Taifa Stars wanaoenda Cape Verde wachezaji kutoka Zanzibar wamo?

cutelove

JF-Expert Member
Joined
Oct 3, 2017
Posts
3,448
Reaction score
7,972
Nauliza tu ,Taifa Stars wanaoenda Cape Verde au waliocheza na Uganda imejumuisha wachezaji wa Zanzibar ili ule uwakilishi wa Kitanzania uonekane

Wakati Taifa Stars wakiwa uwanjani vibao vya matangazo vitakuwa vimeandikwa

Cape Verde Vs Tanzania

Je Zanzibar iko upande gani?

CAF ilitupilia mbali maombi ya Zanzibar kuwa na timu ya Taifa kwenye nchi moja ya Tanzania

Je wazanzibar wapo upande gan?
 
Km stakosea cuf wanaitambua Zanzibar ila FIFA haitambui Zanzibar inaitambia Tanzania
 
Wapo,mmojawapo in Fei Toto was Yanga...kimsingi FIFA walishatengua ile nafasi waliyopewa Zanzibar kuwa mwanachama was Caf.....hivyo Zanzibar sio mwanachama was Caf kwa maana sio nchi mkuu.....Zanzibar wanabaki kwenye Cecafa tu
 
Wachezaji wa timu ya taifa wanaweza wakatoka hata kwenye kijiji kimoja, ilimradi tu wafanye vizuri...
Tuacheni siasa kwenye mambo ya msingi.
Toa jibu la kueleweka! Hajaongea siasa,ameuliza swali! Kama una jibu sahihi jibu
 
Toa jibu la kueleweka! Hajaongea siasa,ameuliza swali! Kama una jibu sahihi jibu
Kipi kigumu hapo? Zanzibar ni sehemu ya Tanzania kama ilivyo maeneo mengine/ mikoa mingine. Sasa kama waliopo huko viwango vyao haviwafikii wa ukanda mwingine unataka wachezeshwe hivyo hivyo ili wacheze hovyo halafu muanze kuzomea. Au mnatakaje?
 
Aggrey Morris ni Mzanzibar
Feisal Salum ni Mzanzibar
Kama sikosei hata Mudathir Yahaya.

Lakin wachezaji wa taifa stars wanatakiwa kuwa na viwango bora pasipo kujali wanatokea wapi mradi tu wawe raia wa Tanzania.
Upo sahihi, hata kama timu nzima ingetokea Rukwa ilimradi wamekidhi viwango, nakazia tu!
 
Fei toto
Mudathri
Aggrey moris
Tucheze mpira twende afcon
 
Tanzania = Tanganyika + Zanzibar
Mchezaji yoyote kutoka sehemu hizo ana haki kucheza taifa stars, hata kama wachezaji wote wakitoka upande mmoja (tanganyika/zanzibar), kikubwa wakidhi viwango.
 
Aggrey Morris ni Mzanzibar
Feisal Salum ni Mzanzibar
Kama sikosei hata Mudathir Yahaya.

Lakin wachezaji wa taifa stars wanatakiwa kuwa na viwango bora pasipo kujali wanatokea wapi mradi tu wawe raia wa Tanzania.
Himid Mao, Shaaban Chirunda
Wanaweza kuwa wengi zaidi, huwa inategemea sehemu walikochukulia paspoti ingawa m-zanzibar anaweza kuchezea Kilimanjaro Stars ila wa Bara hawezi kuchezea Zbar Heroes.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…