Taifa Tanzania lapinga sababu 51 za Kikwete kutogombea 2010!

Taifa Tanzania lapinga sababu 51 za Kikwete kutogombea 2010!

Tunaanza na sababu 3:

Rais Kikwete amekuwa mstari wa mbele wa kutaka kuwepo utawala wa sheria. Utawala wa sheria ndiyo msigi mkuu wa utawala wa kidemokrasia, Tanzania ni nchi mojawapo miongoni mwa nchi changa kuwa na asasi zenye mamlaka zinazofanya kazi kwa uhuru kamili.

Tumepata uhuru tangu mwaka 1961, sasa huo uchanga wa Tanzania unatoka wapi? mimi naona huyu aliyetoa haya majibu hajui alifanyalo.
 
amka2.gif

KATIKA utafiti na mijadala yangu na makada kadhaa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), nimegundua mambo mawili ya msingi.
Kwanza, wana-CCM wenyewe, wakiwamo makada waandamizi, wanakiri kwamba chama chao kimechafuka na kimeathirika sana kisiasa.
Wanasema chama chao kimeshuka umaarufu kwa umma, hakina mvuto; na kwamba kama nchi hii ingekuwa na mfumo wa uchaguzi ulio huru na wa haki, CCM isingechaguliwa tena.
Lakini hawayasemi haya katika vikao rasmi. Hawayasemi hadharani, bali katika mazungumzo ya kawaida, lakini yanayotoka mioyoni mwao. Wanasema kweli.
Wanajua kwamba wananchi wameichoka CCM. Lakini faraja waliyo nayo ni kwamba wanahisi watachaguliwa tena mwakani kwa sababu vyama vya upinzani havijaweza kujipenyeza kwa nguvu za kutosha na kukita mizizi katika vijiji, mitaa na vitongozi vyote nchini.
Wanajua kuwa vyama vya upinzani havijulikani kama CCM. Na kwa kuwa nchi hii haijawahi kutawaliwa na chama kisicho TANU au CCM, wananchi hawajafikishwa mahali pa kuona kwamba wasio katika CCM wanaweza kushika dola na nchi ikatawalika vema. Kwa hiyo, faraja hii ya wana-CCM imejijenga katika ujinga wa umma na unyonge wa upinzani. Lakini wanajua pia si kwamba vyama vya upinzani ni vinyonge kuliko CCM.

Tofauti kubwa ya sasa kati ya CCM na vyama vya upinzani vinavyoonekana (CHADEMA au CUF) ni kwamba CCM imeshika dola; inatumia kodi ya wananchi kuwanyanyasa wananchi wanaoipinga na hata wanaoiunga mkono serikali. Siku ikipoteza nguvu za dola itakuwa chama dhaifu kiasi cha kukosa hata wabunge 10 nchi nzima.
Niliwahi kusema haya huko nyuma, na sasa nasisitiza tena. Yaliyotokea kwingine, Kenya na Zambia, kwa mfano yatatokea hapa kwetu. Nguvu ya UNIP ya Kenneth Kaunda na KANU ya Daniel arap Moi, ilinyauka ghafla na kutoweka siku ile ile vyama hivyo vilipoondoka Ikulu. Jeuri ya watawala iligeuka kuwa unyonge usiomithilika. Vyama hivyo sasa vinaishi nje ya Ikulu, vikiwa katika homa ya uchaguzi na kivuli cha kifo cha kisiasa.

Kwa mantiki hiyo hiyo, CCM isiyoshikilia Ikulu, haiwezi kuwa na ubavu wa kivibeza vyama vingine, kwa sababu yenyewe ni dhaifu zaidi. Lisilojulikana kwa mtu yeyote sasa ni lini CCM itaondoka madarakani, lakini dalili zinaonyesha kwamba siku hiyo haiko mbali.
Maana kama walivyo wana-CCM wetu hawa, wana-KANU na wana-UNIP walikuwa wanajiamini kwamba wangetawala milele.
Hadi siku ya uchaguzi uliowaondoa madarakani, waliamini kwamba wangeshinda wao. Sababu ilikuwa moja tu – mazoea. Hawakuwahi kushindwa kabla ya hapo, hasa kwa kuwa mifumo ya uchaguzi ilikuwa inaendeshwa na wao, na iliwapendelea wao.
Lakini kwa kuwa walishachokwa na umma, walishakosa mvuto, walifanya siasa za kutumia nguvu za dola kuliko ushawishi wa itikadi, sera na utendaji adilifu na makini; waliwachimbia wapinzani kaburi lenye kina kirefu mno, wakatumbukia wao. Sasa inawawia vigumu kutoka!
Huko ndiko CCM inakoelekea. Wanaoamini katika mazoea kwa kuwa hawajawahi kuona upinzani unatawala, hawaelewi ninachosema.
Wanaodhani upinzani ni dhaifu kwa kuwa hawajui kuwa nguvu ya sasa ya CCM ni matumizi ya dola, wanaweza kubeza hoja yangu hii.
Lakini walio makini, hata viongozi wenyewe wa CCM, wanajua ukweli wa hoja hii. Ndiyo maana wanafanya kila jitihada kuhakikisha CCM inabaki madarakani kwa kuzingatia na kutekeleza suala la pili nililogundua na ambalo sikubaliani nalo. Nalo ni kwamba, mtu pekee wa kuivusha CCM 2010 ni Rais Jakaya Kikwete.

Wanadai kwamba CCM hakikubaliki mbele ya umma, lakini bado inaweza kuchaguliwa kwa sifa za mgombea anayekubalika. Wanadai Rais Kikwete anakubalika.
Na hawasemi kwamba Kikwete hana udhaifu. Wanakiri kwamba amekuwa kiongozi dhaifu kuliko wote waliomtangulia. Lakini amefanikiwa kujenga umaarufu binafsi kwa muda mrefu, na kuwafanya watu wampende na kumwonea huruma hata kama ameshindwa kazi.
Lakini kwa chama kutegemea kibebwe na mtu aliyeshindwa kazi, ni kuishi kwa matumaini yanayofananishwa na ramli ya kisiasa. Bahati nzuri yao, vyombo vya habari na taasisi kadhaa za utafiti nchini vimetumika kisiasa kueneza propaganda kwamba rais anafanya kazi nzuri tu, bali anaangushwa na wasaidizi wake.

