Zinazile
Senior Member
- Sep 11, 2020
- 116
- 126
Habari zenu watanzania wenzangu, jioni hii kuna mechi ya kusaka ticket ya kushiriki AFCON 2023 kati ya Team yetu ya Taifa( Taifa Stars) na team ya Taifa la Niger, mpaka muda huu kila team imepata goli, wawakilishi wetu walikuwa wa kwanza kupata goli kunako dk ya 2 na Niger wakasawazisha baada ya dk kadhaa. Wafungaji wa mabao kwa team zote sijapata bahati ya kujua ni akina nani kwani nasikiliza kwenye radio na nimekuta mechi imeanza hata line up kwa team zote sijasikiliza, kama kuna mtu anajua ni channel gani inaonyesha live anisaidie ili niweze kuangalia.
Naomba watanzania wenzangu tuendelee kuwatakia kheri wawakilishi wetu ili watuwakilishe vema, Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Taifa Stars
Up date: Mpira mpaka sasa ni mapumziko team zote zikiwa sawa kwa 1- 1 goli la Taifa Stars likifungwa na George Mpole wakati goli la kusawazisha kwa wenyeji Niger likifungwa na Adebayor
FT : 1-1
Mungu ni mwema tumeambulia point 1 ugenini, ahsanteni kwa maombi
Naomba watanzania wenzangu tuendelee kuwatakia kheri wawakilishi wetu ili watuwakilishe vema, Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Taifa Stars
Up date: Mpira mpaka sasa ni mapumziko team zote zikiwa sawa kwa 1- 1 goli la Taifa Stars likifungwa na George Mpole wakati goli la kusawazisha kwa wenyeji Niger likifungwa na Adebayor
FT : 1-1
Mungu ni mwema tumeambulia point 1 ugenini, ahsanteni kwa maombi