Samahani sana kama hujui maana ya public goods uliza kwanza. Nini kazi ya kodi ya wazazi wa hao watoto kama wao wanatakiwa pamoja na kulipa kodi wajenge madarasa? Ni kwa siasa hizi hizi za kuwakandamiza raia na kutokuwaeleza nini haki yao katika serikali ndo maana rushwa haitaisha maana haki na favour hazitofautishwi nchini mwetu. Kwa mtu yeyote anaejali asingethubutu kutamka hayo maneno. Kama una moral standards jaribu kuona GDP ya tanzania inachangiwa na akina nani na je bila wao primary producers of goods je hizo jeuri zingetoka wapi? Wakati mwingine kua mstaarabu, bila kumumunya maneno MAFISADI NDO CHANZO cha halii hiyo no less no more.
Wee Felister,
Wala sipokei samahani yako. Naona na wewe uko katika kilema kilekile. Unafikiri ukishatoa kodi basi umemaliza kazi. Ndiyo maana tuna ukilema wa mawazo kwa kila kitu.
Kama ningeliupata ubunge wa eneo hilo, kabla sijapata fedha basi ningeliwahenyesha wanakijiji na mie mwenyewe siku nzima hadi tumalize hizo kuta na ndiyo niwaruhusu. Mie ningelifanya kazi bure na wao bure. Hayo ya hela za kodi ndiyo ningelifuatilia baadaye.
Mama, tafadhali sana. Nduguyo kijijini leo akianguka na kuzimia, utaita ambulance maana umetoa kodi. Isipofika, UTAKAA chini pwetee kusubiri hadi ifike. Kibaya zaidi unaweza kukuta ndiyo wanaisubiri ije kutoka German maana wametoa msaada. Na bandarini nako kitu hakitoki maana wafanyakazi wa TACT (Karamagi) wamegoma. Utasubiri sana hadi .......
Sijui kama umeshasafiri nchi wanazotoa kodi na kufuatilia hizo kodi. Siyo kweli kuwa kwa wazungu ukitoa kodi basi umemaliza kila kitu.
Nilishawahi kumtembelea Ngosha mmoja pale Stockholm (dr Sal. salamu zako) na akaniambia jambo lililonishangaza sana. Wakati wa winter, kwenye jengo lao (gorofa) ni kuwa ikianguka snow(barafu), ni kazi ya member wote kumwaga mchanga around hilo jengo na kuizoa hiyo snow. Mtu akipita hapo na akateleza na kuvunjika, basi member wote wanaoishi hapo, mtalipia gharama za matibabu. Na sweden gharama ya matibabu iko juu kinoma.
Kwa hiyo, hebu tupisheni na huu kupweteka kwenu kwa kusubiri kila kitu mje mfanyiwe na serikali ya matapeli na nyie wenyewe mnaKURA maraha. Watu wanakaa kwenye mitaro ya maji machafu, mvua ikinyesha watu wanatapisha vyoo, mifereji ya maji kila mwaka na hawawezi kujijengea kadaraja kadogo ili wasilowane. Mkisikia michango ya harusi, birthday, kitchen party na upupu mwingine, mnawahi ili MKARE BIA....... MIAFRICA.
Serikali ya KIFISADI ya Tanzania tumeshaisema sana. Kama tutaanza kubadilika na kufuatilia hali kama hizi, utakuwa mwanzo mzuri. Fisadi akija katika kijiji kama kile, anajua hapa ni ng'ombe na T-shirt, umechaguliwa. Akija na kukuta watu wamejitahidi kwa kutumia kila kilichopo ili kubadili maisha yao, basi hata FISADI atajua hapa kuna kazi kweli maana muamko uko juu.....
Sawa mama FISADI NDIYO CHANZO CHA KILA MATATIZO YA WATANZANIA. Nina amini kuwa TUKIUWA MAFISADI YOTE, basi TANZANIA ITAKUWA NI kama EUROPE. Kodi yetu itatupa kila kitu tunachotaka.
Is this not sounding like USSR era????? Ufanye kazi, usifanye kazi, UNALIPWA.