Taifa Tanzania lapinga sababu 51 za Kikwete kutogombea 2010!

Taifa Tanzania lapinga sababu 51 za Kikwete kutogombea 2010!

- Only ukinigusa kwenye masilahi ya taifa!

Respect!

FMEs!


halafu nilitaka kukuuliza..
hili la salim a salim kuwa vice president ndo limekufa
now sasa anahusishwa na kina butiku?
wewe unasikia nini huko ndani?
 
Nafikiri kampeni maalumu imeshaanza kulazimisha mafanikio ya JK. Leo kulikuwa na kipindi maalumu kwenye ITV mahsusi kuimba mafanikio ya JK. Lakini kama mafanikio yapo si uache wananchi wayaone, kwa nini uyapigie upatu kiasi hicho?!
 
halafu nilitaka kukuuliza..
hili la salim a salim kuwa vice president ndo limekufa
now sasa anahusishwa na kina butiku?
wewe unasikia nini huko ndani?

- Dataz huko ndani ni kwamba bado wanajaribu kumpa Urais wa Zanzibar!, Wanaamini kwamba itakuwa ndio dawa ya Pemba na CCM, hasa Muungano!

Respect.


FMEs!
 
Nafikiri kampeni maalumu imeshaanza kulazimisha mafanikio ya JK. Leo kulikuwa na kipindi maalumu kwenye ITV mahsusi kuimba mafanikio ya JK. Lakini kama mafanikio yapo si uache wananchi wayaone, kwa nini uyapigie upatu kiasi hicho?!

Kwa nini anyamaze kama anaona ana mafanikio? Hiyo ndio siasa bana...la sivyo kusingekuwa na haja ya kampeni
 
Lenin aliwaita watu wa design hii (mwandishi wa article) 'Useful Idiot'.
 
Nafikiri kampeni maalumu imeshaanza kulazimisha mafanikio ya JK. Leo kulikuwa na kipindi maalumu kwenye ITV mahsusi kuimba mafanikio ya JK. Lakini kama mafanikio yapo si uache wananchi wayaone, kwa nini uyapigie upatu kiasi hicho?!

- Tatizo ni pale wanaposhindwa kujibu hoja bila personal attacks, hapa sio siri kwamba wamekunwa na hoja 51 za Mwanakijiji, mpaka wamekuja mbio kujibu lakini bado wanadai zimetolewa na mtu asiyekwua na uwezo mkubwa wa kuchambua siasa katika jamii, lakini amekuja kujibu anyways!

- Kule kongamano la Mwalimu Foundation, kiongozi wao akadai wana chuki na wivu tena wa binafsi kwa sababu walikosa urais, wakati wote tunajua kuwa Butiku na Quaresi hawajhawahi kugombea urais, licha ya Mwanakijiji, baba wa kujengea hoja Sitta hayupo tena Mtandao, si unaona wanavyopwaya!

- Sasa wataenda kwa Ruhinda tena na Kisumo! Bwa! ha! ha! yamewafika shingoni!

Respect.


FMEs!
 
Nafikiri kampeni maalumu imeshaanza kulazimisha mafanikio ya JK. Leo kulikuwa na kipindi maalumu kwenye ITV mahsusi kuimba mafanikio ya JK. Lakini kama mafanikio yapo si uache wananchi wayaone, kwa nini uyapigie upatu kiasi hicho?!
Alafu huyu mwalimu mwenzio Prof Mushi alianza na hoja nzuri sana kwa kusema anashangaa wapi tumekosea? maana anasema Tanzania mpaka tunapata uhuru miaka 40 iliyopita tulikuwa sawa na nchi kama Korea kimaendeleo lakini leo wala hata hatuwafuati nyuma bali tuko maili maelfu toka walipo.
Ajabu nimeona hakuendeleza hoja hiyo badala yake akaanza naye kumtetea Kikwete kwamba kazi ya urais ni ngumu.
Shit! hivi kama kazi ya urais ni ngumu nani alimwambia agombee na kutupatia ahadi za uongo?
Sikuona ajabu yule mama Shelukindo kumtetea kikwete maana alikuwa pia mwana mtandao. Wala sikuona shaka Sendeka kutetea maslahi ya chama chake.
Katika yote waliyozungumza hakuna hata mmoja aliyetoa point nzuri ya kutuonyesha tutavuka vipi mbali na kushambulia watu wanaomlalamikia Kikwete kwa kutochukua maamuzi mazito.
Chua naye leo kwa hali isiyokuwa ya kawaida hakuweka nafasi ya wasikilizaji kuporomosha maswali badala yake katuwekea one sided mahojiano. Sijui naye sasa amenyweshwa ya kijani? Mungu wangu tusaidie Tanzania. Ondoa hii takataka yote!
 
