishiwa kaloleni. Lakini hapa mjini kati mama Lobikoki ana magoli kibao nae hukusanya tozo zake aka rushwa. Msimlaumu sana Lobikoki jaman, hilo tatizo kila mtu analifahamu kwamba mke wake ndio muhusika.
 
Kwa kiandika na kipost ni rahisi sana kama unataka kujua utamu wa Ngoma ingia ukaicheze, swala la usafi ni issue mtambuka sana,machinga waliondolewa mjini lakini siasa ziliingia katikati machinga wameanza kurudi.Lobikok anajitaidi kadri anavyoweza ila changamoto,ukimnyanganya mzigo machinga anakimbilia Kwa wakuu ngazi za mkoa na wilaya, kuhusu madampo ya re-cyling ni kweli zinaanzishwa mtaani ila Bado zoezi la kuwaondoa kinafanyika.
Lobikoki alikuwa hatoshi kwenye hiyo nafasi...mh mkuu wa mkoa Paul Makonda amehamisha wote waliokaa mda mrefu jiji akiwemo yeye..Lobikoki alikuwa hafai na alkuwa anaendeshwa na yule mke wake bibi afya MLA rushwa aliekuwa kata ya levolosi kwa muda mrefu Sasa kahamishiwa kaloleni
 
Lobikoki alikuwa hatoshi kwenye hiyo nafasi...mh mkuu wa mkoa Paul Makonda amehamisha wote waliokaa mda mrefu jiji akiwemo yeye..Lobikoki alikuwa hafai na alkuwa anaendeshwa na yule mke wake bibi afya MLA rushwa aliekuwa kata ya levolosi kwa muda mrefu Sasa kahamishiwa kaloleni
Vipi baada ya kuondolewa jiji limekuwa safi!?
 
Back
Top Bottom