Zitto
Former MP Kigoma Urban
- Mar 2, 2007
- 1,562
- 10,888
Tamko la Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo Juu ya Ugonjwa wa Corona
Ndugu Watanzania
A: Utangulizi
Dunia imekumbwa na ugonjwa wa Covid - 19 (maarufu zaidi kama Corona). Nchi yetu kama sehemu ya dunia haijasalimika na kadhia hii. Machi 2, 2020 wakati nikitoa hotuba yangu kwenye kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya ACT Wazalendo niliitaka Serikali ifanye tathmini juu ya athari za kiuchumi za ugonjwa huu, na kwa kuwa katika kipindi husika hatukuwa na maambukizi yaliyoripotiwa nchini, nilitaka tathmini husika ijikite kwenye athari za kukosekana kwa malighafi viwandani (Hasa kutoka nje ya nchi), masoko ya bidhaa zetu nje, bidhaa za vyakula tunavyoagiza kutoka nje, athari kwenye sekta ya usafirishaji, utalii nk, na mjumuisho wa hayo kwenye uchumi wetu.
Juzi Serikali imethibitisha uwepo wa virusi vya Corona hapa Tanzania, na mpaka jana idadi ya wagonjwa iliyosemwa imefikia watu Sita (6), Mmoja kutoka Zanzibar, na watano kutoka Tanzania Bara. Hatua kadhaa za kujaribu kukinga na kupunguza kasi ya maambukizi zimetangazwa kuchukuliwa, ikiwemo kuhamasishaji kunawa kwa sabuni kwenye maji yanayotiririka, kutumia vitakasa (Sanitizers), kuacha kupeana mikono, kuvaa barkoa (masks), kupunguza mikusanyiko, kutenga maeneo maalum kwaajili ya wanaogundulika kupata maambukizi, kufunga shule na vyuo, nk.
Taarifa hii ya uwepo wa wagonjwa nchini inakazia juu ya wito wetu ACT Wazalendo wa Machi 2, 2020, juu ya umuhimu wa kufanya tathmini ya athari za kiafya, kiuchumi na kijamii zitokanazo na janga hili la Corona, pamoja na kuja na hatua za haraka, za kati na za muda mrefu za kuchukua ili kupambana na athari hizo.
B: Hatua za Haraka za Kuchukua Kupunguza Maambukizi Nchini
ACT Wazalendo inaishauri Serikali kuchukua hatua zifuatazo kushughulikia suala hili la kujikinga na maambukizi mapya ya virusi vya Corona:
1. Kuzuia safari za kwenda au kuingia nchini za watu kutoka nchi zilizoathirika zaidi na virusi vya Corona, nchi hizo ni China, Italia, Iran, Uhispania, Ujerumani, Uingereza, Canada, Marekani, pamoja na nchi yoyote ambayo itaonekana kuwa na maambukizi zaidi.
2. Kuwahimiza watu wote waliosafiri kutoka kwenye nchi zenye maambukizi zaidi ya vizuri vya Corona ndani ya wiki tatu zilizopita kujitokeza na kufanyiwa vipimo kubaini kama wana maambukizi ama la. Wale wote watakaokutwa na maambukizi wawekwe kwenye uangalizi maalum pamoja na kuwapima watu wote waliokuwa na miingiliano nao.
C: Hali ya Chakula Nchini na Sukari Viwandani
Tunayo maradhi ya Corona tayari, lakini kabla ya chochote ni Lazima kwanza watu wetu wawe na uwezo wa kula chakula. Nchi yetu (Kwa maana ya Wakala wa Hifadhi ya Chakula Nchini) ina chakula cha kula kila Mtanzania kwa muda wa siku Tatu (3) tu. Sera za Serikali ya awamu ya tano za kutokutoa hela kwaajili ya kununua chakula cha akiba ndio msingi wa uwepo wa akiba ndogo kiasi hicho. Tayari kabla ya uwepo wa Corona athari za uwepo wa akiba ndogo ya chakula kwenye ghala la Taifa zilishaanza kuonekana kwa mfumuko wa bei mkubwa utokanao na kupanda kwa bei ya bidhaa za chakula nchini. Uwepo wa Corona unafanya hali iwe mbaya zaidi, tayari kuna taharuki ya ununuzi wa dharura, jambo ambalo limepandisha bei ya bidhaa nchini.
Pia, Nchi yetu ina nakisi ya uzalishaji wa bidhaa mbili muhimu sana, mafuta ya kula na sukari (Ile ya matumizi majumbani pamoja na ile ya viwandani). Uzalishaji wetu wa ndani hautoshelezi mahitaji ya bidhaa mbili hizo, na hivyo tunatumia wastani wa shilingi bilioni 800 kununua kutoka nje ya nchi. Ni dhahiri kuwa mnyonyoro wa ununuzi na usafirishaji wa bidhaa hizo kutoka nje utakuwa umetibuliwa, hasa kwa kuwa tunatoa bidhaa hizo kutoka Asia na Amerika ya Kusini, mahali ambako athari za Corona ni kubwa kuliko huku barani Afrika.