Vyombo hivyo hivyo vimeshindwa kutufafanulia rais anafanya kazi kwa kutumia nyenzo gani na watu gani. Vimeshindwa kutwambia kwamba udhaifu wa mawaziri wenyewe unatokana na uteuzi mbaya unaofanywa na rais.
Vimekataa pia kutueleza kwamba hata akishawateua, wanapofanya vibaya na ‘kumharibia’ anakosa kabisa uwezo wa kuwachukulia hatua. Je, ni sahihi kumsifia kiongozi anayeshindwa kufanya uteuzi mzuri wa wasaidizi na washauri wake, na badala yake tukawalaumu washauri wake?
Bahati mbaya, kazi hii imekuwa pia sehemu ya majukumu ya kihuni ya watumishi wetu wanaotambulika kama mashushushu au makachero.
Badala ya kutumika kusambaza taarifa muhimu za kuliokoa taifa, wamekuwa wanatumika sana kusambaza na kufuatilia taarifa za kutunga za kumsaidia mtu mmoja ambaye udhaifu wake wa kiuongozi ndiyo sababu kuu ya nchi hii kuporomoka na kudoroa kiuchumi; kuibuka kwa makundi hasimu ndani ya chama tawala na serikali, na kulifikisha taifa mahali pa kukabiliwa na ombwe la uongozi.
Naamini kwamba kama vyombo hivi vya habari na usalama wa taifa vingekuwa vinajali taifa katika uzito unaokubalika; kama vingekuwa vinaona masilahi ya umma katika maisha ya wanyonge na maskini wa nchi hii; kama vingekuwa vinaona madhara ya ufisadi kwa taifa, na vikatambua kuwa watawala ndio wamekuwa vinara na walezi wa ufisadi huo, visingetumia rasilimali zetu kuwalinda.
Sana sana vingewashauri wabadilike au vingesambaza na kufuatilia taarifa za kuwadhoofisha na kuwaondoa, huku vikijenga mazingira ya kuwawezesha wengine wenye nguvu kuchukua nafasi ya walio dhaifu.
Na hata pale ambapo washauri wa rais wameonekana kushindwa kazi au hata kumpotosha, vyombo hivi ndivyo vingetumika kumshauri kiongozi mkuu mwenyewe, na hata kumlazimisha kuchukua hatua kali kulinusuru taifa.
Si tu kulinusuru taifa bali hata kumnusuru yeye binafsi hata kwa kumwambia aachie ngazi kwa heshima kabla mambo hayajaharibika ili taifa liweze kupiga hatua. Si jambo la kujivunia kama vyombo hivi vya habari na usalama wa taifa vinatumika kujenga, kutetea na kusimika udhaifu wa viongozi badala ya kuuondoa; huku vikifanya jitihada za kuwadhoofisha na hata kuwaondoa walio na nguvu ambazo taifa hili linazihitaji kupiga hatua ya kimaendeleo.

Vyombo hivi, kama vingesimamiwa kitaalamu na kizalendo, ndivyo vingetusaidia kuubomoa mfumo mkongwe wa utawala wa nchi hii. Vingetusaidia kuwabomoa watawala wabovu na kuwashauri wapumzike kabla mambo hayajaharibika zaidi.
Vingesaidiana na wananchi wenye nia njema na taifa hili kujenga na kusimika mfumo mpya unaoendana na enzi hizi za karne ya 21.
Kwa maana nyingine, udhaifu wa makusudi wa vyombo hivi ndio unawafanya makada wa CCM leo waone kwamba ingawa kiongozi wao ni dhaifu na hakubaliki kama zamani (kwa sababu za kujitakia), bado anaonekana kuwa ndiye pekee anayeweza kukibeba chama chake kushinda uchaguzi mkuu.
Maana mantiki inakataa. Kama tumekwama kwa sababu ya kukosa uongozi madhubuti, inawezekanaje tufikiri na kukubali kwamba hao waliotukwamisha ndio wanaostahili kushinda tena katika uchaguzi? Kwanini tuwang’ang’anie walioshindwa?
Inawezekanaje, kwa mfano, kwamba ndani ya CCM hakuna mwanachama anayekubalika, anayeuzika na mwenye uwezo wa kuongoza nchi kuliko Jakaya Kikwete?
Yaani, kama Rais Kikwete (kwa utendaji huu wa miaka minne) ndiye taswira halisi ya uwezo na mafaniko ya CCM, tutakuwa waongo tukisema chama kimeishiwa talanta za uongozi? Kama huyu ndiye sampo wa viongozi bora wa CCM, na ndiye pekee anayeweza, tutapata wapi maneno makali zaidi ya kuwatukana watu makini ndani ya CCM?
Je, tutakuwa na makosa gani tukisema inatosha, tutazame kwingine? Kama CCM haina mgombea mwingine mwaka 2010, wakati makada wake wakikiri kwamba chama chao kimekosa mvuto kwa umma, tunakuwa tunalitendea haki taifa hili kumng’ang’ania aliyeshindwa aendelee kutawala, hata kama yeye anataka?
Jambo moja ni dhahiri. Kinachowafanya wengi wao wajipendekeze kwa rais ni unafiki binafsi na kujipendekeza. Wanaogopa mamlaka yake ya kikatiba kitaifa na katika CCM, maana ndiye kiongozi wa vikao vikuu vya maamuzi makubwa yanayohusu pia masilahi yao binafsi kisiasa.
Na wanajua kuwa wanapokuwa na mgombea ambaye yuko madarakani, atatumia nguvu zote za dola kujipa ushindi kupitia mifumo ile ile inayoandaa na kuratibu uchaguzi. Wanataka ushindi hata kama hawana mkakati wa kuutumia kuleta maendeleo ya taifa.
Lakini kama wanakiri kwamba wameshindwa kazi, na kama wanaamini kwamba chama kina hazina kubwa ya talanta za uongozi, kuna ubaya gani wakaanza mchakato rasmi na usio rasmi wa kupata uongozi utakaolikwamua taifa hili kutoka kwenye lindi la maradhi, ujinga, umaskini na ufisadi? Kama wana-CCM wanaipenda nchi hii, kwanini wanakosa ujasiri wa kusema ukweli daima (kama kanuni yao mojawapo inavyosema), wakatusaidia kutafuta mbadala wa Kikwete katika chama chao? Lakini haya yote yanaleta ujumbe mwingine mzito kwa taifa. Enzi za kutawaliwa na CCM zimekwisha. Na kama enzi za CCM zimekwisha kwa nini tusishirikiane sasa kutafuta mbadala wa uongozi wa kitaifa nje ya CCM? Au bado tunadhani haiwezekani?
 
