DOKEZO TAKUKURU, TAMISEMI mje Karagwe - Kagera, Walimu Wakuu na Maafisa Elimu (Karagwe) wanaumiza wanaopewa tenda

DOKEZO TAKUKURU, TAMISEMI mje Karagwe - Kagera, Walimu Wakuu na Maafisa Elimu (Karagwe) wanaumiza wanaopewa tenda

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Hapa Halmashauri ya Wilaya Karagwe, Mkoa wa Kagera kuna changamoto kubwa ya kukosekana kwa uadilifu na uwajibikaji unaofanywa hasa na Walimu Wakuu wa Shule pamoja na Ma-Afisa Elimu katika ngazi ya Shule za Msingi.

Inapotokea kuna tenda Mkandarasi anapata inayohusu Shule fulani, ili uweze kupata tenda hiyo unatakiwa ukubali ufanye kazi kisha kabla ya kupata malipo yako, wewe Mkandarasi uwape Walimu Wakuu na Afisa Elimu ‘kitu flani’ ili malipo yako yaweze kupitishwa.

Wakandarasi wanapokamilisha mradi au unapokuwa katika hatua fulani nzuri ukihitaji malipo, yanatakiwa yapite katika ngazi Tatu ikiwemo kwa Afisa Elimu na Mwalimu Mkuu.

Licha ya kuwa tenda kwa sasa zinatangazwa na Shule moja kwa moja na wale Wakandarasi wanazungumza na Walimu Wakuu lakini ukihitaji malipo wanakwambia “Afisa Elimu amekataa kusaini kwa kuwa hakuna fungu lake.”

Wale Wakandarasi wakienda kwa Afisa Elimu anawaambia “Mimi sijawapa tenda, nendeni kwa Walimu mliozungumza nao.”

Mkurudi kwa Mwalimu Mkuu anawaambia ukweli na kuwaonesha nyaraka kuwa mzigo haujasainiwa kwa kuwa Afisa Elimu bado “hajafurahi”.

Wakandarasi wakisema walipwe kisha watoe ‘kifuta jasho’ jamaa wanagoma kabisa, mara kadhaa wameamua kutoa mifukoni mwao ili kuona kama hilo litafanyika, wakishafanya hivyo tu malipo yanafanyika fasta.

Unakuta tenda zenyewqe sio za hela kubwa lakini hapohapo unatakiwa kugawana nao kitu ambacho kinawaumiza Wakandarasi.

Kwa umoja wetu tumeona sehemu sahihi ya kufikisha ujumbe wetu Serikalini hasa kwa TAKUKURU, Wizara ya Elimu, TAMISEMI pamoja na kwa Rais Samia Suluhu ni kupitia hapa Jamii Forums ili hatua zichukuliwe kwa kuwa wanaoumizwa na hali huyo ni wengi.

Kwa ufupi Watumishi wa Serikali hao wajuu wanatuumiza sana sisi Wakandarasi wadogo, na ukigoma kutoa ushirikiano kwanza kama unadai haupati hela zako na kama umeshalipwa ukaonekana unachonga haupati dili tena.

Risiti za malipo yote tunazo, tunasubiri TAKUKURU waoneshe ushirikiano tutawapa, pia kuna muda wanataka wapewe kifuta jacho mkononi tumewapiga picha pia, zote tuko tayari kuziwasilisha kwa Mamlaka wakizihitaji.
 
Daaah kila mtu anapiga dili hii tabia wameiga kutoa kwa wakubwa zao
Ten percent
Ngoja tulambe asali kwanza
Kula kwa urefu wa kamba yako,tusiingiliane
 
Wazabuni kama Nyie huwa hata hauhitaji kumuomba posho ww nenda nae jino kwa jino mbona hela atatoa mwenyewe.
Apo mwalimu kataka laki tu kelele nyingiii.
 
kuna mzabuni alikuwa ivo ivo alivofika level la Lenta akaambiwa leta tofali,nondo,cube za zege tukapime maabara kilichomkuta atasimuliza vizazi.
 
Hao takukuru unataka waje washughulikie rushwa ndiyo Wala rushwa zaidi.ukiwaita wafanye uchunguzi watakuomba wanaita ya maji na chai ili wachunguze haraka
 
Ukienda kumuona Daktari Hospital lazima uwe na pesa,

Ukienda kuomba Tenda kwa Mwalimu Mkuu lazima uwe na pesa,
Kila Mmoja atakula anakopeleka mboga😂

Ila Watanzania tubadilike.
Rushwa ni adui wa haki.