Wadau, mchomeko wa mada nyingine kwenye Taifa Tanzania inayohitaji kujadiliwa.

TUNAMJIBU M.M. MWANAKIJIJI:

Sababu 102 kwa nini Jakaya Kikwete agombee 2010 na aendelee kuongoza

MWANDISHI WETU


Wana CCM milioni 4 (kasoro Nungayembe wa kisiasa) na wapiga kura kwa mamilioni, wanatambua uongozi wa Rais Jakaya Kikwete. Hao waliopiga kura katika Uchaguzi Mkuu 2005, pamoja na wapiga kura wapya tuna hakika, hawajaona au hawategemei kuona mbadala kwa nafasi ambayo Kikwete anayoishikilia. Kwa nini tunaona hivyo?

Hali iliyopo kwa watu wanaofanya shughuli zao za kuzalisha mali na katika kujenga taifa inaridhisha tofauti na ramli za kutabiri mwisho wa dunia ya Tanzania yenye amani zinazopigwa na baadhi ya vyombo vya habari.

Kuna kundi dogo la watu ambao wana nongwa ya kuukosa Urais 2005 na wengine ambao hawana uwezo wa kuchambua matukio, michakato na mienendo ya kisiasa na kijamii wanaendeshwa na kuamini katika hisia zao, ambazo zinawatuma kuandika vitu vya kubuni na alnacha.

Walipofanikiwa kumg’oa Edward Lowassa hawakuridhika. Wamekuwa wakijidanganya kwamba wanaweza kutimiza ndoto yao ya kumng’oa na Kikwete na kuzika kizazi hicho cha uongozi. Katika Gazeti la Mwanahalisi, toleo Na. 167 Jumatano Desemba 16-22, 2009 makala ya M.M. Mwanakijiji (sababu 51 za kumkwamisha Kikwete) mwandishi anaonyesha alivyokosa cha kuandika, akalazimisha hoja na sababu kwa nini Rais Kikwete asigombee nafasi ya Urais mwaka 2010.

Kwanza kabisa hakuna mwanachama ndani ya CCM anayeweza kutaka kugombea na akawa tishio kwa Rais Kikwete. Kikwete alishapitia tanuru la moto mwaka 1995 na 2005.

Hakuna watu wenye nguvu na uwezo wa kila hali ambao wanaweza kujitokeza sasa kuliko wale ambao aliishashindana nao huko nyuma. Majina ya akina John Samwel Malecela, Frederick Sumaye, Profesa Mark Mwandosya, Cleopa Msuya, Benjamen Mkapa, Jaji mstaafu Mark Bomani, Salim Ahmed Salim na mengineyo ni majina makubwa. Alishindana nao na akawashinda.

Kikwete kugombea Urais siyo kwa maslahi ya wapambe, kuna mambo makubwa zaidi ya wapambe ambayo yanamfanya mtu agombee nafasi kuu ya Urais. Tamaa ya mtu katika nafsi yake kutaka kugombea uongozi ni kwamba ana uwezo fulani na anataka atekeleze mambo fulani nje ya nafsi yake. Wako watu wengi katika uwanja wa siasa ambao hawafikii hatua hiyo.

Ukweli wa mambo ni kwamba tangu achukue madaraka 2005, mambo mengi yamekuwa yanafanyika hapa nchini. Miradi imekuwa inatekelezwa na serikali watu katika sekta binafsi, mashirika makubwa ya kimataifa na mashirika ya kidini. Kusema kwamba wanaotaka Kikwete agombee ni wale ambao wanakariri kikasuku msemo wa “kuendeleza umoja, utulivu, amani na mshikamano” wa nchi yetu, ni fikra za mtu ambaye akili yake imedumaa na kukwama kutokana na kutotaka kujifunza mabadiliko yanavyotokea katika mazingira na nani analeta mabadiliko hayo.