Sijaona hiyo article ya Mwanakijiji kwa hivo nitaongea kutokana na kilicholetwa katika hii reply.

Kikwete mwenyewe amesema kwamba 70% ya Watanzania ni bendera kufuata upepo, huyu ndiye rais anayeshabikiwa?

Labda amesema kweli, maana wangekuwa si bendera kufuata upepo wasingemchagua yeye.Hapa kuna hao bendera kufuata upepo na wale wanaolinda/ kutafuta maslahi binafsi kwa kujikomba kwa wakubwa, style iliyowatoa kina Kikwete na Makamba.

Mwandishi anamsifia Kikwete kwamba amepitia tanuru la moto kwa kushindanishwa na magwiji kama vile Tanzania tuna system ya meritocracy na Kikwete kashinda on the merit (merit gani?).Tunajua Tanzania uongozi wa juu haufuati meritocracy, bali kuna Machiavellianism tupu na Kikwete was simply the best courtesant at stabbing his opposition in the back with a dagger and better at obtaining illegal funding.

Ndiyo maana nikasema rais ajaye atakuwa mbaya kuliko Kikwete kwa sababu system yetu haijakaa kum reward mtu mwenye uwezo na track record (meritocracy) ila the best deceiver kama Kikwete.

Mtu wa kwanza anayejikomba ni Dr Bana wa REDET
 
Binafsi mimi sio mwandishi wa habari kitaaluma lakini naona habari yenyewe haijatulia kabisa. Kichwa cha habari kinazungumzia kujibu hoja za Mwanakijiji,halafu unayejibu unasema kwamba unaitwa mwandishi wetu, huo ni undishi wa habari wa mwaka 47 kwanza unaogopa nini kujitambulisha wakati unatetea dola kama sio unafiki?

Jitambulishe watu tukufahamu,tukusifie,tukukosoe kama kweli habari na hoja unazopingania ni za kweli.
 
Wadau, mchomeko wa mada nyingine kwenye Taifa Tanzania inayohitaji kujadiliwa.

TUNAMJIBU M.M. MWANAKIJIJI:

Sababu 102 kwa nini Jakaya Kikwete agombee 2010 na aendelee kuongoza

MWANDISHI WETU

Wana CCM milioni 4 (kasoro Nungayembe wa kisiasa) na wapiga kura kwa mamilioni, wanatambua uongozi wa Rais Jakaya Kikwete. Hao waliopiga kura katika Uchaguzi Mkuu 2005, pamoja na wapiga kura wapya tuna hakika, hawajaona au hawategemei kuona mbadala kwa nafasi ambayo Kikwete anayoishikilia. Kwa nini tunaona hivyo?

Hali iliyopo kwa watu wanaofanya shughuli zao za kuzalisha mali na katika kujenga taifa inaridhisha tofauti na ramli za kutabiri mwisho wa dunia ya Tanzania yenye amani zinazopigwa na baadhi ya vyombo vya habari.

Kuna kundi dogo la watu ambao wana nongwa ya kuukosa Urais 2005 na wengine ambao hawana uwezo wa kuchambua matukio, michakato na mienendo ya kisiasa na kijamii wanaendeshwa na kuamini katika hisia zao, ambazo zinawatuma kuandika vitu vya kubuni na alnacha.

Walipofanikiwa kumg'oa Edward Lowassa hawakuridhika. Wamekuwa wakijidanganya kwamba wanaweza kutimiza ndoto yao ya kumng'oa na Kikwete na kuzika kizazi hicho cha uongozi. Katika Gazeti la Mwanahalisi, toleo Na. 167 Jumatano Desemba 16-22, 2009 makala ya M.M. Mwanakijiji (sababu 51 za kumkwamisha Kikwete) mwandishi anaonyesha alivyokosa cha kuandika, akalazimisha hoja na sababu kwa nini Rais Kikwete asigombee nafasi ya Urais mwaka 2010.

Kwanza kabisa hakuna mwanachama ndani ya CCM anayeweza kutaka kugombea na akawa tishio kwa Rais Kikwete. Kikwete alishapitia tanuru la moto mwaka 1995 na 2005.

Hakuna watu wenye nguvu na uwezo wa kila hali ambao wanaweza kujitokeza sasa kuliko wale ambao aliishashindana nao huko nyuma. Majina ya akina John Samwel Malecela, Frederick Sumaye, Profesa Mark Mwandosya, Cleopa Msuya, Benjamen Mkapa, Jaji mstaafu Mark Bomani, Salim Ahmed Salim na mengineyo ni majina makubwa. Alishindana nao na akawashinda.

