Nimeishajiandikisha...! Kituoni nimewakuta wanawake wawili (hawakujitanmbulisha) pembeni ya mwandikishaji wakiume mmoja mwenye kofia ya "Tamisemi". Nimekaribishwa kwa bashasha huku nikiombwa kutaja majina yangu matatu, kisha nikasaini, na nikaambiwa tayari Mimi Sasa ni mpiga kura halali mwaka huu.
Sijaona changamoto yoyote. Twende kujiandisha, tumchague viongozi tunaowataka watuongoze siyo wale tunaotaka watutawale!!