Kwa upande mwingine dhana ya utulivu wa kisiasa (political stability) imepitwa na wakati. Wanataaluma na watunga sera, sasa hivi wanazungumzia utulivu utokanao na mkusanyiko wa sababu mbalimbali za maendeleo katika sekta za uchumi na ustawi wa jamii (structural stability). Kwamba watu hawali maneno matupu na nadharia za siasa.

Utulivu kimfumo una nafasi kubwa kutokana na sekta mbalimbali kutegemeana ili kuleta maendeleo yenye ulinganifu, hivyo ni wazi kwamba sera zote zinazotungwa na miradi inayotekelezwa inakuwa imepangwa kimtambuka kiasi kwamba yanayotokea sekta moja yanaathiri maendeleo yatakavyokuwa katika sekta nyingine.

Kwa namna moja au nyingine watanzania walio wengi katika sekta mbalimbali wanaguswa na kufikiwa na miradi ya maendeleo ya kubadilisha maisha yao . Yawezekana kwamba kasi ya maendeleo inazidiana. Lakini kwa namna moja au nyingine kuna mabadiliko ya msingi kule wanapoishi watu.

Watu wasioelewa hali inavyobadilika wanakuwa wa kwanza kupiga mayowe jinsi serikali ilivyoshindwa kuwaletea watu maendeleo, bila kutambua ukweli wa mambo kwamba watu wenyewe ndiyo watajiletea maendeleo na kazi hiyo ndiyo wameshaianza. Kwa waandishi wapiga ramli, kwa sababu wanataka kuonyesha msimamo wao wa “kupinga kila kisemwacho au kufanywa na hasimu wao”, wanakuwa na watu wao ambao wanawaumba na kuwatengenezea mazingira.

Wanapoanzia siyo kuonyesha uwezo wa kiongozi wao wa kufikirika bali ni kubuni na kuzua mambo, na kujaribu kugeuza mkondo wa maji utoke ziwani na kupanda mlima. Kwa hili la Kikwete kugombea 2010 tunasema binadamu ana uwezo mkubwa, lakini hawezi kuzuia jua kuchwa!

Katika jamii inayokua kwa misingi ya kidemokrasi wapiga kura na raia kwa ujumla wana nafasi yao katika mchakato wa siasa, uchumi na maendeleo ya jamii. Nchi inaweza ikawa katika matatizo makubwa ya kiuchumi lakini hakuna matukio ya uvunjivu wa sheria wa makusudi kutoka kwa watu wengi. Tanzania ilipitia vipindi vigumu ambapo uchumi wa nchi ulikuwa mbaya. Hakuna fujo zilizotokea ambao zilitishia usalama wa watu na mali zao.
Kuna sababu 102 ambazo tunaona kwa nini Rais Kikwete agombee Urais 2010. Tutazitolea maelezo machache baadhi ya sababu kila panapokuwa haja.

Tunaanza na sababu 3:

Rais Kikwete amekuwa mstari wa mbele wa kutaka kuwepo utawala wa sheria. Utawala wa sheria ndiyo msigi mkuu wa utawala wa kidemokrasia, Tanzania ni nchi mojawapo miongoni mwa nchi changa kuwa na asasi zenye mamlaka zinazofanya kazi kwa uhuru kamili.

Hivi sasa ni wazi kwamba nchini Tanzania hakuna mtu anayekuwa juu ya sheria; awe ni raia wa kawaida, kiongozi mkuu serikalini au watendaji wakuu waandamizi. Matukio ya kutaka sheria ichukue mkondo, yako wazi na sasa tunaweza kusema sheria inatawala na watu wanaongoza. Tanzania haitumii utawala kwa sheria.

Rais Kikwete anajali mgawanyo wa madaraka kati ya mihimili mikuu mitatu

Sasa hivi mgawanyo wa madaraka kati ya utawala wa dola, mabaraza ya utungaji sheria na Mahakama uko wazi. Kila mhimili una eneo lake na mipaka yake utawala wa dola unafanya kazi ya utendaji katika mfumo wa dola. Utumishi wa umma, majeshi ya ulinzi na usalama na srikali za mitaa zote ni asasi za mamlaka. Uhuru wa Mahakama ni jambo lisilo la kubishaniwa. Tangu miaka ya 1960 bunge la Tanzania limekuwa linajaribu kuwa muhimili usiothibitiwa. Sasa hivi hilo limewezekana kutokana na Rais Kikwete kujali na kutaka kila mhimili uwe huru kufanya mambo yake na yote kwa maslahi ya taifa.

