Utotoni kulikuwa na mambo mengi tuliyokuwa tunaambiwa na wakubwa wetu lakini baada ya kukua, ndio tukaja kugundua ilikuwa ni uongo!
Binafsi mimi nilikutana na haya;
1. Ukifukia soda ardhini ukiiacha wiki mbili itamea halafu inazaa utachuma, nililpofukia tu wakaichimba na kuinywa🤣🤣🤣daah walah..
2. Ngurumo wakati wa mvua ilikuwa ni mapipa yanapigwa mateke na mungu, mvua ni maji yaliyomwagika kutoka kwenye hayo mapipa[emoji23][emoji23]kwa kweli walitushinda...
3.Mwenzio akijamba usipotema mate utaota meno matakoni[emoji23][emoji23][emoji23][emoji38][emoji38]
4.Ukikalia mafiga unapata majipu kwenye makalio....
5.Ukilia usiku, sauti yako itachukuliwa na mashetani[emoji39][emoji23][emoji23]🤣
Hebu tiririkeni hapa uongo ambao ushaambiwa, tutoe stress kidogo....