Kikwete kugombea Urais siyo kwa maslahi ya wapambe, kuna mambo makubwa zaidi ya wapambe ambayo yanamfanya mtu agombee nafasi kuu ya Urais. Tamaa ya mtu katika nafsi yake kutaka kugombea uongozi ni kwamba ana uwezo fulani na anataka atekeleze mambo fulani nje ya nafsi yake. Wako watu wengi katika uwanja wa siasa ambao hawafikii hatua hiyo.

Ukweli wa mambo ni kwamba tangu achukue madaraka 2005, mambo mengi yamekuwa yanafanyika hapa nchini. Miradi imekuwa inatekelezwa na serikali watu katika sekta binafsi, mashirika makubwa ya kimataifa na mashirika ya kidini. Kusema kwamba wanaotaka Kikwete agombee ni wale ambao wanakariri kikasuku msemo wa "kuendeleza umoja, utulivu, amani na mshikamano" wa nchi yetu, ni fikra za mtu ambaye akili yake imedumaa na kukwama kutokana na kutotaka kujifunza mabadiliko yanavyotokea katika mazingira na nani analeta mabadiliko hayo.

Kwa upande mwingine dhana ya utulivu wa kisiasa (political stability) imepitwa na wakati. Wanataaluma na watunga sera, sasa hivi wanazungumzia utulivu utokanao na mkusanyiko wa sababu mbalimbali za maendeleo katika sekta za uchumi na ustawi wa jamii (structural stability). Kwamba watu hawali maneno matupu na nadharia za siasa.

Utulivu kimfumo una nafasi kubwa kutokana na sekta mbalimbali kutegemeana ili kuleta maendeleo yenye ulinganifu, hivyo ni wazi kwamba sera zote zinazotungwa na miradi inayotekelezwa inakuwa imepangwa kimtambuka kiasi kwamba yanayotokea sekta moja yanaathiri maendeleo yatakavyokuwa katika sekta nyingine.

Kwa namna moja au nyingine watanzania walio wengi katika sekta mbalimbali wanaguswa na kufikiwa na miradi ya maendeleo ya kubadilisha maisha yao . Yawezekana kwamba kasi ya maendeleo inazidiana. Lakini kwa namna moja au nyingine kuna mabadiliko ya msingi kule wanapoishi watu.

Watu wasioelewa hali inavyobadilika wanakuwa wa kwanza kupiga mayowe jinsi serikali ilivyoshindwa kuwaletea watu maendeleo, bila kutambua ukweli wa mambo kwamba watu wenyewe ndiyo watajiletea maendeleo na kazi hiyo ndiyo wameshaianza. Kwa waandishi wapiga ramli, kwa sababu wanataka kuonyesha msimamo wao wa "kupinga kila kisemwacho au kufanywa na hasimu wao", wanakuwa na watu wao ambao wanawaumba na kuwatengenezea mazingira.

Wanapoanzia siyo kuonyesha uwezo wa kiongozi wao wa kufikirika bali ni kubuni na kuzua mambo, na kujaribu kugeuza mkondo wa maji utoke ziwani na kupanda mlima. Kwa hili la Kikwete kugombea 2010 tunasema binadamu ana uwezo mkubwa, lakini hawezi kuzuia jua kuchwa!

Katika jamii inayokua kwa misingi ya kidemokrasi wapiga kura na raia kwa ujumla wana nafasi yao katika mchakato wa siasa, uchumi na maendeleo ya jamii. Nchi inaweza ikawa katika matatizo makubwa ya kiuchumi lakini hakuna matukio ya uvunjivu wa sheria wa makusudi kutoka kwa watu wengi. Tanzania ilipitia vipindi vigumu ambapo uchumi wa nchi ulikuwa mbaya. Hakuna fujo zilizotokea ambao zilitishia usalama wa watu na mali zao.
Kuna sababu 102 ambazo tunaona kwa nini Rais Kikwete agombee Urais 2010. Tutazitolea maelezo machache baadhi ya sababu kila panapokuwa haja.

Tunaanza na sababu 3:

Rais Kikwete amekuwa mstari wa mbele wa kutaka kuwepo utawala wa sheria. Utawala wa sheria ndiyo msigi mkuu wa utawala wa kidemokrasia, Tanzania ni nchi mojawapo miongoni mwa nchi changa kuwa na asasi zenye mamlaka zinazofanya kazi kwa uhuru kamili.

Hivi sasa ni wazi kwamba nchini Tanzania hakuna mtu anayekuwa juu ya sheria; awe ni raia wa kawaida, kiongozi mkuu serikalini au watendaji wakuu waandamizi. Matukio ya kutaka sheria ichukue mkondo, yako wazi na sasa tunaweza kusema sheria inatawala na watu wanaongoza. Tanzania haitumii utawala kwa sheria.

Rais Kikwete anajali mgawanyo wa madaraka kati ya mihimili mikuu mitatu

Sasa hivi mgawanyo wa madaraka kati ya utawala wa dola, mabaraza ya utungaji sheria na Mahakama uko wazi. Kila mhimili una eneo lake na mipaka yake utawala wa dola unafanya kazi ya utendaji katika mfumo wa dola. Utumishi wa umma, majeshi ya ulinzi na usalama na srikali za mitaa zote ni asasi za mamlaka. Uhuru wa Mahakama ni jambo lisilo la kubishaniwa. Tangu miaka ya 1960 bunge la Tanzania limekuwa linajaribu kuwa muhimili usiothibitiwa. Sasa hivi hilo limewezekana kutokana na Rais Kikwete kujali na kutaka kila mhimili uwe huru kufanya mambo yake na yote kwa maslahi ya taifa.

Rais Kikwete anajali na kutambua ulazima wa utawala bora kwa maendeleo ya taifa Utawala bora ni dhana mpya ambayo imebuniwa katika jitihada za dola kukabiliana na hali mpya inayotokana na matakwa mapya kadri mazingira ndani na nje ya jamii yanavyokuwa na matatizo mengi ya kijamii na kiuchumi. Utawala bora una maana ya ushirikishwaji wa wadau na dola kuwa chombo cha kuelekeza matumizi ya raslimali. Na hivyo utawala (bora) ni pamoja na njia zilizo bora za kudhibiti na kuratibu shughuli zinazolenga kuwapa watu uhuru zaidi na uwezo wa kuthibiti mazingira.

