Tamasha la Vuka na Chako la Mtume Mwamposa lamfukuzisha kazi kwa uzembe Meneja wa Uwanja wa Mkapa

Tamasha la Vuka na Chako la Mtume Mwamposa lamfukuzisha kazi kwa uzembe Meneja wa Uwanja wa Mkapa

Cognizant

JF-Expert Member
Joined
Aug 13, 2022
Posts
626
Reaction score
1,409
Salum mtumbuka,

Ametambulishwa rasmi kuwa Meneja mpya wa uwanja wa Benjamin Mkapa, Jijini Dar es Salaam akichukua nafasi ya Daniel Madenyeka ambaye alikuwa anakaimu nafasi hiyo.

Utambulisho huo umefanyika siku moja baada ya kutokea kwa tukio la kushindwa kuondolewa kwa jukwaa la injili kwenye mchezo wa ligi kuu na mrusha matangazo kulalamika kitendo kilichotafsiriwa kama uzembe kwa Meneja wa uwanja.

Habari: cloudstv

Ni matumaini yangu makubwa Cognizant (Alias) Adorable Angel mimi kuwa Mtume Mwamposa atamuajiri nyumbani au kanisani kwake au atamuombea arejeshwe hapo alipokuwa kwakuwa yeye ndiyo anajinasibu kuwa mwanadamu pekee mwenye nguvu ya upako na kiroho na aliyekaribu na Mwenyezi Mungu na mbali na Shetani.
 
Back
Top Bottom