TAKUKURU, Polisi waja na muarobaini wa rushwa za barabarani wakishirikiana na wadau

Vibao vya speed limit ya 50/km ndio chanzo kikuu cha hawa mabwana kudai virushwa vya kipumbavu.

Hivi vibao vimeshapitwa na wakati. Wangeweka hata most places speed limit iwe 80km/hr. Unakuta eneo lipo wazi barabara imenyooka ila speed limit ni 50. Na hawa ndio vinajibanza hayo maeneo kuvizia dereva atembee hata na 52km/hr wamtishie kumpiga fine au waombe kitu kidogo.

Kwahiyo TAKUKURU acheni unafiki, serikali ndio inawapa jeuri ya kuomba rushwa hawa jamaa na sio kwamba wao wenyewe ndio wanaamua.
 
LESIRIAMU,
Kiutumishi kina maadili ya utumishi TAKUKURU wakipitia huku watawabana wengi. Pili kuna ngazi za mishahara za watumishi zimenainishwa kwenye circular. Ajabu utakuta Mtumishi wa Umma anashindana na mfanyabiashara.

Gari kubwa injini Ina 4200cc.3500cc 2400cc hawana hofu tinted ya kutosha. Nyumba kubwa fensi hatari unajiuliza maadili yako wapi na unajiuliza huyu mtumishi ana biashara gani kwenye ofisi za umma.

Suala la rushwa mmomonyoko wa maadili Na Ni kukosa uzalendo na kazi yako. Turudishe maadili tuanze sasa na ofisi ya maadili na utumishi wapo kwanini hawakushirikishwa?
 
Huku horohoro kwetu...yaaani mpakani kenya-tanzania wasomali ndio illegal transit route wanakimbilia south africa, sasa traffic akichungulia akiwaona hao jamaa Basi wote mnaomba passport, sasa hao jamaa hawana...

Basi traffic na konda wanaenda nyuma ya Basi wakirudi kazi imeisha safari inaendelea.....

Kwa rushwa hii tumekuwa njia ya kupitisha haramu na la Shabaab pia.
 
Tuchekelee tu ila wakianza kusimamia sheria ya kulipa kiwango chote 30,000 naomba tuchekelee pia maana we una makosa zaidi ya moja unatozwa kisela buku 5 unasepa.

ANYWAY HII NCHI KWA SASA NI KUUMIZANA MPAKA TUTIE ADABU.
 
Punguza trafiki barabarani ndio suluhisho kamili, tuache utani jamani.
 
Jamani, msipingane na mkuu wa kaya aliyesema tuwape za kung'arishia viatu.
 
Hongereni kwa kukaa kikao hicho na mkalipana na posho kuzungumzia zimwi ambalo hamuwezi kuliua nchi hii. Suala la rushwa Polisi ni kama KPI (key perfomance indicator) kwao, imefika hatua polisi wao kwa wao wanashindana kupaua msauzi, wanashindana kununua magari na kugawana magari na pikipiki zilizo kaa muda mref kituoni baada ya kukamatwa, wamachomoa vipuri kwny magari hayo na vipuri hivyo. Imefika hatua katika nchi hii ni bora ukutane na jambazi mwenye silaha ukimpa hela na simu anakuachia huru, ila ukikutana na polisi watakuchukua hela zote na watakubambika kesi na kesi yoyote hata ya mauaji. Imefika hatua sasa polisi wanapasiana taarifa za wahalifu ili kila polisi aende akachukue hela kwa muhalifu wanamgeuza shamba la bibi maisha yake yote,(ukiwa na duka la vipodozi utalea polisi wote wa eneo ulipo mpaka mkuu wao). Imefika hatua mwananchi akiingia kituo cha polisi anaweza ugua ugonjwa wa moyo kwani atakayo kutana nayo mule ataambiwa ameua. Imefika hatua ukikutwa na simu ya mtu unabambikiwa na kesi ya mauwaji. Gereza zimejaa mahabusu na wafungwa walio onewa kisa hawakutoa rushwa, ama hawana connection na watu wakubwa . Katika nchi hii Polisi wa kawaida tu Koplo au Inspekta anaweza kuwa na kipato cha juu kuliko afisa mwandamizi wa kada nyingine serikalini. Polisi akila rushwa hata TAKUKURU hawahangaiki nae hii nchi inasikitisha sana nadhani kuna siri kubwa serikali inayo juu ya watu hawa.
 
Roving Journalist,
Kwa matrafki barabarani serikali iweke faini 10,000 badala ya 30,000 kwa kosa.Mtu akikamatwa na kosa iwe ni rahisi kulipa elfu kumi serikalini na akapewa na risiti yake. Hii elfu 30 ndo mzizi wa tatizo inafanya polisi kujiona miungu watu na wanakubambika makosa watakavyo wao na ukweli ni kwamba elfu 30 ni kubwa na inakaribisha mazungumzo ya rushwa na serikali kupoteza mapato yake kwa hawa wapuuzi.
 
Maisha ya Polisi wala rushwa yatakuwa magumu sana

Binafsi siamini hivyo. Hivi kuna polisi asiyekula rushwa? Polisi usalama barabarani mbona wanachukua rushwa hadharani? panda daladala ndipo utaona wengi wa trafiki wana magari binafsi ambayo yamepatikana kwa fedha za rushwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…