Rais Kikwete anathamini mashauriano kati ya wadau juu ya utungaji sera Rais Kikwete anajali usawa wa kijinsia.

Ametunza lengo la kuendeleza sera za kuvutia wawekezaji

Amekubali ushauri wa kufanya mabadiliko katika sera na sheria za madini (kuleta ulinganifu)

Ni kiongozi anayekubali ushauri katika miswada ya serikali inayopelekwa bungeni

Ni kiongozi mwenye kuwa na ubunifu katika utungaji sera za maendeleo mfano mzuri ukiwa ni sera ya Kilimo Kwanza.

Source: TAIFA Tanzania , Desemba 18, 2009
( Mambo yamepamba moto. Nyingine hii nimeinasa kutoka mtandao wa kwanzajamii.com)

Kwenye redhighlights hilo ni swala la kwanza la kutilia maanani.
Secondly,hata kama wadau wengi wanasema JK hafai second term,bado nakubaliana na Mrema kwamba kusema "Hajafanya kitu" ni uonevu,uonevu ambao umetokana na kile wengi wetu wanachokiita "udhaifu" ambao inawezekana udhaifi hu umetokana na jitihada zake za kufanikisha utawala bora ambapo jitihada hizo zinaweza zikawa zimetafsiriwa vibaya....Pengine alitakiwa awe mbabe maana wabongo ndivyo walivyozoea,ukicheka nao wanakuona we ****.
 
tuambieni wote ujinga wenu enyi vibudu mnaotafuta madaraka kwa nguvu.
 
wote mmenena enyi waungwana ila mie nauliza jambo moja tu naomba mnijibu kama kikwete wako wanaomuona hafai kumalizia ngwe yake ya mwisho ya miaka 5 je nani mnaona atatufaa kutuongoza ktk miaka m5 ijayo,naomba mnipe mwangaza ndugu zangu je nani afaa ili tujiandae kumchagua,nijuzeni waungwanaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa.
 
Kwenye redhighlights hilo ni swala la kwanza la kutilia maanani.
Secondly,hata kama wadau wengi wanasema JK hafai second term,bado nakubaliana na Mrema kwamba kusema "Hajafanya kitu" ni uonevu,uonevu ambao umetokana na kile wengi wetu wanachokiita "udhaifu" ambao inawezekana udhaifi hu umetokana na jitihada zake za kufanikisha utawala bora ambapo jitihada hizo zinaweza zikawa zimetafsiriwa vibaya....Pengine alitakiwa awe mbabe maana wabongo ndivyo walivyozoea,ukicheka nao wanakuona we ****.

Wananchi wanataka tangible things/services na wala hawahitaji siasa. Mkapa kweli alikuwa mwizi na muuzaji wa raslimali za nchi kwa wageni na yeye kujiuzia mgodi. Kikwete tangu ameingia ni migogoro tu hakuna lolote alilolisimamia na likaonekana. mfano:

  1. TRL ni uozo na hapo kashindwa, kwa nini asiige Hugo Chaves
  2. TICTS ni uozo kwa nini asi wafurushe wale wahuni pale akina karamai?
  3. Richmond/Dowans ni uozo
  4. Loliondo amewauzia waarabu na hakuna tamko lolote mpaka waarabu wanakuwa na mawasiliano yao ndani ya nchi yetu, sijui hata JWTZ kama wanajua kazi za vizuri.
  5. mauaji ya Mbagala, kwa nini asimfukuze waziri wa ulinzi??
  6. Mauaji ya albino, masha anafanya nini pal wizara ya mambo ya ndani??
Kuna mambo mengi ambayo kikwete kama raisi ameonyesha kushindwa. Halafu kama ni muungwana kwa nini asitangaze kwamba hata gombea ili amuandae mtu mwingine naye ajaribu?? make hii nchi ni ya kujaribia kuongoza/kutawala.
 
wote mmenena enyi waungwana ila mie nauliza jambo moja tu naomba mnijibu kama kikwete wako wanaomuona hafai kumalizia ngwe yake ya mwisho ya miaka 5 je nani mnaona atatufaa kutuongoza ktk miaka m5 ijayo,naomba mnipe mwangaza ndugu zangu je nani afaa ili tujiandae kumchagua,nijuzeni waungwanaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa.

Dr. John Pombe Magufuli anafaa sana hili taifa kwa sasa.
 
Kama kuna mtu aliewahi fanya dhambi ya kuwadharau hawa jamaa (mafisadi and the like) na kufikiri kwamba hawana uwezo mkubwa, ni mimi. At first nilifikiri Watanzania wangewashtukia mapema na kung'amua pumba zao. Sikujua kuwa wana uwezo wa kuweka pumba zao hadharani kwa mtindo walio uweka. Kuna mtu aliwahi sema humu bodini kwamba hawa jamaa ni wale wale tu, hakuna cha nani wala nani. Nami nakubaliana nae asilimia zote.

Mjengwa, duh!!! At least you should have a choice...

Kwa wana JF ... "kwa nini kumlaumu dobi kwa uachafu wa kaniki? ... ni rangi yak ile..."
 
Wana CCM milioni 4 (kasoro Nungayembe wa kisiasa) na wapiga kura kwa mamilioni, wanatambua uongozi wa Rais Jakaya Kikwete. Hao waliopiga kura katika Uchaguzi Mkuu 2005, pamoja na wapiga kura wapya tuna hakika, hawajaona au hawategemei kuona mbadala kwa nafasi ambayo Kikwete anayoishikilia. Kwa nini tunaona hivyo?

