Tambaza vs Azania (that Infamous Battle)!

mchanga wa macho!....wee si ulisema umesoma shaban Robert?..how come tena ukasoma Tambaza?....juzi hapa kwenye matangazo uliandika unamtafuta shori mmoja ulisoma naye shaban robert ulikuwa unamtamani lakini unakufa kisabuni||
Na we binti Maringo ujifunze kumezea, huna dogo!!!!
 
Nipo hapa nimeboreka, najaribu ku-reminisce matukio mbalimbali ya maisha yangu. Wangapi hapa walishuhudia hii shughuli kwa namna moja ama nyingine? Unakumbuka nini kuhusu tukio hili?
Tulikuwa na mchizi mmoja kitaa, ni full bhange full vurugu!!! Tukienda disko la uswazi na isipopigwa "Jamaican in NewYork" ya .....(nishamsahau), jamaa lazima alete fujo na disco haliendelei hadi Jamaican in NewYork ipigwe!!! Uzuri ni kwamba kitaa kwenyewe kulikuwa na manunda kibao wa Tambaza ambao alijivuna wangemlinda!!!
 
Sidhani kama ni sahihi kusema azania walikuwa legelege, hawakuwa watu wa fujo lakini vurugu zilivyozidi walistep up, matukio aliyosema 'Waberoya' nayakumbuka, ilikuwa lazima mtembee kwa makundi, hasahasa mida ya kwenda nyumbani. Siku moja naelekea nyumbani mida ya mchana, nimeshaachana na washikaji niko mwenyewe, nikakutana na kundi la wanafunzi wa tambaza wakaanza kuniapproach, sikukimbia wala nini, nikasimama. Bahati wakaona wanajeshi (mnakumbuka kipindi kile wananunua chakula na vinywaji kwenye fence ya kambi pale upanga), wakageuza na kuondoka zao.

Kipindi hicho hicho migomo ya walimu ndiyo imepamba moto, kama sikosei. Companero nakumbuka kwa mbali Azajangwa, ilikuwa ni wanafunzi wa azania wanahook up na wanafunzi wa jangwani, right?

jmushi1, buza namkumbuka kwa mbali. azania walikuwa na jamaa mmoja hivi alikuwa anabeba chuma, amejaza hivi, baadaye alikuja kuwa bouncer casino ya pale newafrica hotel, sijui yupo wapi siku hizi, nadhani na yeye alikuwa anakaa sinza. Ila nakubali, tambaza walikuwa wababe. Hawakuwaga hata na timu ya kutisha ya mpira, labda basketball enzi za kina kelvin twissa, kiasi.
 
Nyie wote mlikuwa rough na wahuni katika enzi zile ni st.Joseph[Forodhani] pekee ndiyo ilikuwa shule ya wastaarabu. katika maisha yangu ya shule hiyo sikuwahi hata siku moja kuona mwanafunzi akivuta sigara lakini kwa azania na tambaza ilikuwa siyo ajabu. ninakumbuka hata wakati wa sherehe za kitaifa kule uwanja wataifa zikitolewa soda kwa kila shule lakini jamaa hawa walikuwa wanachukua hata za kwetu .
Ahsante sana kwa kukumbushia enzi zile
 

Nimecheza mpira sana hapo, uwanja ulikuwa una mashimo huo, na mipira ilikuwa inaenda barabarani sana tu. Mlivyomuua kondakta ndiyo ukawa mwisho wenu, Profesa Sarungi akaona basi. The fact kwamba mlihamishwa nyie na azania haikuguswa inaonyesha serikali walikuwa wanajua mgomvi ni nani.
 
Nasikia mnaa Hawanga kajifia zake, kweli?
haaaaaa, mkuu bruurei ulikua azaboy kumbe??
azaboys chama kubwa, huyu ticha alikua kimeo kwenye advanced maths,
alikua anatumia likitabu la SHAYO, duh ticha kimeo sana.
inawezekana amevuta, maana alikua anakula FEGI kama hana akili nzuri.
 