Nakupa pole sana.

Ila Wasi wasi wangu Mimi mnyororo uloutaja usishangae hao unaowataka waje kumbe na wenyewe kwenye mgao huo wamo😂😂

Labda watoke makao makuu ambao mgao haukuwafikia😀
 
Hapa Halmashauri ya Wilaya Karagwe, Mkoa wa Kagera kuna changamoto kubwa ya kukosekana kwa uadilifu na uwajibikaji unaofanywa hasa na Walimu Wakuu wa Shule pamoja na Ma-Afisa Elimu katika ngazi ya Shule za Msingi.

Inapotokea kuna tenda Mkandarasi anapata inayohusu Shule fulani, ili uweze kupata tenda hiyo unatakiwa ukubali ufanye kazi kisha kabla ya kupata malipo yako, wewe Mkandarasi uwape Walimu Wakuu na Afisa Elimu ‘kitu flani’ ili malipo yako yaweze kupitishwa.

Wakandarasi wanapokamilisha mradi au unapokuwa katika hatua fulani nzuri ukihitaji malipo, yanatakiwa yapite katika ngazi Tatu ikiwemo kwa Afisa Elimu na Mwalimu Mkuu.

Licha ya kuwa tenda kwa sasa zinatangazwa na Shule moja kwa moja na wale Wakandarasi wanazungumza na Walimu Wakuu lakini ukihitaji malipo wanakwambia “Afisa Elimu amekataa kusaini kwa kuwa hakuna fungu lake.”

Wale Wakandarasi wakienda kwa Afisa Elimu anawaambia “Mimi sijawapa tenda, nendeni kwa Walimu mliozungumza nao.”

Mkurudi kwa Mwalimu Mkuu anawaambia ukweli na kuwaonesha nyaraka kuwa mzigo haujasainiwa kwa kuwa Afisa Elimu bado “hajafurahi”.

Wakandarasi wakisema walipwe kisha watoe ‘kifuta jasho’ jamaa wanagoma kabisa, mara kadhaa wameamua kutoa mifukoni mwao ili kuona kama hilo litafanyika, wakishafanya hivyo tu malipo yanafanyika fasta.

Unakuta tenda zenyewqe sio za hela kubwa lakini hapohapo unatakiwa kugawana nao kitu ambacho kinawaumiza Wakandarasi.

Kwa umoja wetu tumeona sehemu sahihi ya kufikisha ujumbe wetu Serikalini hasa kwa TAKUKURU, Wizara ya Elimu, TAMISEMI pamoja na kwa Rais Samia Suluhu ni kupitia hapa Jamii Forums ili hatua zichukuliwe kwa kuwa wanaoumizwa na hali huyo ni wengi.

Kwa ufupi Watumishi wa Serikali hao wajuu wanatuumiza sana sisi Wakandarasi wadogo, na ukigoma kutoa ushirikiano kwanza kama unadai haupati hela zako na kama umeshalipwa ukaonekana unachonga haupati dili tena.

Risiti za malipo yote tunazo, tunasubiri TAKUKURU waoneshe ushirikiano tutawapa, pia kuna muda wanataka wapewe kifuta jacho mkononi tumewapiga picha pia, zote tuko tayari kuziwasilisha kwa Mamlaka wakizihitaji.
Ndivyo wahusika wote wa Tender za serikali wanavyofanya.


Kutokana na ukaguzi wa CAG hivi sàa ni ngmu muiba directly.

Kinachofanyika, yule anayelipwa ndio anatakiwa atoe kitu awape wahusika.

Haya ndio madili ya mainjinia wa Halmashauri.

Mfano:

Kwenye tenda bei ya ufundi ni milioni 20. Hao watu watakupanga mapema, ili wakupe hiyo kazi kwenye hiyo milioni 20 unawapa ngapi?

UKisema 2M na mkakubaliana, ukilipwa hiyo 20M yako ya ufundi, unatoa 2M yao unawapa. Hata CAG akague vipi, hawana hatia ya mahesabu kwasababu vitabu vinaonesha umelipwa wewe.
 
Back
Top Bottom