Rais Kikwete anajali na kutambua ulazima wa utawala bora kwa maendeleo ya taifa Utawala bora ni dhana mpya ambayo imebuniwa katika jitihada za dola kukabiliana na hali mpya inayotokana na matakwa mapya kadri mazingira ndani na nje ya jamii yanavyokuwa na matatizo mengi ya kijamii na kiuchumi. Utawala bora una maana ya ushirikishwaji wa wadau na dola kuwa chombo cha kuelekeza matumizi ya raslimali. Na hivyo utawala (bora) ni pamoja na njia zilizo bora za kudhibiti na kuratibu shughuli zinazolenga kuwapa watu uhuru zaidi na uwezo wa kuthibiti mazingira.

Rais Kikwete anathamini mashauriano kati ya wadau juu ya utungaji sera Rais Kikwete anajali usawa wa kijinsia.

Ametunza lengo la kuendeleza sera za kuvutia wawekezaji

Amekubali ushauri wa kufanya mabadiliko katika sera na sheria za madini (kuleta ulinganifu)

Ni kiongozi anayekubali ushauri katika miswada ya serikali inayopelekwa bungeni

Ni kiongozi mwenye kuwa na ubunifu katika utungaji sera za maendeleo mfano mzuri ukiwa ni sera ya Kilimo Kwanza.

Source: TAIFA Tanzania , Desemba 18, 2009
( Mambo yamepamba moto. Nyingine hii nimeinasa kutoka mtandao wa kwanzajamii.com)
Na kwa kujua kuwa ni pumba alizoandika na ili asichekwe kaamua kutoandika jina lake.
MMkjj huwa anaweka id yake pale na wao waweke basi.
 
Nafikiri kampeni maalumu imeshaanza kulazimisha mafanikio ya JK. Leo kulikuwa na kipindi maalumu kwenye ITV mahsusi kuimba mafanikio ya JK. Lakini kama mafanikio yapo si uache wananchi wayaone, kwa nini uyapigie upatu kiasi hicho?!

Mwalimu, hapa umeteleza,

Serikali iliyoko madarakani ina haki ya kusema yale iliyotekeleza, na wapinzani wana haki kusema yale ambayo hayakutekelezwa. Then Mwananchi ataamua mwenyewe nani mkweli.


Ati serikali isiambiwe wananchi wake imefanya jambo mahali ... aliyeko Mbeya ajue ya Bukoba bila kuhabarishwa ni upotoshaji wa habari mkubwa sana.
 
Unaposema tangu 2005 Kikwete alipoingia madarakani mambo mengi yamefanyika na miradi mingi imetekelezeka bila kuwa more specific ni kujidanganya. Mwanakijiji katika makala yake alieleza very specifically mambo ambayo Kikwete has been a let down mfano, serikali yake kushindwa kutekeleza mapendekezo ya bunge, kutoshughulikia ipasavyo watuhumiwa wa EPA, KAGODA etc. Nilidhani angekuwa more specific ili tuweze kujua mazuri ya Kikwete, he has not done so...!!!for reasons only known to himself...
 
CCM watampendekeza kuwa mgombea wao, then our duty ni kuwaelimisha wananchi umuhimu wa kutomchagua kwa kuweka scientific reasons zenye data badala ya vague statement wanazosema wao, kuna statistics nyingi za kuonyesha kuwa kikwete hatufai, lakini wao watakuja na vague statements na kibaya zaidi kwenye nafasi mbaya zaidi kwani wao wanamiliki vyombo vyahabari.

Pamoja na hayo tunatakiwa kuweka masirahi ya Taifa mbele hasa sisi tunaojadili hapa, mtu unaona kabisa hapa Rais amekosea lakini unamchagua kwa kuwa ww unatekeleza ibara ya 15 ya katiba ya CCM, that is not fair kwa Taifa lako, wazazi wako na ndugu zako wanaoitaji maendeleo ya nchi kuliko ww unayeangalia maendeleo ya mfuko wako

Wana JF charity begins at home, wanachama wa CCM hapa ndio mnatakiwa kuwa wa kwanza kuadvocaye changes kwenye chama chetu kitukufu kwa kuwaadabisha viongozi wetu ambao hawawezi kutekeleza majukumu yao, tuseme ukweli na kuwambia kuwa hawawezi kuwajibika na ikinidi tuwawajibishe kwa njia sahii