Mimi naweza kusema nilifuata mkombo kumpa kura yangu 2005. Akili yangu hainitumi kurudia kosa hilo tena. Hivyo, katika hao milioni 4, mimi simo. Nitaangalia mgombea mwingine mwenye nafuu, nitampa kura yangu. By the way, we are all Tanzanians. It doesn't matter where the better candidate comes from.

Hali iliyopo kwa watu wanaofanya shughuli zao za kuzalisha mali na katika kujenga taifa inaridhisha tofauti na ramli za kutabiri mwisho wa dunia ya Tanzania yenye amani zinazopigwa na baadhi ya vyombo vya habari.
Sijui hali gani inayoridhisha katika ongezeko la masikini nchini. Sijui ni hali gani inayozungumziwa wakati mfumo wa bei unapaa kila kukicha. Sijui mwandishi anasema nini. Naomba msaada. Tanzania haina mwisho. Kama kuna ramli kama hiyo, mimi siiungi mkono. Ila mwisho au mwanzo wa Tanzania hauna uhusiano na JK kuchaguliwa au kutochaguliwa tena 2010.
Kuna kundi dogo la watu ambao wana nongwa ya kuukosa Urais 2005 na wengine ambao hawana uwezo wa kuchambua matukio, michakato na mienendo ya kisiasa na kijamii wanaendeshwa na kuamini katika hisia zao, ambazo zinawatuma kuandika vitu vya kubuni na alnacha.
Sioni uhusiano wa waliokosa urais 2005 na kinachosemwa na wananchi kwa wingi wao kuhusu udhaifu wa serikali yao. Waliokosa, wameshakosa. Hata wakifanyaje hawawezi kuwa wameupata urais 2005. Kauli hizi za waliokosa na waliopata ni dhaifu sana, na zina lengo hafifu la kukwepa hoja. Watu wanalalamika jinsi mafisadi wanavyofaidi matunda ya Taifa kinyume na taratibu na kuachiwa huru. Watu wanasema jinsi serikali isiyo na sababu ya kushindwa kutekeleza mambo yake inavyoendelea kushindwa kutekeleza hata yale madogo yanayotekelezeka kwa urahisi. Watu wanavilio visivyosikilizwa na viongozi wao.
Walipofanikiwa kumg'oa Edward Lowassa hawakuridhika. Wamekuwa wakijidanganya kwamba wanaweza kutimiza ndoto yao ya kumng'oa na Kikwete na kuzika kizazi hicho cha uongozi. Katika Gazeti la Mwanahalisi, toleo Na. 167 Jumatano Desemba 16-22, 2009 makala ya M.M. Mwanakijiji (sababu 51 za kumkwamisha Kikwete) mwandishi anaonyesha alivyokosa cha kuandika, akalazimisha hoja na sababu kwa nini Rais Kikwete asigombee nafasi ya Urais mwaka 2010.
Nani aliemng'oa Edward Lowassa? EL aliamua mwenyewe kwa busara zake kuachia mamlaka ya uongozi wa juu wa nchi. Kuna haja ya kuendelea kukumbusha yaliyopelekea kujiuzuru?

Kikwete anayo haki ya kugombea kama mwananchi mwingine yeyote aliekidhi mahitaji ya Katiba kwa nafasi hiyo. Ni uhuru wetu kumchagua au lah.
Kwanza kabisa hakuna mwanachama ndani ya CCM anayeweza kutaka kugombea na akawa tishio kwa Rais Kikwete. Kikwete alishapitia tanuru la moto mwaka 1995 na 2005.
Hii ni kauli ya kisiasa zaidi ya ukweli.
Hakuna watu wenye nguvu na uwezo wa kila hali ambao wanaweza kujitokeza sasa kuliko wale ambao aliishashindana nao huko nyuma. Majina ya akina John Samwel Malecela, Frederick Sumaye, Profesa Mark Mwandosya, Cleopa Msuya, Benjamen Mkapa, Jaji mstaafu Mark Bomani, Salim Ahmed Salim na mengineyo ni majina makubwa. Alishindana nao na akawashinda.
Nadhani mwandishi anakusudia kutukana wazee wa Taifa bila sababu. Hata hivyo, ni lini JK alimshinda Mkapa katika uchaguzi wowote? Kauli nyingine ya kisiasa yenye nia ya kuchafua zaidi hata kidogo kilichopo.
Kikwete kugombea Urais siyo kwa maslahi ya wapambe, kuna mambo makubwa zaidi ya wapambe ambayo yanamfanya mtu agombee nafasi kuu ya Urais. Tamaa ya mtu katika nafsi yake kutaka kugombea uongozi ni kwamba ana uwezo fulani na anataka atekeleze mambo fulani nje ya nafsi yake. Wako watu wengi katika uwanja wa siasa ambao hawafikii hatua hiyo.
Kama sio kwa maslahi ya wapambe ni kwa maslahi ya nani? Maana hakuna maslahi kwa mwingine yeyote zaidi ya wale wanaoendelea kuvuna kidogo kilichopo (wapambe).
Kuwepo kwa wengi wasiofikia hatua ya kuwa na tamaa ya kutekeleza mambo fulani nje ya nafsi yake ni tusi kwa wananchi wa Taifa hili. Maana ya kawaida ya sentensi hii ni kuwa, hakuna mtu mwenye walau ndoto ya kuweza kuinua hali ya maisha ya watanzania na kuleta maisha bora zaidi kwa watu wa nchi hii. Kama nimeielewa vizuri, kauli hii inamaanisha kuwa hakuna mTanzania mwenye uwezo wa kuongoza Taifa endapo JK atamaliza kipindi chake, au atakaposhindwa uchaguzi wa Rais. Kauli hii siikubali kabisa.

Na kwa tusi hili, namwambia mwandishi "MWENYEWE".

