Nimekuwa nikifuatilia michuano ya kombe la COSAFA inayoendelea mpaka sasa kule nchini AFRIKA KUSINI na hasa hasa mechi ambazo timu yetu ya TAIFA STARS (Kilimanjaro Stars) imekuwa ikicheza. Mungu jalia timu yetu imeweza ‘kufurukuta’ mpaka kufikia hatua ya nusu fainali japo kwa ‘mbinde’ na hii imetokana na wapinzani wetu tunaokutana nao ama kutokuwa wamejiandaa vya kutosha au waliamua kutuma vikosi dhaifu kwenye mashindano haya. Nisiwe mnafiki na mtovu wa nidhamu kwa kukosoa tu bila kutoa shukrani,nianze kwa kuwapongeza wachezaji wetu kwa kufikia hatua ya nusu fainali kwani hakuna mtu alitarajia hilo achilia mbali waandaaji wa mashindano waliotualika kama wageni "wachovu" .Nasema wachovu kwa kuwa pamoja na kualikwa ilibidi tupitie mchakato wa kucheza na timu ‘vibonde’ ili kuweza kufuzu hatua ya robo fainali na kukutana na timu kama Afrika Kusini, Namibia na Zimbabwe ambazo zilikuwa mapumzikoni zikisubiri vibonde wa kwenye makundi tutoane (sawa kuna baadhi ya watu watasema wachezaji wetu walichoka saana kutokana na "Fatigue" ya mechi za mfululizo tofauti na timu kama Afrika kusini na wengine tuliowakuta mbele laikini hii haiondoi mapungufu ya msingi yaliyopo kwenye timu yetu kama nitakavyo yaelezea hapo chini).Tuyaache hayo pamoja na kufanikiwa kufika hatua ya nusu fainali na hatimaye kushika nafasi ya tatu baada ya kuwafunga LESOTHO jana kwa mikwaju ya penalty ( kama ungekuwa unaugonjwa "pressure " usingeangalia dk.90 zote au ungekuja kuambiwa baadae mpira umeisha kwa timu zoote kutoka bila kufungana usingeamini, shukrani zimuendee golikipa wa timu ya TAIFA stars aliedaka jana SIO Manura… Kwa kifupi timu yetu imeonyesha kiwango kibovu kupita kiasi pengine cha chini kuliko hata timu tulizozifunga kama Afrika Kusini...Malawi....
Yafuatayo ni mapungufu niliyoyaona na kama hayatafanyiwa kazi basi tutaendelea kuwa kichwa cha mwendawazimu mpaka atakaporudi Mtume au Yesu.
Wachezaji wetu karibia woote (98%) hawaelewi nini wanatakiwa kufanya wanapokuwa uwanjani..hakuna malengo,wachezaji wanapapara mtu akipewaa pasi anaanza kutetemeka kabla ya kupokea mpira ‘by the time’ mpira unapomfikia ‘either’ utamgonga au atatoa pasi butu.
Kadiri wanavyozidi kusogelea lango la wapinzani (kutokana na papara) ndivyo wanavyozidi kupoteza umakini (wasiwasi mwingi).
Stamina ni tatizo kubwa (stamina sio lazima kuwa na mwili mkubwa nieleweke) tatizo la wachezaji wetu mchezaji akifanikiwa kupiga chenga ya kwanza kinachofuata ni kuanguka na mpira mwenyewe (mfano.Msuva, Kapombe na Kichuya) na wengine wengi.
Sikuona mkakati wa mwalimu wakati wa mechi kufanya mabadaliko kadiri mpira unavyobadirika (badiriko wanalolifanya ni kukariri aanze Msuva badae aingie Ulimwengu) au Msuva awe anabadirishana na Kichuya (rotation) kwa wingi ya kushoto na kulia Jambo ambalo mchezaji haitaji kufundushwa na Mwalimu.
