Taja aina ya muziki usioupenda

Taja aina ya muziki usioupenda

tpaul

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2008
Posts
24,225
Reaction score
22,632
Naingia kwenye mada moja kwa moja bila kuwachosha. Kwa mujibu wa nguli wa muziki wa dansi nchini, marehemu Remy Ongalla, muziki ni burudani, furaha, huzuni, nk. Hapa anamaanisha kuwa muziki ni kila kitu.

Hakuna binadamu aliyekamilika asiyependa kusikiliza au kucheza muziki. Pamoja upenzi wa muziki, kila mtu ana aina fulani ya muziki asioupenda hata kidogo.

Binafsi siupendi katu muziki wa bongofleva kwa sababu mbalimbali. Kwanza muziku huu hauna maadili yoyote bali umejaa matusi na ushabiki wa mambo ya ovyo kama vile ngono, bangi, uhalifu, uvunjivu wa amani na kila aina ya ghasia.

Pili, muziki huu hauna mpangilio mzuri wa mahadhi (melody) ukiachilia mbali jinsi waimbaji wake wanavyoimba kwa kubana pua na kuhemea juu juu.

Tatu, muziku huu unatukuza ngono 100%. Nyimbo za bongofleva zinazohamasisha uzalendo, uwajibikaji, maendeleo na utu hazizidi 10 tangu muziki huu ulipoasisiwa hapa nchini zaidi ya miongo miwlili iliyopita.

Wakati nikuwa safarini kwenye basi ya abiria huwa napata taabu na aibu kubwa sana, hasa ninapokuwa nasafiri na watoto wangu au watu wa heshima. Unakuta safari nzima tangu Dar hadi Karagwe zinapigwa vudeo za bongofleva zenye maudhui ya matusi tupu huku mabinti wakiwa uchi wakishikwashikwa makalio na wavulana.

Pia wakati fulani nikihitaji kusikiliza redio napata taabu sana pale ninapotafuta stesheni lakini najikuta stesheni zote zinapiga nyimbo za bongofleva. Inabidi tu nizime redio nisubiri DW na BBC watakapokuwa hewani nisikilize. Ni shida sana kwa kweli.

Aina nyingine ya muziku ambao hauiingii akilini mwangu ni muziki wa taarabu. Kama ilivyo kwa bongofleva, muziku huu umejaa vichambo, masengenyo, masuto na upumbavu mwingine kama huo.

Kusema kweli nikisikia wimbo wa bongofleva au taarabu unapigwa, nahisi kutapika. Yaani najisikia kichefuchefu kabisa kama mwanamke mwenye mimba changa.

Je, ni aina gani ya muziki ambao wewe hauupendi hata kidogo na ambao ukiusikia unapigwa unahisi umeguswa na kitu chenye ncha kali?
 
Naingia kwenye mada moja kwa moja bila kuwachosha. Kwa mujibu wa nguli wa muziki wa dansi nchini, marehemu Remy Ongalla, muziki ni burudani, furaha, huzuni, nk. Hapa anamaanisha kuwa muziki ni kila kitu.

Hakuna binadamu aliyekamilika asiyependa kusikiliza au kucheza muziki. Pamoja upenzi wa muziki, kila mtu ana aina fulani ya muziki asioupenda hata kidogo.

Binafsi siupendi katu muziki wa bongofleva kwa sababu mbalimbali. Kwanza muziku huu hauna maadili yoyote bali umejaa matusi na ushabiki wa mambo ya ovyo kama vile ngono, bangi, uhalifu, uvunjivu wa amani na kila aina ya ghasia.

Pili, muziki huu hauna mpangilio mzuri wa mahadhi (melody) ukiachilia mbali jinsi waimbaji wake wanavyoimba kwa kubana pua na kuhemea juu juu.

Tatu, muziku huu unatukuza ngono 100%. Nyimbo za bongofleva zinazohamasisha uzalendo, uwajibikaji, maendeleo na utu hazizidi 10 tangu muziki huu ulipoasisiwa hapa nchini zaidi ya miongo miwlili iliyopita.

