Tahadhari kwa Watoaji wa Sadaka

Mifuko miwili ya cement iliyochanganywa na kokoto kidogo ikapigwa rangi we unaita ni mtakatifu?
Huyo jamaa anaonekana msomi. Mpaka apige magoti hapo, unafikiri hajui kwamba huyo ni mtakatifu. Halafu amekubali apigwe picha ya ukumbusho na magari yake mawili yamepaki pembeni.
 
Huyo jamaa anaonekana msomi. Mpaka apige magoti hapo, unafikiri hajui kwamba huyo ni mtakatifu. Halafu amekubali apigwe picha ya ukumbusho na magari yake mawili yamepaki pembeni.
Kipimo kinachoonyesha ni msomi mpumbavu ndo hicho kuomba toba mbele ya mifuko miwili ya cement
 
Pesa imesha kuwa ngumu bora nikabeti kuliko kumpa mwamposa
Uamuzi mzuri, lakini kubeti si ni sawa na kuruka majivu ukakanyaga makaa ya moto. Ungesema ukawekeze shambani ningekuunga mkono
 
Kipimo kinachoonyesha ni msomi mpumbavu ndo hicho kuomba toba mbele ya mifuko miwili ya cement
Ah, kanyaga pole pole, mkuu. Huyo amejifunza kutoka kwa wakuu wake wa dini. Wakuu wake wa dini kabla ya kuanza "utume" huwa wanasoma miaka mpaka tisa kwenye vyuo vikuu. Ukisema ni msomi mpumbavu unawatukana na wasomi waliomfundisha. Tafadhali bwana, acha maneno yako
 
Hujajiuliza kwanini Yesu hakutaja Acc number aliposema:
"...Lakini jiwekeeni hazina mbinguni, ambapo nondo na kutu haviharibu, wala wezi hawavunji na kuiba. Kwa sababu mahali hazina yako ilipo, hapo ndipo pia moyo wako utakapokuwa."
Umefunga pm mkuu
 
Hii nayo haipo kwa sasa, ila inalazimishwa tuu, walawi walikuwa wakohudumu siku zote kwenye hekalu la Mungu, wanafunzi wa yesu walikuwa wanafanya kazi na wanahudumu na yesu, wachungaji wa sasa wanakomaa na zaka kwasababu ya uvivu wa kufanya kazi. Kwenye makanisa Kuna watenda kazi wengi, wazee wa kanisa, wanakwaya, viongozi wa vikindi, mashemasi n.k kama vipi wote wapewe zaka.
 
Sawa Ntakuletea mifuko miwili ya cement na kokoto uwe unaiomba toba
 
Sawa Ntakuletea mifuko miwili ya cement na kokoto uwe unaiomba toba
Hiyo ni imani yake. Anao uhuru wa kuabudu. Kama una uhakika anakosea, badala ya kumcheka, msaidie kwa kumwandikia barua ya wazi(uzi maalum unaoelezea kwa kina hasara/madhara ya kuiomba ulinzi mifuko ya cement).

Mimi nimekuonyesha mfano. Badala ya kuweka picha za wanaotoa sadaka ya kujimaliza, nimewapa elimu wajue kuna matapeli wa kiroho. Tuko pamoja?
 
Ni sahihi ulivyosema. Jambo lingine ni kwamba kuna wahubiri wenye maagano na shetani ukitoa sadaka kwenye huduma zao unakuwa umeungamanishwa na mafhabahu za giza na maisha yako yanakuwa kifungoni.
 
Ni sahihi ulivyosema. Jambo lingine ni kwamba kuna wahubiri wenye maagano na shetani ukitoa sadaka kwenye huduma zao unakuwa umeungamanishwa na mafhabahu za giza na maisha yako yanakuwa kifungoni.
Duh! Kweli watu wanaangamia kwa kukosa maarifa.
Tuombe Mungu awafungue macho ya rohoni wasijiungamanishe na madhabahu za giza. Na tuzidi pia kuwafunulia Maandiko
 
Hii nayo haipo kwa sasa, ila inalazimishwa tuu,
Tukizingatia Andiko la Mathayo 23:23(NEN) bado ni sahihi kutoa zaka hata wakati huu wa Agano Jipya. Mstari huo unasema:

"Ole wenu walimu wa Torati na Mafarisayo, ninyi wanafiki! Kwa maana mnatoa zaka ya mnanaa, bizari na jira, lakini mmeacha mambo makuu zaidi ya sheria, yaani haki, huruma na uaminifu. Iliwapasa kufanya haya makuu ya sheria bila kupuuza hayo matoleo(zaka).

Wakati wa Agano la Kale watu walitoa zaka ili chakula kiwemo nyumbani mwa BWANA. Makuhani na Walawi wapate chakula ili waweze kufanya huduma.

Yesu alipokuja aliweka mkazo kwenye chakula cha kiroho(kazi ya Mungu)
Yohana 4:34 SRUV
"Yesu akawaambia, Chakula changu ndicho hiki, niyatende mapenzi yake aliyenituma, nikaimalize kazi yake."

Hivyo zaka inapaswa kutolewa hata wakati huu ili chakula alichosema Yesu kiwepo. Chakula hicho ni kuikamilisha kazi yake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…