Kati ya mambo yaloniumiza saana pamooja na timu kuwa mbovu ni kuona wachezaji ambao wamekuwa wakisifiwa saana kwenye ligi ya Vodacom kwa matarumbeta (Kichuya na msuva) wakionyesha kiwango cha chini kabisa kuanzia katika umiliki wa mpira,kufanya maamuzi (papara nyingi) kutoa pasi bila malengo. N.k...nikajiuliza hivi ndio hawa tunaowasikiaga wamazifunga Yanga na Simba?..Kwa ufupi hali ni mbaya saana kupita kiasi yaani kama ningekuwa napewa nafasi ya kuchagua timu kwa hawa wa sasa ningewatimua woote labda kutokana na changamoto ya mashindano yanayotukabiri kwa sasa hivi karibuni ningewabakiza Maguri,Mkami (kapteni),Yasini, Erasto ,Nyoni, beki number tatu sijui sudi au said, Mbwana Samatta, Ulimwengu (nkimtazama kwa jicho la ndani) na Kipa wa jana sio Manura.
Wadau haya ni maoni yangu kama mdau wa soka anayefuatilia soka kwa siku nyingi natumai wadau mtaniunga mkono japo sio lazima kwa kila mtu kuwa na maoni kama yangu lakini ukweli ndio huo natamani hii makala isomwe na Baraza la Michezo au Waziri wa Miichezo kwa kuwa najua TFF kwa sasa hakuna mtu mwenye ‘moody’na hivi vitu watu wanawaza chakula yao… Mwisho naomba Wizara ifuatilie malipo ya zawadi waliopata wachezaji jana isije ikaishia kulipia mawakili wa Kesi za TFF…
Yafuatayo ni mapungufu niliyoyaona na kama hayatafanyiwa kazi basi tutaendelea kuwa kichwa cha mwendawazimu mpaka atakaporudi Mtume au Yesu.
Wachezaji wetu karibia woote (98%) hawaelewi nini wanatakiwa kufanya wanapokuwa uwanjani..hakuna malengo,wachezaji wanapapara mtu akipewaa pasi anaanza kutetemeka kabla ya kupokea mpira ‘by the time’ mpira unapomfikia ‘either’ utamgonga au atatoa pasi butu.
Kadiri wanavyozidi kusogelea lango la wapinzani (kutokana na papara) ndivyo wanavyozidi kupoteza umakini (wasiwasi mwingi).
Stamina ni tatizo kubwa (stamina sio lazima kuwa na mwili mkubwa nieleweke) tatizo la wachezaji wetu mchezaji akifanikiwa kupiga chenga ya kwanza kinachofuata ni kuanguka na mpira mwenyewe (mfano.Msuva, Kapombe na Kichuya) na wengine wengi.
Sikuona mkakati wa mwalimu wakati wa mechi kufanya mabadaliko kadiri mpira unavyobadirika (badiriko wanalolifanya ni kukariri aanze Msuva badae aingie Ulimwengu) au Msuva awe anabadirishana na Kichuya (rotation) kwa wingi ya kushoto na kulia Jambo ambalo mchezaji haitaji kufundushwa na Mwalimu.
Kati ya mambo yaloniumiza saana pamooja na timu kuwa mbovu ni kuona wachezaji ambao wamekuwa wakisifiwa saana kwenye ligi ya Vodacom kwa matarumbeta (Kichuya na msuva) wakionyesha kiwango cha chini kabisa kuanzia katika umiliki wa mpira,kufanya maamuzi (papara nyingi) kutoa pasi bila malengo. N.k...nikajiuliza hivi ndio hawa tunaowasikiaga wamazifunga Yanga na Simba?..Kwa ufupi hali ni mbaya saana kupita kiasi yaani kama ningekuwa napewa nafasi ya kuchagua timu kwa hawa wa sasa ningewatimua woote labda kutokana na changamoto ya mashindano yanayotukabiri kwa sasa hivi karibuni ningewabakiza Maguri,Mkami (kapteni),Yasini, Erasto ,Nyoni, beki number tatu sijui sudi au said, Mbwana Samatta, Ulimwengu (nkimtazama kwa jicho la ndani) na Kipa wa jana sio Manura.
Wadau haya ni maoni yangu kama mdau wa soka anayefuatilia soka kwa siku nyingi natumai wadau mtaniunga mkono japo sio lazima kwa kila mtu kuwa na maoni kama yangu lakini ukweli ndio huo natamani hii makala isomwe na Baraza la Michezo au Waziri wa Miichezo kwa kuwa najua TFF kwa sasa hakuna mtu mwenye ‘moody’na hivi vitu watu wanawaza chakula yao… Mwisho naomba Wizara ifuatilie malipo ya zawadi waliopata wachezaji jana isije ikaishia kulipia mawakili wa Kesi za TFF…