Kwenye mambo ya biashara kuna kitu kinaitwa cannibalization, kama huwezi kuwa creative enough na kutumia opportunities zinazojitokeza kwenye environment, then competitor watakucanibalize, then tunachokiiona hapa cha vyama vya upinzani kuja na ufisadi wa CCM kila siku ni kwa sababu CCM imeshindwa kusoma harama za nyakati na inakumbana na environmental punishment

Siku zote jipu linaanza kama kipele, haiwezekani jipu likaanza na ukubwa wake, CCM then jipu limeanza kama mnasubiri liive mjue rangi ya usaa subirini kama mnatafuta njia sahihi ya kuakikisha jipu haliendelei, Kikwete may not be the right person to drive you out of problems
 
kuna msemo mmoja niliupata kwenye filamu fulani usemao...its not about who does what,what matters is how well one does the job..so kwenye swala la JK kupewa nafasi ya kugombea uraisi tena mm binafsi naunga mkono kupinga mana ameonyesha efficiency ni dhahifu,mm sina shida nani apewe ila how well can that person do the job,ahata kama mtampa nchi mwanakijiji well and good muimu ni output
 
Hata zije sababu 10001 za kumsapoti.
Je macho hayaoni ukweli??
 
Sijaona hiyo article ya Mwanakijiji kwa hivo nitaongea kutokana na kilicholetwa katika hii reply.

Kikwete mwenyewe amesema kwamba 70% ya Watanzania ni bendera kufuata upepo, huyu ndiye rais anayeshabikiwa?

Labda amesema kweli, maana wangekuwa si bendera kufuata upepo wasingemchagua yeye.Hapa kuna hao bendera kufuata upepo na wale wanaolinda/ kutafuta maslahi binafsi kwa kujikomba kwa wakubwa, style iliyowatoa kina Kikwete na Makamba.

Mwandishi anamsifia Kikwete kwamba amepitia tanuru la moto kwa kushindanishwa na magwiji kama vile Tanzania tuna system ya meritocracy na Kikwete kashinda on the merit (merit gani?).Tunajua Tanzania uongozi wa juu haufuati meritocracy, bali kuna Machiavellianism tupu na Kikwete was simply the best courtesant at stabbing his opposition in the back with a dagger and better at obtaining illegal funding.

Ndiyo maana nikasema rais ajaye atakuwa mbaya kuliko Kikwete kwa sababu system yetu haijakaa kum reward mtu mwenye uwezo na track record (meritocracy) ila the best deceiver kama Kikwete.
Hakika uko sahihi kabisa! Tunahitaji mfumo huo unaotoa mwianya ya watu wenye uweza halisia kupewa nafasi za kugombea hadi hatua ya mwisho kabia. Huko CCM kuna vitu ambavyo hufanyika katika uteuzi wa mgombea Urais hakika haviwatendei haki wananchi, maana vyovyote vile mtu akijitokeza kugombea lakini anasifa zinazofaa kabisa kwa mjibu ya uzoefu wake wa utendaji kwa kufuata taratibu, sheria na uwezo binafsi hao hutupiwa vilago kwa kuambiwa ondoa jina lako! Tunakumbuka kwa mfano Mzee Malecela alivyofanyiwa kwa mara kadhaa na huo ni mfano mmoja tu!

Hivyo binafsi nakupongeza kwa uchambuzi wako huo mfupi juu ya kuelezea majibu ya hawa jamaa tusiowafahamu. Kwanza ni wababaishaji tu fulani hawa. Thread ya M. M. Mwkjj iltolewa siyo siku nyingi zilizopita na kwa maana hiyo, leo isingewezekana watu milioni 4 kuwa walishayafanyia kazi mapendezezo yaliyotolewa kwenye kipindi kifupi kama hiki na kuweza kutoa majibu yao. Huyu ni mtu mmoja tu amekaa ama na mwenzake wakaandika kwa kusema watanzania milioni 4.

Tuache ubabaishaji katika masuala ya msingi, masuala yanayotujengea uwezo kama jamii, halafu mtu fulani anaingiza hoja yake ya uongo na kusema ni ya watu milioni 4. Namshauri ajitambulishe kama mtu na siyo kuja kwa mgongo wa kundi. Hata hivyo bado hoja zake ni dhaifu. Maana CCM haijawahi kuwa na tanuru lolote linalopia viongozi wa dhati kama siyo ushabiki tu.
 
Back
Top Bottom