Ukweli wa mambo ni kwamba tangu achukue madaraka 2005, mambo mengi yamekuwa yanafanyika hapa nchini. Miradi imekuwa inatekelezwa na serikali watu katika sekta binafsi, mashirika makubwa ya kimataifa na mashirika ya kidini. Kusema kwamba wanaotaka Kikwete agombee ni wale ambao wanakariri kikasuku msemo wa "kuendeleza umoja, utulivu, amani na mshikamano" wa nchi yetu, ni fikra za mtu ambaye akili yake imedumaa na kukwama kutokana na kutotaka kujifunza mabadiliko yanavyotokea katika mazingira na nani analeta mabadiliko hayo.
Ningefaidika zaidi na mifano ya miradi hiyo, kwa maana kama ipo, ni michache sana ukilinganisha na kasi tulioitegemea kwa nchi tulivu.
 
Wananchi wanataka tangible things/services na wala hawahitaji siasa. Mkapa kweli alikuwa mwizi na muuzaji wa raslimali za nchi kwa wageni na yeye kujiuzia mgodi. Kikwete tangu ameingia ni migogoro tu hakuna lolote alilolisimamia na likaonekana. mfano:

  1. TRL ni uozo na hapo kashindwa, kwa nini asiige Hugo Chaves
  2. TICTS ni uozo kwa nini asi wafurushe wale wahuni pale akina karamai?
  3. Richmond/Dowans ni uozo
  4. Loliondo amewauzia waarabu na hakuna tamko lolote mpaka waarabu wanakuwa na mawasiliano yao ndani ya nchi yetu, sijui hata JWTZ kama wanajua kazi za vizuri.
  5. mauaji ya Mbagala, kwa nini asimfukuze waziri wa ulinzi??
  6. Mauaji ya albino, masha anafanya nini pal wizara ya mambo ya ndani??
Kuna mambo mengi ambayo kikwete kama raisi ameonyesha kushindwa. Halafu kama ni muungwana kwa nini asitangaze kwamba hata gombea ili amuandae mtu mwingine naye ajaribu?? make hii nchi ni ya kujaribia kuongoza/kutawala.

Magezi,hayo unayosema ni kweli,ila uozo huo ulikuwepo hata kabla hajaingia madarakani,shida kubwa tuliyokuwa nayo na ambayo ndiyo imetu cost ni mikakati mbinu ya kutupitisha wakati wa transformation period kwenda kwenye ubepari,Mkapa alitumia dola na kila aina ya other means kuhakikisha maamuzi hayo ya kibepari wakati wa transformation,mengi yake yakiwa hayana manufaa kwa wananchi yalipitishwa na kusimamiwa,yani hata wizi na ujambazi wa wazi wazi wa rasilimali za Taifa unalindwa kibabe,hiyo ikiwa ni mojawapo ya characteristics za kibepari....Ceratinly JK licha ya kuonekana kuufuata mfumo huo wa kibepari bado haonekani kuchukua the same measurements.

Nina imani tuna Ombwe la kiuongozi kwasababu hata viongozi wetu in reality hawajui in what direction is our country going or needs to go,hakuna vision wala mission ya kutuguide towards any kind of a vision....Na ndio maana unasema kuwa bado tuna migogoro,inawezekana JK hakuchagua njia nzuri ya ku correct yale ya Mkapa,na matokeo yake ndiyo hayo ya kuonekana mdhaifu.

Taifa letu bado ni "changa" sana tu,na kwahivyo ni lazima tujadili accordingly.Ni juzi tu tumepata uhuru,na baada ya uhuru,viongozi wetu waliwafanya wananchi waamini kuwa sasa everything is ok,kumbe kazi ngumu ya kujitegemea ndio kwanza imeanza,maana chini ya system ya kikoloni,utaratibu wa kuwategemea waliujenga wao,na wakahakikisha kuwa utaratibu huo unakuwepo na kulindwa kwa kila hali kwa manufaa yao.

Bado hatujajinasua kutoka kwenye makucha hayo,ni issue ambayo inahitaji watu wakae chini na kutafakari kuwa where are we as a nation,and where we're going etc.

Mkapa yeye kazi yake ilikuwa ni ku uenforce ubepari na madhambi yake yote,hicho ndicho alichotaka kufanya,kuwafurahisha kina Mr Smith na makuburu wengineo in leu of wananchi and our National interests....Kwasababu madicteta wengi wanajuwa kupona kwao ni kumtumikia kaburu kwani ndiyo anayewalinda...JK ameurithi mfumo huo,tatizo ni kwamba consequences za mfumo huo uliokuwa ukisimamiwa na Mkapa tayari zilikuwa zimewafikia wananchi na maisha kwa upande wao yakazidi kuwa magumu na ndio maana JK akaja na kuwadanganya kwamba sasa maisha ya kila mmoja wao yatakuwa bora tofauti na mfumo unaopelekea wachache tu ndio wawe na maisha bora,na baadae kwa mshangao wa wengi wa wananchi ni kwamba wale waliouziwa rasilimali zetu kwa bei chee ndiyo wenye kuusifu uchumi wetu pamoja na wale wachache waliofaidika wakisapoti kuwa eti Mkapa aliuinua uchumi,what a pathetic statement...Kutokana na uchanga wa Taifa letu,hakuna uwezekano wa kiongozi yeyote yule ambaye tumeshawahi kuwa naye wa kutufanya tuwe all the way developed at this time,no matter how right they could have been,viongozi wetu walijaribu,na bado wanajaribu ale ambayo hayawezekani kwa wakati huu,ni kama tuko kwenye shimo,na hakuna uwezekano wa kuondolewa moja kwa moja kutoka kwenye shimo na kiongozi yeyote yule,kila kiongozi atakayekuja anachotakiwa kufanya ni kujenga mazingira mazuri kwa kiongozi anayefuatia kuendeleza pale alipofikia yule aliyopita,na hilo linawezekana pale tu Taifa litakapokuwa na dira na mwelekeo,mwalimu alikuwa navyo,akikiri vimeshindikana,since then hatujatafakari kwamba ni what direction we should now take....Ni lazima tuwe na mkakati utakaotuletea mfumo mpya na hivyo si vyema kumuonea JK kwamba hajafanya lolote chini ya mfumo huu wa kipuuzi.