Tunashauri yafuatayo:
1. Serikali inunue chakula cha dharura cha kuhimili zaidi ya mwezi mmoja kutoka kipindi cha siku tatu cha sasa, na chakula husika kihifadhiwe na kugaiwa bure ama kwa bei nafuu mno pale athari za janga la Corona zitakapodhizi na kuathiri hali ya chakula nchini.
2. Serikali ina wajibu wa kueleza hatua inazochukua kuhakikisha hakuna uhaba wa bidhaa za Mafuta ya Kula na Sukari (ya matumizi ya kawaida na ile ya Viwandani).
3. Serikali ifanye haraka kurudisha fedha za wamiliki wa Viwanda zitokanazo na VAT Returns za Uagizaji wa Sukari viwandani. Fedha hizo ni nyingi (karibu shilingi trilioni moja), na ni malimbikizo ya zaidi ya miaka minne sasa, wenye viwanda wanazihitaji sasa kuliko wakati mwengine wowote.
4. Bunge la Bajeti lijadili tathmini ya hali ya chakula na uzalishaji wa bidhaa za chakula nchini, lipitishe fedha za dharura za ununuzi wa chakula cha akiba, pamoja na kupitisha unafuu wa kikodi kwa waagizaji wa chakula na bidhaa kutoka nje katika kipindi hiki cha dharura.
C: Uwezo wa Sekta Yetu ya Afya (Kibajeti na Rasilimali Watu)
D: Athari za Corona Kwenye Sekta ya Utalii
Tunajua mapendekezo ya kuzuia watu kutoka nchi zenye maambukizi makubwa ya virusi vya Corona nchini yataleta mtikisiko kwenye sekta ya utalii nchini, hivyo kwa upekee tuna mapendekezo kadhaa ya kujaribu kupunguza makali ya kiuchumi yatokanayo na hatua hizo za kuzuia watu kuingia nchini.
Uchumi wa Tanzania unategemea kwa kiasi kikubwa sana ufanisi wa Sekta ya Utalii nchini, 25% ya mapato yetu ya fedha za kigeni yanatokana na sekta hii, wastani wa Dola za Marekani 2.5 bilioni kwa mwaka, na kwa sababu ya upana wake sekta hii ina ajira zaidi rasmi na zisizo rasmi kwa wananchi wetu, kuanzia wafanyakazi wa mahoteli, wauza bidhaa kwenye mahoteli, wapishi, watembeza watalii, madereva nk. Ni mnyororo mpana wa shughuli za kiuchumi ambao utaathirika sana kutokana na maambikizi haya ya virusi vya Corona.
ACT Wazalendo tunaishauri Serikali kufanya yafuatayo:
Kjhggg 1. Serikali ikutane na Wafanyabiashara wote kwenye sekta ya Utalii, pamoja na Vyama vya Wafanyakazi kwenye sekta husika. Lengo liwe ni kupata tathmini ya Pamoja ya madhara ya mlipuko huu kwa sekta ya Utalii na huduma zake.
2. Serikali itengeneze mpango maalum wa kuhakikisha ajira za wafanyakazi katika sekta ya Utalii hazipotei, kwa aidha kutoa Unafuu|Msamaha wa Kodi zote ama kwa kuwafidia (stimulus package) wafanyabiashara gharama wanazoingia kwa kuwalipa mishahara wafanyakazi katika kipindi ambacho hawatakuwa na biashara. Lengo ni kuzifanya biashara husika zisife.
3. Serikali kuja na mpango maalum wa kuhakikisha mabenki yenye mikopo ya wafanyabiashara na wafanyakazi wa sekta ya utalii yanatoa kipindi maalum cha msamaha wa kulipa mikopo hiyo kati ya miezi sita na mwaka mmoja. Lengo likiwa ni kupunguza mikopo chechefu (NPL) pamoja na kuzuia kupotea kwa mali za wafanyabiashara na wafanyakazi walio kwenye sekta ya Utalii.
D: Hitimisho
Kwa wakati husika bado athari za Maambukizi ya virusi vya Corona hayajagusa kiundani sekta ya afya, na hivyo ni vigumu kujua athari na mapungufu yetu ya kimaandalizi. Ni matarajio yetu kuwa Serikali italeta bungeni mpango Kazi wa kuonyesha utayari wetu wa kupambana na janga hili, pamoja na Bajeti ya dharura ya utekelezaji wa mpango Kazi husika.
