Taja misemo ya wahenga isiyo na tija

Kila mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake...Mimi nakataa, atakula kwa huruma ya mchungaji...
 
Kisicho riziki,hakiliki.
Je wewe sio riziki au hauliki?
Ukisema wewe,sio riziki,mhhh,ni hatari!!!!kumbe mtoto sio riziki wewe!!!
Ukisema hauliki,maana wewe sio riziki(shoga).Ukisema unalika,hii nayo ni hatar!!!Unalika??
 
Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni.

Hivi mtu akinyongwa Akafa, hiyo haki yake ataipata kaburini?
Hiyo ni namna ya uandishi lakini ni HAKI YAKE MPENI MNYONGE,HALAFU MKITAKA MNYONGENI.

kama vile PUNDA AFE MZIGO UFIKE yaani MZIGO UFIKE HATA PUNDA AKIFA , YAANI ACHOKE ATAKAVYOCHOKA LAKINI AFE BAADA YA KUFIKISHA MZIGO
 
Hii kampeni dhidi ya wahenga,ni moja ya kampeni za ubaguzi wa kishenzi sana.Ni dalili ya ushenzi na kutokustaarabika.Ni kampeni dhidi ya watu wanaoonekana kuwa na mapungufu aidha kutokana na ufukara,kukosa elimu,na ajali za kibiolojia.
Wanaoendesha kampeni hii,wengi ni vijana wadogo na ambao pia,wanawaona wazee wasiowapendeza machoni pao kama wahenga,na hapa wahenga ikitumika kama neno la dhalili,dharau na masimango!Wanafanikiwa kuchekesha watu,lakini,hii ni dalili tosha ya kuonesha bara hili lilistahili kutawaliwa hadi Yesu atakaporudi.Zamani nilisikia kuwa mwafrika huko ulaya aliwekwa kwenye zoo!Niliwashangaa sana wazungu lakini leo,naiona zoo imehamia mtandaoni.Vijana wengi wangefurahi kuona watu walioharibika sura,maumbile na hata akili zao,kuwekwa kwenye zoo,ili waweze kuwafaidi na kuchekeshana.Ninahofu na kiwango cha ustaatabu huu.Kama nimewagusa,poleni maana hii haiwezi kupita bila kukemewa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mteja anayekimbizwa na askari kilema

great thinker
 
kuchapiwa siri ya ndani

huyu mhenga namtaguta hadi leo

Do Something 2day That Your Future Will Thank You 4
 
Tuorodheshe misemo ambayo haina tija kwa jamii ya sasa.
Samahanini wahenga;Mi naanza
Wa juu mngoje chini.
Nguo ya kuazima haisitiri mat*k*
Polepole ndo mwendo
Mtegemea vya ndugu hufa maskini
Kikulacho ki nguoni mwako

Mimi nadhani wewe ndio hauna tija, mbona misemo yote hapo ina maana hebu jaribu kunyumbulisha akili.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…