Tamasha la Chris Brown Johannesburg: Tiketi zote zimeuzwa, zikiwa na bei kuanzia Tsh. 94,000 hadi 800,000

Tamasha la Chris Brown Johannesburg: Tiketi zote zimeuzwa, zikiwa na bei kuanzia Tsh. 94,000 hadi 800,000

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Tiketi za tamasha la Chris Brown ‘Breezy in South Africa’ katika Uwanja wa FNB, Johannesburg, zimeuzwa zote, huku tukio hilo kubwa likitarajiwa kufanyika tarehe 14 Desemba. Hili ni moja ya matukio yanayosubiriwa kwa hamu, ambapo mashabiki wamenunua tiketi kuanzia shilingi 94,000 hadi 800,000.
IMG_0031.jpeg

Tamasha linakuja wakati ambapo kuna maswali kuhusu maisha ya msanii huyu maarufu. Taarifa zinasema kuwa kutakuwa na documentary inayopangwa kuonyeshwa kwenye Investigation Discovery, ikiangazia matukio ya kikatili yanayohusishwa na Chris Brown.

Kwa muda mrefu, amekuwa kwenye kizungumkuti cha madai mbalimbali, baadhi amekiri na kuomba msamaha, huku mengine akiyakanusha bila ushahidi wa kutosha, lakini yote haya yameibua mijadala kuhusu tabia zake na maisha yake binafsi.

Kwa mashabiki wa Chris Brown nchini Afrika Kusini, tamasha hili linatoa fursa ya kipekee ya kumshuhudia staa huyu wa R&B akifanya onyesho live, licha ya changamoto za kisheria zinazomwandama.
 

Attachments

  • IMG_0031.jpeg
    IMG_0031.jpeg
    203.3 KB · Views: 6
Wajinga ndio waliwao

Mie siwezi kulipa hata buku kwenda kumuona huyo mnyanyasaji wa wanawake mpenda ugomvi na sie badala ya kwenda kupigana na kina p didy huko
 
Tiketi za tamasha la Chris Brown ‘Breezy in South Africa’ katika Uwanja wa FNB, Johannesburg, zimeuzwa zote, huku tukio hilo kubwa likitarajiwa kufanyika tarehe 14 Desemba. Hili ni moja ya matukio yanayosubiriwa kwa hamu, ambapo mashabiki wamenunua tiketi kuanzia shilingi 94,000 hadi 800,000.
View attachment 3114419
Tamasha linakuja wakati ambapo kuna maswali kuhusu maisha ya msanii huyu maarufu. Taarifa zinasema kuwa kutakuwa na documentary inayopangwa kuonyeshwa kwenye Investigation Discovery, ikiangazia matukio ya kikatili yanayohusishwa na Chris Brown.

Kwa muda mrefu, amekuwa kwenye kizungumkuti cha madai mbalimbali, baadhi amekiri na kuomba msamaha, huku mengine akiyakanusha bila ushahidi wa kutosha, lakini yote haya yameibua mijadala kuhusu tabia zake na maisha yake binafsi.

Kwa mashabiki wa Chris Brown nchini Afrika Kusini, tamasha hili linatoa fursa ya kipekee ya kumshuhudia staa huyu wa R&B akifanya onyesho live, licha ya changamoto za kisheria zinazomwandama.
Dunia watu wanapenda starehe na kushindwa kumtumikia alietuumba
 
Kweli kabisa,na mimi na my wife tunazo tiketi zetu tayari,tunasubiria show tu
 
Ktk sheria za kiislam unatakiwa upigwe mawe mpaka ufe ili usisambaze ukimwi. Lkn kwa sababu sheria za kiislam hazitumikii ndii maana ukimwi umeshika kasi
Weee,eti eeeh,mbona masheikh wengi ndio waathirika sasa,hawazitaki hzo bikra 72??
 
Weee,eti eeeh,mbona masheikh wengi ndio waathirika sasa,hawazitaki hzo bikra 72??
Wanaishi ktk jamii iliopotoka kama wewe. Sheria haingalii sheikh wala walii..mzimifu yoyote yule hata akiwa Imam mawe mpaka afe
 
Back
Top Bottom