Kabwe Z. Ruyagwa Zitto
Kiongozi wa Chama, ACT Wazalendo
Dar Es Salaam
Machi 20, 2020
Ndugu Watanzania
A: Utangulizi
Dunia imekumbwa na ugonjwa wa Covid - 19 (maarufu zaidi kama Corona). Nchi yetu kama sehemu ya dunia haijasalimika na kadhia hii. Machi 2, 2020 wakati nikitoa hotuba yangu kwenye kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya ACT Wazalendo niliitaka Serikali ifanye tathmini juu ya athari za kiuchumi za ugonjwa huu, na kwa kuwa katika kipindi husika hatukuwa na maambukizi yaliyoripotiwa nchini, nilitaka tathmini husika ijikite kwenye athari za kukosekana kwa malighafi viwandani (Hasa kutoka nje ya nchi), masoko ya bidhaa zetu nje, bidhaa za vyakula tunavyoagiza kutoka nje, athari kwenye sekta ya usafirishaji, utalii nk, na mjumuisho wa hayo kwenye uchumi wetu.
Juzi Serikali imethibitisha uwepo wa virusi vya Corona hapa Tanzania, na mpaka jana idadi ya wagonjwa iliyosemwa imefikia watu Sita (6), Mmoja kutoka Zanzibar, na watano kutoka Tanzania Bara. Hatua kadhaa za kujaribu kukinga na kupunguza kasi ya maambukizi zimetangazwa kuchukuliwa, ikiwemo kuhamasishaji kunawa kwa sabuni kwenye maji yanayotiririka, kutumia vitakasa (Sanitizers), kuacha kupeana mikono, kuvaa barkoa (masks), kupunguza mikusanyiko, kutenga maeneo maalum kwaajili ya wanaogundulika kupata maambukizi, kufunga shule na vyuo, nk.
Taarifa hii ya uwepo wa wagonjwa nchini inakazia juu ya wito wetu ACT Wazalendo wa Machi 2, 2020, juu ya umuhimu wa kufanya tathmini ya athari za kiafya, kiuchumi na kijamii zitokanazo na janga hili la Corona, pamoja na kuja na hatua za haraka, za kati na za muda mrefu za kuchukua ili kupambana na athari hizo.
B: Hatua za Haraka za Kuchukua Kupunguza Maambukizi Nchini
ACT Wazalendo inaishauri Serikali kuchukua hatua zifuatazo kushughulikia suala hili la kujikinga na maambukizi mapya ya virusi vya Corona:
1. Kuzuia safari za kwenda au kuingia nchini za watu kutoka nchi zilizoathirika zaidi na virusi vya Corona, nchi hizo ni China, Italia, Iran, Uhispania, Ujerumani, Uingereza, Canada, Marekani, pamoja na nchi yoyote ambayo itaonekana kuwa na maambukizi zaidi.
2. Kuwahimiza watu wote waliosafiri kutoka kwenye nchi zenye maambukizi zaidi ya vizuri vya Corona ndani ya wiki tatu zilizopita kujitokeza na kufanyiwa vipimo kubaini kama wana maambukizi ama la. Wale wote watakaokutwa na maambukizi wawekwe kwenye uangalizi maalum pamoja na kuwapima watu wote waliokuwa na miingiliano nao.
C: Hali ya Chakula Nchini na Sukari Viwandani
Tunayo maradhi ya Corona tayari, lakini kabla ya chochote ni Lazima kwanza watu wetu wawe na uwezo wa kula chakula. Nchi yetu (Kwa maana ya Wakala wa Hifadhi ya Chakula Nchini) ina chakula cha kula kila Mtanzania kwa muda wa siku Tatu (3) tu. Sera za Serikali ya awamu ya tano za kutokutoa hela kwaajili ya kununua chakula cha akiba ndio msingi wa uwepo wa akiba ndogo kiasi hicho. Tayari kabla ya uwepo wa Corona athari za uwepo wa akiba ndogo ya chakula kwenye ghala la Taifa zilishaanza kuonekana kwa mfumuko wa bei mkubwa utokanao na kupanda kwa bei ya bidhaa za chakula nchini. Uwepo wa Corona unafanya hali iwe mbaya zaidi, tayari kuna taharuki ya ununuzi wa dharura, jambo ambalo limepandisha bei ya bidhaa nchini.
Pia, Nchi yetu ina nakisi ya uzalishaji wa bidhaa mbili muhimu sana, mafuta ya kula na sukari (Ile ya matumizi majumbani pamoja na ile ya viwandani). Uzalishaji wetu wa ndani hautoshelezi mahitaji ya bidhaa mbili hizo, na hivyo tunatumia wastani wa shilingi bilioni 800 kununua kutoka nje ya nchi. Ni dhahiri kuwa mnyonyoro wa ununuzi na usafirishaji wa bidhaa hizo kutoka nje utakuwa umetibuliwa, hasa kwa kuwa tunatoa bidhaa hizo kutoka Asia na Amerika ya Kusini, mahali ambako athari za Corona ni kubwa kuliko huku barani Afrika.