Wakati nikuwa safarini kwenye basi ya abiria huwa napata taabu na aibu kubwa sana, hasa ninapokuwa nasafiri na watoto wangu au watu wa heshima. Unakuta safari nzima tangu Dar hadi Karagwe zinapigwa vudeo za bongofleva zenye maudhui ya matusi tupu huku mabinti wakiwa uchi wakishikwashikwa makalio na wavulana.

Pia wakati fulani nikihitaji kusikiliza redio napata taabu sana pale ninapotafuta stesheni lakini najikuta stesheni zote zinapiga nyimbo za bongofleva. Inabidi tu nizime redio nisubiri DW na BBC watakapokuwa hewani nisikilize. Ni shida sana kwa kweli.

Aina nyingine ya muziku ambao hauiingii akilini mwangu ni muziki wa taarabu. Kama ilivyo kwa bongofleva, muziku huu umejaa vichambo, masengenyo, masuto na upumbavu mwingine kama huo.

Kusema kweli nikisikia wimbo wa bongofleva au taarabu unapigwa, nahisi kutapika. Yaani najisikia kichefuchefu kabisa kama mwanamke mwenye mimba changa.

Je, ni aina gani ya muziki ambao wewe hauupendi hata kidogo na ambao ukiisikia unapigwa unahisi umeguswa na kitu chenye ncha kali?
hakuna muziki usiopendwa na mtu yoyote yule na ukiona mtu hapendi muziki fulani jua ana shida kichwani mwake
 
Binafsi siupendi katu muziki wa bongofleva kwa sababu mbalimbali. Kwanza muziku huu hauna maadili yoyote bali umejaa matusi na ushabiki wa mambo ya ovyo kama vile ngono, bangi, uhalifu, uvunjivu wa amani na kila aina ya ghasia.
Uko sahihi kabisa.
 
Mama yangu kasema atasafiri na wanamuziki. wewe kaa pembeni
Mama kusafiri na wasanii kuna uhusiano gani ma mtu kutopenda muziki wa aina fulani mkuu?
 
Mimi napenda muziki wa aina yoyote, inategemea tu hiyo nyimbo imeimbwaje.

Sichukii muziki kwa sababu ni wa aina fulani, nitauchukua kama sijakipenda kinachoimbwa ndani yake au mahadhi yake.

Ahsanteni
 
Electro na Metal mpaka huwa najiuliza ujinga gani huu. Alafu unakuta wenyewe wakiwa high wanazungusha vichwa kama vichaa na yale makele.
Hahaha! Hata mm sipendi kabisa muziki wenye zogo aisee. Lakini utamkuta mtu mzima kabisa anasikiliza/,kucheza muziki wa bongofleva hadi unamshangaa. Watu tunatofautiana sana.😳😳🤯
 
sipendi:
1. amapiano
2. singeli
3. bongo fleva ya kisasa

napenda:
1. bongo fleva ya zamani (kushuka 2010)
2. traditional taarab(culture)
Unadhani ni nini kilichoharibu muziki wa bongoflrva wa kisasa mkuu?
 
Mimi napenda muziki wa aina yoyote, inategemea tu hiyo nyimbo imeimbwaje.

Sichukii muziki kwa sababu ni wa aina fulani, nitauchukua kama sijakipenda kinachoimbwa ndani yake au mahadhi yake.

Ahsanteni
Je, muziki wa bongofleva unauelewa mkuu?
 
Amapiano, Trap, Bongo fleva za Kishogashoga mfano kina Zuchu, kusah, jaymelody, lavalava na wengine wa uimbaji wa aina hiyo.
 
Amapiano,, wee unakuta mtu mzima unarembua macho ndo nini sasa..
Hahaha! Amapiano ni muziki wa aina gani mkuu? Unaweza kuweka mfano tuusikie? Inaonekana watu wengi hawapendi aina hii ya muziki.
 
Back
Top Bottom