Taja madeni yako: Je, unadaiwa kiasi/ kitu gani?

Zero IQ

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2016
Posts
13,959
Reaction score
24,935
Wanasema kwamba hata uwe tajiri vipi huwezi kukosa deni. Lazima kutakuwa na mtu, kampuni/ benki inayokudai.

Wengine wanafika mbali zaidi na kusema kama mtu unaogopa kukopa na kudaiwa, basi huwezi kuwa na mafanikio.

Je, wewe hapo kwa sasa unadaiwa nini? Kama ni pesa, ni kiasi gani?

Binafsi hapa nilipo nipo na madeni haya:

-Tala=45,000
-Tigo =36,000
-Airtel =37,000
-Branch=6,000
-Nadaiwa bili ya maji 9,200, hii leo nitailipa.
-Nadaiwa na jamaa 35,000.
-Nadaiwa hela ya posa milioni 1 na laki 3, kati ya milioni 1 na laki 5, nilitoa laki 2 tu.


Hayo ndiyo madeni yangu hayo ya juu ukitoa matatu ya mwisho, yameshakuwa sugu sasa.


Cc Zero iq
 
Voda Mpawa 125K yaani sina raha kila siku kupokea simu na sms za vitisho kutoka kwao najua nimepitiliza muda ila nitailipa.

Mpendwa mteja, MPAWA, Kila jambo lina mwisho. Mkopo tuliokupa sio kiwango cha mwisho, Ila marejesho yake tulikuekea mwisho wa kufanya. Umekaidi,Umedharau,Umepuuzia, Tafsiri yako kwetu ni mteja anaetaka kutapeli kampuni. Mwisho wa ubaya ni Aibu, HATUTAKI KUKUAIBISHA AU KUKUDHALILISHA KWA MKOPO MDOGO. Bonyeza *150*00#KULIPA LEO HII.
 
Tigo : 180,000
Airtel : 420,000

hawa eatel ntawalipa tu siku maana sina namna hela hata iingie bahati mbaya wanailamba,ila tigo sitegemei kwakweli maaana hata tigo pesa iwe na 500,000 hawakati wala kuigusa hela yako na wanakudai.

Eatel kuna siku ntafunga macho paaaaap "ila ndio wasubiri nijazwe upako"
 
Aiseeeeee
 
Umekaidi,umedharau,umepuuza.....duuh unaweza kuhamia mitandao mwingine kwao hasira
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…