Tambaza High school yashika nafasi ya 3 kutoka mwisho matokeo ya form six 2014

mtvbase

JF-Expert Member
Joined
May 22, 2014
Posts
1,243
Reaction score
561
Hii shule imeshakuwa kimeo kutoka kuwa shule bora kwa mkoa wa DSM hadi kuwa shule ya 3 kutoka mwisho
 
THE RISE AND FALL OF TAMBAZA
Sabab za kuanguka
1:headmaster mpya kuna baadh ya walim wanamwangusha kwa makusud kwakuwa ameingilia ugomv asiojua baina ya walim
2:kuna mwalim aitwae Mjuni huyu analudisha shule nyuma NB:huyu ndiye refa alopigwa ktk mechi ya yanga na azam
3:serikali imezisahau nsana shule kongwe
4:miundombinu ya ufundishaj hakuna
5:wanafunz nao social netwoks zimewahalib sn
6;
7:..........
 
Wote mnaosema social networks kwa hiyo hao walioongoza hawatumii??acheni sababu zisizo na mashiko.
 
Wakati nasoma A-Level Tambaza... ilikuwa ni balaha kwa watu kama mimi ambao tulitoka Private School ambako tulizoewa kupikiwa na kuwekewa mezani... hadi namaliza O-Level, sikuwa na sababu ya kwenda tution!

Nafika Tambaza, nakumbuka hadi tunamaliza Form V, tulikuwa na Mwalimu mmoja tu, wa Adv. Mathematics... hatukuwa na Mwalimu wa Physics wala Chemistry... mwaka mzima! Tunaingia Form VI, yule wa Mathematics akahama... tukapata wa Physics ambao alikuw ahodari wa kunong'ona na ubao... miezi kadhaa baadae, tukapata walimu wa field wa Chemistry!! Nakumbuka jinsi ambavyo walichanganyikiwa manake muda miezi ilikuwa imeshakatika lakini hatujasoma chochote... jamaa wakawa wanashindwa hata pa kuanzia!!!! Taabu ilikuwa zaidi kwetu ambao hatukuzoea mambo ya tuition coz' wenzetu kutoka shule kama Azania au Kibasila, walikuwa tayari wameshajipigilia minondo mara baada ya kupiga paper ya form IV.

Pamoja na yote hayo, watu tuliweza kupambana na kufaulu... thanks God, wakati ule hapakuwa na Facebook wala Twitter! Si hivyo tu, wala Ligi Kuu ya UK na Europe hatukuwa nazo! Sehemu pekee ya ku-socialize ni maskani!! Jambo pekee ambalo enzi zile lilikuwa likituweka macho ni mpambano wa Mike Tyson... ambao kwa mwaka mzima, ungekuta ni mpambano mmoja tu!!!!

Hapa nimeuliza kuhusu Mzizima Sec. School... jamaa walikuwa wabaya kufuru lakini na wenyewe siku hizi, balaha tupu!!! Na kule mitaani kwao kulivyojaa tablets, sipati picha!!
 
# 5 inachangia zaidi... mie nimesoma pale A-Level miaka ya 90's mwishoni... hayo mapungufu yalikuwapo tangu enzi hizo lakini kwa kuwa hatukuwa busy na dunia, watu tulifaulu!! Wakati tunasoma hata walimu wenyewe hatukuwafahamu kv kila mmoja ilikuwa na lwake... lakini watu tulifaulu! Hadi leo Second Mistress wetu namfahamu kwa jina la Bi. Mkora... simafahamu jina lake kv hakuwa na time na mimi na wala mimi sikuwa na time nae!!!!
 
Nmesoma tambaza 2007-2009 ila kimsingi pale hamna shule, walimu hawatosh na hao wachache wanaendekeza kazi za nje so mwanafunz hacpokua m2 wa kujtafutia mwenyew imekula kwake.
 
Hii ndio hali halisi ya shule nyingi za Serikali nchini. Serikali badala ya kuchukua hatua muafaka za kuboresha shule hizi inakaa kufanya usanii na kuwadanganya Watanzania kwa kushusha viwango vya ufaulu ili kuongeza idadi ya Wanafunzi waliofaulu. Shule nyingi za Serikali nchini ziko katika hali mbaya sana hatua madhubuti inabidi zichukuliwe haraka iwezekanavyo ili kurekebisha muelekeo unaotisha wa kuanguka kwa elimu nchini.

Nmesoma tambaza 2007-2009 ila kimsingi pale hamna shule, walimu hawatosh na hao wachache wanaendekeza kazi za nje so mwanafunz hacpokua m2 wa kujtafutia mwenyew imekula kwake.
 
wanafunzi wanachangia kuzishusha shule zao
 
dsm jiji la maraha. naona almost top ukitoa feza nyingine ni za vichochoroni.
 
mapigo ya moyo yanaenda mbio
region wise 27/27
nation wise 266/268
 
tatizo hao jamaa mchikichini inawaharibu,yani laiti kama mchikichini ingekua inafaulisha basi Azania na Tambaza zingekuwa kwenye kumi bora
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…