Taja namba yako halafu taja majina ya classmates wako Na namba Yao husika.

Maisha yangu yalikua Class Z.

Wakajichanganya kunipa ukiranja ndiyo nikawa sishindi darasani kwa kinga ya ukiranja.

Hilo neno 'Class Z' kwa aliyepita pale atajua ni shule gani.
 
Mimi nilikuwa mtu wa kisasi

Nikiibiwa peni ujue darasa zima watalizwa.
 
Mtoa mada mbona unatuchanganya, tuchague kutoka kwenye orodha ya mkono wako au ya picha?
 
Wakati niko shule ya msingi nilikuwa namba tano. Ila nilikuwa naiba vitabu tu, nothing else 😃😃😃😃
 
Kwel mimi simo

Wakujaradia

Unavaa ka kipande ka jinzo ndani kaliko shonewa ngozi ya mbuzi matakoni kila fimbo ikipita mwalimu akimaliza unampa pole ki moyoyo hatupo humu?

Mganga watimu ya shule je? anawekwa wapi?


Sisi wa kubana chooni hata kama tumewahi namba je hatumoo?

Wa kuangalizia a.k.a jicho la kinyonga tuko wapi?
 
Mkiweka namba 14 mniambie.
@LIKUD ni fundi; 1-13 ni attachment kisha mwendelezo akafanya kuandika. Kwaio kila kitu kipo sawa, japo kuleta logical sequence angeanza na attachment.

Yangu hapo naona ni HAKUNA JIBU
 
Sijajiona wengine tuliingia darasani kwaajili ya kuitwa jina tu na baada ya hapo tuliishiia mitaani au kwenye miembe na mapera.
 
Mhuni wa darasa ni namba ngapi ? Kuna walinu walinitabiria nitachomwa moto kabla ya kufika miaka 25, sasa hivi nawacheka hiiiiiiiiii🤣
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…