Taifa stars imeshinda, lakini haikustahili, imecheza ovyo sana

Taifa stars imeshinda, lakini haikustahili, imecheza ovyo sana

Niwapongeze stars Kwa ushindi wa bahati tu
Team imeshinda ila ndo hivo maajabu ya mchezo wa soka. Team dhaifu inaweza kushinda dhidi ya team Bora kabisa
Sisi tusiopumbazwa na ushindi wa ngekewa tunakosowa yafuatayo.

1 Eneo la goal keeper
Sio GK mzuri, hajui kuji position, Haiti mabeki yupo kimya.
Ni dhaifu kwenye kuanzisha mipira. Naiona nafasi ya Manula badala ya Ali Salim

2 Beki Lusajo ni dhaifu mno

Hana nguvu amekata moto mapema. Upande wake ulikuwa uchochoro Kocha aone uwezekano wa kumpa nafasi Paschal Msindo. Napendekeza Kapombe ajumuishwe kwa ajili ya uzoefu.

3. Feisal kafunga goli zuri sawa, lakini hakuwa bora kabisa
Nashauri coach amuanzishe bench

4. Balua kacheza vizuri, lakini imedhihirika yeye bado haya mashindano ya amzidi kiwango

5. Waziri JR, imeonekana daraja lake bado anatakiwa Mbwana Samatta

6. Zimbwe, Baca na Mwamnyeto kazi nzuri ni mabeki Bora kabisa

Nashauri coach awape vijana confidence, wamecheza ovyo, pasi hazifiki.

Physical hawapokei vizuri, waingie gym wafanye tiz la maana

NB: wanasiasa acheni shobo na kiki Kwa Taifa stars, Tunaweza kufuzu bila hamasa zenu fake

PIA SOMA: FT: Guinea 1-2 Taifa Stars | Kufuzu AFCON 2025 | Septemba 10, 2024| Charles Konan Banny Stadium
umeandika sawa kabisa,timu imecheza bila plan,haijulikani walikuwa wanafanya nini uwanjani,balua bado sana kuchezea taifa hafai hata chembe,kipa wetu ndio kituko,makocha wetu ni waganga wa kienyeji
 
umeandika sawa kabisa,timu imecheza bila plan,haijulikani walikuwa wanafanya nini uwanjani,balua bado sana kuchezea taifa hafai hata chembe,kipa wetu ndio kituko,makocha wetu ni waganga wa kienyeji
Unajua mpira mkuu
 
Kwa game ya jana taifa staz amestahili kushinda, alikua timu bora uwanjani tangu mwanzo wa mechi sana sana zile dakika zilizofuata baada ya kufungwa goli., wale Guinea ni kama walikua na papara, staz wangetumia vizuri nafasi wangefunga goli nyingi.

Udhaifu wetu mkubwa ni kutengeneza nafasi za kufunga, kuzitumia nafasi chacche tunazopata kwa ufasaha, pia suala la physique ni tatizo sehemu ya kutumia nguvu mara nyingi wachezaji wetu wanapoteza mpira.

Mabeki na viungo wanajitahidi kukinda na kumiliki mpira, tatizo lonaanzia pale kwa namba 10 na washambuliaji wa mbele yake hawana maarifa ya kupata goli
 
Mleta mada uko sahihi kabisa, mchezo uliochezwa na Stars jana wakikutana na timu iliyojiandaa watapigika sana. Kocha asibweteke na ushindi ajue kuna pa kufanyia kazi
 
Back
Top Bottom