Takwimu zaonyesha Marekani ndio nchi inayoongoza kwa kuanzisha vita duniani

Takwimu zaonyesha Marekani ndio nchi inayoongoza kwa kuanzisha vita duniani

ldleo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
1,116
Reaction score
1,121
战争之国.jpg
Mwandishi huru wa habari za uchunguzi raia wa Marekani Benjamin Norton, hivi karibuni amenukuu nyaraka zilizotolewa na Bunge la Marekani akisema, kuanzia mwaka 1789 hadi mwaka 2022, Marekani imeanzisha vita 469 nje ya nchi.

Katika miaka 240 tangu kuasisiwa kwa taifa la Marekani, ni miaka 16 tu ambayo Marekani haikuwa katika vita. Baada ya kumalizika kwa Vita Baridi, Marekani ilitarajiwa kuacha kufanya vita nje ya nchi, lakini nchi hiyo ilianzisha vita mara kwa mara zaidi kuliko awali. Takwimu zinaonesha kuwa katika zaidi ya miaka 30 iliyopita tangu kumalizika kwa Vita Baridi, Marekani imeanzisha vita 251. Ripoti ya Norton pia imeeleza kuwa vita za Marekani zinalenga nchi mbalimbali duniani, haswa nchi za Latin-Amerika, na Afrika.

Marekani imedai mara kwa mara kuheshimu na kulinda “utaratibu wa kimataifa unaozingatia sheria”, lakini nyaraka hizo zimeonesha kikamilifu kuwa Marekani ni nchi inayopenda vita, na inafanya umwamba bila ya kujali utaratibu wa kimataifa. Marekani inapaswa kusahihisha makosa ya kuanzisha vita duniani, kuacha kuingilia kati mambo ya ndani ya nchi nyingine haswa kwa njia ya kijeshi, na kutoendelea kuwa mzushi mkuu wa vita duniani.
 
Nashangaa kuna watu sijui ni majitu hawajui historia ila wao ni ushabiki tu refer to Lumumba,gadaf nk
 
View attachment 2377431Mwandishi huru wa habari za uchunguzi raia wa Marekani Benjamin Norton, hivi karibuni amenukuu nyaraka zilizotolewa na Bunge la Marekani akisema, kuanzia mwaka 1789 hadi mwaka 2022, Marekani imeanzisha vita 469 nje ya nchi.

Katika miaka 240 tangu kuasisiwa kwa taifa la Marekani, ni miaka 16 tu ambayo Marekani haikuwa katika vita. Baada ya kumalizika kwa Vita Baridi, Marekani ilitarajiwa kuacha kufanya vita nje ya nchi, lakini nchi hiyo ilianzisha vita mara kwa mara zaidi kuliko awali. Takwimu zinaonesha kuwa katika zaidi ya miaka 30 iliyopita tangu kumalizika kwa Vita Baridi, Marekani imeanzisha vita 251. Ripoti ya Norton pia imeeleza kuwa vita za Marekani zinalenga nchi mbalimbali duniani, haswa nchi za Latin-Amerika, na Afrika.

Marekani imedai mara kwa mara kuheshimu na kulinda “utaratibu wa kimataifa unaozingatia sheria”, lakini nyaraka hizo zimeonesha kikamilifu kuwa Marekani ni nchi inayopenda vita, na inafanya umwamba bila ya kujali utaratibu wa kimataifa. Marekani inapaswa kusahihisha makosa ya kuanzisha vita duniani, kuacha kuingilia kati mambo ya ndani ya nchi nyingine haswa kwa njia ya kijeshi, na kutoendelea kuwa mzushi mkuu wa vita duniani.
Super power atakwepa vita yeye ndo aliwahi soko la ushawishi kwa nchi nying dunian kwa technologia, uchumi na kila kitu na nchi nying US ndo kimbilio lao., atakwepaje vita
 
Back
Top Bottom