Tunashauri yafuatayo:
1. Serikali inunue chakula cha dharura cha kuhimili zaidi ya mwezi mmoja kutoka kipindi cha siku tatu cha sasa, na chakula husika kihifadhiwe na kugaiwa bure ama kwa bei nafuu mno pale athari za janga la Corona zitakapodhizi na kuathiri hali ya chakula nchini.
2. Serikali ina wajibu wa kueleza hatua inazochukua kuhakikisha hakuna uhaba wa bidhaa za Mafuta ya Kula na Sukari (ya matumizi ya kawaida na ile ya Viwandani).
3. Serikali ifanye haraka kurudisha fedha za wamiliki wa Viwanda zitokanazo na VAT Returns za Uagizaji wa Sukari viwandani. Fedha hizo ni nyingi (karibu shilingi trilioni moja), na ni malimbikizo ya zaidi ya miaka minne sasa, wenye viwanda wanazihitaji sasa kuliko wakati mwengine wowote.
4. Bunge la Bajeti lijadili tathmini ya hali ya chakula na uzalishaji wa bidhaa za chakula nchini, lipitishe fedha za dharura za ununuzi wa chakula cha akiba, pamoja na kupitisha unafuu wa kikodi kwa waagizaji wa chakula na bidhaa kutoka nje katika kipindi hiki cha dharura.
C: Uwezo wa Sekta Yetu ya Afya (Kibajeti na Rasilimali Watu)
D: Athari za Corona Kwenye Sekta ya Utalii
Tunajua mapendekezo ya kuzuia watu kutoka nchi zenye maambukizi makubwa ya virusi vya Corona nchini yataleta mtikisiko kwenye sekta ya utalii nchini, hivyo kwa upekee tuna mapendekezo kadhaa ya kujaribu kupunguza makali ya kiuchumi yatokanayo na hatua hizo za kuzuia watu kuingia nchini.
Uchumi wa Tanzania unategemea kwa kiasi kikubwa sana ufanisi wa Sekta ya Utalii nchini, 25% ya mapato yetu ya fedha za kigeni yanatokana na sekta hii, wastani wa Dola za Marekani 2.5 bilioni kwa mwaka, na kwa sababu ya upana wake sekta hii ina ajira zaidi rasmi na zisizo rasmi kwa wananchi wetu, kuanzia wafanyakazi wa mahoteli, wauza bidhaa kwenye mahoteli, wapishi, watembeza watalii, madereva nk. Ni mnyororo mpana wa shughuli za kiuchumi ambao utaathirika sana kutokana na maambikizi haya ya virusi vya Corona.
ACT Wazalendo tunaishauri Serikali kufanya yafuatayo:
Kjhggg 1. Serikali ikutane na Wafanyabiashara wote kwenye sekta ya Utalii, pamoja na Vyama vya Wafanyakazi kwenye sekta husika. Lengo liwe ni kupata tathmini ya Pamoja ya madhara ya mlipuko huu kwa sekta ya Utalii na huduma zake.
2. Serikali itengeneze mpango maalum wa kuhakikisha ajira za wafanyakazi katika sekta ya Utalii hazipotei, kwa aidha kutoa Unafuu|Msamaha wa Kodi zote ama kwa kuwafidia (stimulus package) wafanyabiashara gharama wanazoingia kwa kuwalipa mishahara wafanyakazi katika kipindi ambacho hawatakuwa na biashara. Lengo ni kuzifanya biashara husika zisife.
3. Serikali kuja na mpango maalum wa kuhakikisha mabenki yenye mikopo ya wafanyabiashara na wafanyakazi wa sekta ya utalii yanatoa kipindi maalum cha msamaha wa kulipa mikopo hiyo kati ya miezi sita na mwaka mmoja. Lengo likiwa ni kupunguza mikopo chechefu (NPL) pamoja na kuzuia kupotea kwa mali za wafanyabiashara na wafanyakazi walio kwenye sekta ya Utalii.
D: Hitimisho
Kwa wakati husika bado athari za Maambukizi ya virusi vya Corona hayajagusa kiundani sekta ya afya, na hivyo ni vigumu kujua athari na mapungufu yetu ya kimaandalizi. Ni matarajio yetu kuwa Serikali italeta bungeni mpango Kazi wa kuonyesha utayari wetu wa kupambana na janga hili, pamoja na Bajeti ya dharura ya utekelezaji wa mpango Kazi husika.
Kabwe Z. Ruyagwa Zitto
Kiongozi wa Chama, ACT Wazalendo
Dar Es Salaam
Machi 20, 2020