JK hawezi kufanya lolote la msingi kama mfumo mzima usipobadilishwa,na kama Taifa tusimamishe upuuzi wote halafu tuone where we should be going. ..Kwasababu hatuwezi kuwa on the wrong track to begin with halafu tutegemee hiyo wrong track itatufikisha kwema(at the right place),its wrong before we even depend on it.
 
Tanzania is no longer an ideological society it is a realistic society! hiyo data ya jk kushinda kishindo was it real au ni ya wizi kutokana na pesa za EPA? If that it is tru kwa utendaji wake can you please mention hata barabara moja yenye km 10 ambayo imejengwa kwa kiwango cha lami ambayo haikuwepo kwenye mpango kazi katika utawala uliopita/

ninyi vibaraka wa Makamba na Rostam, acheni uongo, semeni kweli!!!!!!

Mkuu mimi naamini kuwa JK alishinda kihalali kabisa mwaka 2005. Ila alishinda kwa matarajio mapya na yaliyopuuzwa kabisa na utawala wake. Watu walitegemea kuwa, kwakuwa alikuwa kiongozi wa juu katika serikali mbili zilizopita, kwakuwa alikuwa anachanganyika na watu na kuongea nao kwa uwazi, kwakuwa alikuwa mwenye nguvu na akili timamu na kwa kuwa alikuwa na ahiba, basi angeweza kuwa Rais bora sana kwa nchi yetu. Leo ndio tunajiuliza kama alistahili imani yote hiyo.
 
wote mmenena enyi waungwana ila mie nauliza jambo moja tu naomba mnijibu kama kikwete wako wanaomuona hafai kumalizia ngwe yake ya mwisho ya miaka 5 je nani mnaona atatufaa kutuongoza ktk miaka m5 ijayo,naomba mnipe mwangaza ndugu zangu je nani afaa ili tujiandae kumchagua,nijuzeni waungwanaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa.
Daktari Slaa
 
Mkuu mimi naamini kuwa JK alishinda kihalali kabisa mwaka 2005. Ila alishinda kwa matarajio mapya na yaliyopuuzwa kabisa na utawala wake. Watu walitegemea kuwa, kwakuwa alikuwa kiongozi wa juu katika serikali mbili zilizopita, kwakuwa alikuwa anachanganyika na watu na kuongea nao kwa uwazi, kwakuwa alikuwa mwenye nguvu na akili timamu na kwa kuwa alikuwa na ahiba, basi angeweza kuwa Rais bora sana kwa nchi yetu. Leo ndio tunajiuliza kama alistahili imani yote hiyo.

Mkuu Recta;Imani haitasaidia chochote chini ya mfumo huu wa sasa,ni politics tu,i can bet my five cents kuwa chini ya mfumo huu huu,hata aje malaika na tuwe na imani ya kuiong'oa milima bado we'll be in a wrong truck,and thats where we should start at.
Chukulia mfano wa vibaka,kila siku tunasikia wanchomwa moto,lakini je hayo yamepunguza ukibaka?Jibu ni no kwasababu justice system pamoja na dola vimeoza,na hapo tayari inapelekea kutokujali from both wananchi pamoja na vibaka hao.Hatuwezi kuweka imani kwa mkuu wa polisi kama system bado ni ile ile corrupt....It goes all the way up.
 
TUNAMJIBU M.M. MWANAKIJIJI:


Kuna hoja imejibu hoja hapa jamani? Unless kama ni hoja Mpya za Kumtetea Rais

Nilitegemea ningeona mwandishi ameainisha kila hoja ya Mwanakijiji na kuijibu moja moja na siyo tu kutoa majibu ya Jumla
 
wote mmenena enyi waungwana ila mie nauliza jambo moja tu naomba mnijibu kama kikwete wako wanaomuona hafai kumalizia ngwe yake ya mwisho ya miaka 5 je nani mnaona atatufaa kutuongoza ktk miaka m5 ijayo,naomba mnipe mwangaza ndugu zangu je nani afaa ili tujiandae kumchagua,nijuzeni waungwanaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa.

Mkuu, pamoja na hamu kubwa ya kumjua mtu anaeweza au anaekusudia na kufaa kuwa Rais baada ya uchaguzi mkuu ujao. Sidhani kama ni sahihi kutaja mtu kwa jina kuwa ndie anaefaa. Hii ni kwakuwa, inahitaji nia thabiti, kujitokeza na kuchambuliwa kuonekana kuwa unafaa kuwa kiongozi wa juu wa Taifa hili. Itakuwa ni uonevu na uchonganishi kumtaja mtu asie na nia wala sababu ya kugombea kuwa ndie anaefaa. Ukweli ni kuwa wapo wengi sana wanaoweza kufanya mambo mazuri na makubwa katika uongozi wa nchi yetu. Ila wasipojitokeza, uwezo wao hautakuwa na maana yoyote.

Jambo la maana kufanya ni kusubiri, kushawishi wanaoweza kugombea na kuwa viongozi wazuri wajitokeze na kuchambuliwa uwezo wao, halafu wananchi waamue. Ila hakuna anaetakiwa kufundishwa kuwa aliepo madarakani hakidhi haja.
 
Moja ya dawa muhimu ni kubadilisha katiba ili kipindi cha Urais kiwe kimoja tu kuanzia mwaka ujao, 2010. Mbunge jasiri akiamua anaweza kupeleka hoja binafsi bungeni ili zoezi lianze mapema na kwa kasi inayostahili. Hatuhitaji Rais kuwa madarakani kwa vipindi viwili. Kimoja kinatosha sana mtu kufanya yale aliyoyapanga na serikali yake kwa ajili ya nchi yetu. Namini uzoefu tunao wa kutosha katika hili.
 
Back
Top Bottom