Utakuwa unamzungumzia Bazil. au ? Msela alishavuta, kuna thread humu JF niliiona.
 

Bwa ha ha..ndo utoto wa mjini huo.
 

Thanks for da image man!
It made me remember those crazy days.
 
Kipindi hicho kila denti anatamani Sekondari Tambaza..
Sijui ni zile mshikemshike au u-kichwa?
nai-admire kinoma ile shule (kabla ya kuvurugwa) todate..
Unajuaje labda wangetoka akina Eistein wakibongo
 
Nipo hapa nimeboreka, najaribu ku-reminisce matukio mbalimbali ya maisha yangu. Wangapi hapa walishuhudia hii shughuli kwa namna moja ama nyingine? Unakumbuka nini kuhusu tukio hili?
Nawakumbuka wavuta bangi wa shule hizi mbili...........
 
Sio wanafunzi wote wa Tambaza tulikuwa tunakula mmea, ila tulikuwa na solidarity ya ajabu!

Lakini huwezi kuzungumzia Tambaza, na mikwara ya wanafunzi hususan viwanjani, bila kuitaja Kinondoni Muslims. Wale Jamaa walikuwa wamepinda. Ilikuwa ni vita ya katika kipito Tambaza na Kin Muslims wakikutana!

Azania walikuwa ni shule na madaftari muda wote. Kama Seminari fulani hivi wakati ule.
 

That was great great time! mkiwa njiani, mnamwambia dereva vipi, tushuke hatuoni kama unaendesha gari! basi mlilopanda halitakiwi kupitwa!
 
Vurugu za Azania Vs Tambaza zilianza zamani sana. Tulikuwa na Mwalimu mmoja pale Azania aliitwa Mzee Meja na siku moja alitusimulia jinsi alivyokuwa refa kwenye mechi kati ya Tambaza na Azania na jinsi Tarzani Kesi (aliyekuwa Mchezaji wa Yanga baadaye) alivyokuwa mmoja wa watukutu wa Tambaza.

Hata hivyo enzi niliposoma mimi Azania Tambza hawakuwahi kutushinda kwenye Umiseta na hata ngumi, nakumbuka miaka ya mwanzo mwa 1990 au mwisho wa 1980s walikuja kucheza na Azania pale Aznaia tukawaunga na wakaanzisha vurugu, tuliwachapa sana na wakakimbia, walichofanya vijana wa Tambaza ni kutuvizia barabarani tukienda kupanda daladala huo ugomvi ulichukua muda kuja kuisha. Mwisho wa vurugu zilikuwa katikati ya miaka ya 1990s ambapo Aznaia waliwapiga sana Tambaza hadi kupelekea kufutwa kwa O'Level pale Tambaza nasikia kwenye ugomvi huo kuna wanafunzi walikufa ingawa haikutangazwa.
 

Ibrah, umenikumbusha Mzee Meja (RIP), mzee wa kichagga. Enzi za Mwl Kisamo H/Master kabla ya Andrew Kwayu. Nakumbuka ugomvi wa ASS Vs Tambaza muda mfupi baada ya ujio wa Pope John II hapa TZ. Tulikimbizwa toka Muhimbili P/S hadi fire na vijana wa O'level wa Tambaza!
 
Kwenye huu mjadala huwa nakaaga kimya tu kwa kuwa 'A' level nilisoma Tambaza na 'O' level Azania.This talk is among my biggest conflicts of interest.
 
kuna wakati tambaza tuliongoza nchi nzima! 1990s. nilihamishiwamkoani. kufika kule, tulikuwa wa5 shule mpya, tukatengwa shule yenyewe pia fujoo!!! tukatoroka tuliruka hadi banda la nguruwe, wale nguruwe wakapiga kelele, kila mmoja wetu akamkaba nguruwe mmoja. tukachoka na nguruwe mmoja, pale ndio niliamini kuwa kumbe tulistahili kuhamishwa. YULE NGURUWE tulimnyonga porini. ila tulishindwa kumla. tukaamua kumchoam mzima mzima. duh
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…