TAMISEMI mjitahidi kutenda haki kwa Walimu wanaojitolea mashuleni

TAMISEMI mjitahidi kutenda haki kwa Walimu wanaojitolea mashuleni

Tate Mkuu

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2019
Posts
33,092
Reaction score
96,127
Lengo la huu uzi ni kutaka tu kuwakumbusha ndugu zangu wa Tamisemi. Baada ya Mh. Rais kuiagiza Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) kuajiri walimu 6000 kutokana na uhitaji ulio sababishwa na vifo na kuacha/kufukuzwa kazi kwa baadhi ya walimu, natarajia zoezi linalo fuata ni kwa hii Wizara husika kutekeleza agizo la Rais Mh. Samia Suluhu Hassani.

Ombi langu kwa Tamisemi ni moja tu! Watoe kipaumbele kwanza kwa walimu zaidi ya 3000 wanao jitolea kwenye shule zetu kwa miaka nenda huku wakiwa na matumaini ya kukumbukwa siku moja katika ajira rasmi za serikali.

Kiufupi walimu hawa wenye elimu ya stashahada na shahada za elimu, wanafanya kazi ya kujitolea katika mazingira magumu sana mashuleni huku wakilipwa posho kiduchu tu ya laki 1 mpaka laki 1 na nusu na wakuu wa shule, lakini pia ile Taasisis ya TAESA kwa mwezi!

Walimu hawa kimsingi ni viumbe wenye moyo sana! Hivyo naomba ikiwapendeza, muwape kipaumbele! Badala ya kujaza ndugu zenu, mashemeji zenu, wake zenu, waume zenu, watoto wenu, ndugu zenu na wale walio wapa rushwa! Huku mkiwaacha watoto wa maskini wakiendelea kuishi kwa matumaini ya kukumbukwa na serikali siku moja. Mkumbuke hawa walimu wengi wanatokea mazingira magumu kiasi cha kuaamua kujitolea!

Nawasihi sana safari hii muache ule ujanja ujanja wenu wa kuchomekea majina hewa, au kurudia majina ya watu kwa makusudi, ili baadae mje mchomekee majina mengine kwa malango wa nyuma. Wapeni nafasi hao walimu elfu 3 kwanza, halafu hao elfu 3 wengine, mnaweza sasa kuangalia vipaumbele vyenu.

Nb: Mimi si mmoja wao. Ila nimeguswa na hawa walimu, pamoja na wale wahitimu wa kada nyingine ambao wanajitolea kufanya kazi serikalini, huku wakilipwa posho ya laki 1 na nusu na hao TAESA kwa ajili ya nauli.
 
Je, hao walimu elfu 6 wanataraji kuwajira ni wa masomo ya sayansi, sanaa au mchanganyiko sayansi na sanaa?
 
Je, hao walimu elfu 6 wanataraji kuwajira ni wa masomo ya sayansi, sanaa au mchanganyiko sayansi na sanaa?
Ni mchanganyiko bila shaka yoyote ile. Na hiyo idadi bado ni ndogo ukilinganisha na mahitaji.
 
Walimu ni tatizo lingine nchi hii..kazi kulia lia mitandaoni kisa ajira za serikali..tambueni serikali haiwezi ajiri graduates wote..fanyeni kazi jitafutieni kipato..ajira ya serikali ikitokea sawa isipo tokea sawa pia.. acheni kulia lia..kwanza wengi wenu ni waunga juhudi hamna misimamo.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni mchanganyiko bila shaka yoyote ile. Na hiyo idadi bado ni ndogo ukilinganisha na mahitaji.
Pasi na shaka watafanya hivyo kikubwa ni kuwaombea dua hasa ukizingatia majina ya hawa vijana kuna kipindi wakuu wa shule waliambia wayatume kwenye idara husika japo kuna zile rafu za hapa na pale za kuchomeka majina ya watu wao ambao ni tofauti na vijana husika.
 
Figisu ni nyingi sana.

Dah!! Cha msingi hapo wapambane tu na mambo mengine, ila siyo kutegemea ajira hizi za kupeana
...kindugu
...rushwa
...nk
 
Serikali imejenga shule nyingi mpya. Ambacho hakijanipendeza ni kuona inawapa nafasi walimu waajiriwa kwenye hizo shule lihali walimu tusiokuwa na ajira na tunajitolea mwaka watatu sasa hatupewi fursa. Ushauri wangu serikali itutazame kwa jicho la tatu tunaojitolea maana moyo wa kujitolea unapungua kasi
 
Back
Top Bottom