"Tamko la Pinda"


Just speak for yourself dude/ dudette..............

Halafu bado hujui sababu iliyomfanya Pinda azidiwe na hisia bungeni, kwa hiyo funga bakuli!
 


Duu, hii imenipeleka shule ya msingi enzi hizo fulani hajazaliwa. Kulikuwa na vile vitabu vya MALIMWENGU, ila sikumbuki namba. Jamaa waliokolewa kutoka kwenye mikono ya zimwi. Mazimwi walivyokuja kushtuka jamaa haoo wako hewani. Wakaishia tu kusema "Nyama yetu inakwenda......" na hapo vumbi likatimka, jamaa wakikimbilia NYAMA YAO. Sasa huyu Kuku wa graduation, mtu anapoteza maisha, jamani!!! Kweli Tanzania nchi masikini. Kibaya zaidi Mnauwa mtu, kisa kaiba kuku wa PASAKA. Sasa hata PASAKA haina maana tena.
 
Hujui kwa uhakika ni nini kilichomfanya Pinda kuonyesha hisia.

Nyani...Ni speculations tu...Wengine wanadai alilia uwaziri mkuu,wengine wanadai alilia albinos na wengine wanaamini alilia kwasababu alishindwa kufanya something.
Mimi sina haja ya kujua ni kwanini hasa alionyesha hisia ila outcome za hii back and forth certainly unaweza ukatabiri based on your knowledge kuhusu wananchi wa Tanzania.
 
Mfumo dume!!

angalia maneno yako huko nyuma...

Wewe nitajie basi, mwanamke au mwanamme, toka the founding of the nation, mtu aliyekumbwa na public repudiation akaenda kulia kwenye stage.

sijawajui wote waliowahi kukumbwa na Public repudiation? so you tell me wote ambao walilkutwa na public repudiation tangu kuundwa kwa taifa letu.


Ulimbukeni!

Haifanyi hoja yako kuwa na nguvu, bali kunathibitisha udhaifu wake.


Ulinganishe na nani? Sio lazima utupime na wengine.

Ni wewe unayetulinganisha na watu wengine. Kumbuka unasema kina nani wanatabia ya kulia hadharani...!

Sisi Watanzania, bila kuangalia through the prism ya tamaduni nyinginge, sisi wenyewe hatulilii hadharani tukikumbwa na kashfa!!

wewe na nani?



Pinda kafungua dimba la kitabia cha kutumia pulpit kujilizaliza amidst a public debacle. Kama kuna mwingine nitajie basi!!!

angalia jibu langu hapo juu.




"Character"? Nani kasema Pinda ana luck character? Nimesema Pinda is erratic.

Yuko erratic kwa sababu analia, au erratic kwa sababu kasema vitu vya hatari. I know your answer.

Sisumbuliwi na kile alichosema? Sasa kwa nini ningesema Pinda hana judgment to hold the office of Prime Minister?

kwa sababu umesema analia hadharani. Angalia tena sentensi yako.
 

Hehehee....why do I sometimes think you are his (you know who) twin brother from another mother....

Aisee back and forth na Kuhani ni endless....unless una muda sana leo la sivyo mtaendelea kujaza "bandwidth" bure....
 

Angalau wewe ume man up na kukubali kuwa ni speculations tu....
 

Sikonge unajuwa hii issue inanishangaza sana..Hizi na kesi za mauwaji PERIOD.

Kuwekwa neno albino ndio kunawafanya watanzania waanze kurudi kule wanapopapenda...Udaku,ushirikina nk...Hakuna tena kufanya kazi kisayansi,uchunguzi wa kisayansi na wauwaji weswekwe ndani kwa mauwaji hakuna.

Sasa ndio maana ukaona move ya serikali ikawa ni kuwafungia waganga wa jadi...Yani serikali hata kama wananchi wake wengine wako nyuma basi nao wanakaa nao hivyo hivyo tu...Hawamshiki kipofu mkono,kwasababu kama kesi hizi zingeshughulikiwa kama kesi nyingine za mauwaji waganga wa kienyeji wangefungiwa wa nini...?Kama muuwaji ni muuwaji tu awe mganga wa kienyeji ama askari ama jambazi ama raia mwingine yoyote yule....Sheria ni msumeno.

Wananchi wapigwe msasa kwanza kuhusu haki zao na wapewe elimu serikali iweke msisitizo kwenye sayansi na shughuli za uzalishaji wananchi watumie rasilimali zao...Hilo ndo tatizo hakuna kazi na utajiri na mafanikio huwezi kupata mahali ambako hakuna shughuli za kiuchumi hilo serikali inafahamu...Jamii ndiyo ya kubadilishwa...Kama wananchi hawana pa kukimbilia kwenda kuomba kazi wanabakia kufanya mambo kama hayo kukimbilia waganga,wengine wanakimbilia dini nk...Sisi hapa JF ni lazima tujadili issue hii kwa namna ya tofauti na si kuwa nani alilia na nani hakulia na ni kwanini alilia nk.

Maneno aliyoyasema Pinda hapo awali kwa kusema ukweli ni maneno ambayo yalikuwa yam cost,hata kama wananchi wange sympathise lakini bunge lilitakiwa limpige chini kama uwezekano huo upo.

Lakini kwa jinsi issue ilivyokaa ni wazi kuwa siasa zitaingizwa...Na siasa zikaingizwa utakuja kuona pale mfano huo wa kuku unapokuja kutumika...Je wananchi hao wanaouwa vibaka wa kuku watamsikiliza ama ku connect na nani?

Ndio maana ninasema lazima kuwepo na mkakati maalum wa kuibadili jamii yetu na kwa kuanzia ni kuwekeza ili watu wawe busy kufanya kazi na kushop badala ya kwenda kwa waganga ili wapate kazi,pesa nk.
 
Maneno aliyotumia Pinda kuomba radhi:

Version 1:
Kama mnaona kile nilichofanya ni makosa naomba mnivumilie. Naomba Mungu anisamehe kama nimewakosea
- yeye haaamini kuna makosa.. ni nyinyi "mnaona"


Version 2:
(Habari Leo) Huku akifuta machozi, aliendelea kusema iwapo kuna Mtanzania ambaye anaona kuwa ametenda uovu kuliko maovu yote katika suala hilo la albino na iwe hivyo, lakini nia yake ilikuwa nzuri
- Kamwe hakusema hilo!


Version 3: - what?

version 4:
(Gazeti la Mwananchi) Kama mnaona kile nilichofanya ni makosa naomba mnivumilie. Naomba Mungu anisamehe kama nimewakosea
-

Version 5:

Je Pinda alisema nini katika kuomba msamaha? Wakati mwingine Kuhani anakuwaga na point yaani hata kusikiliza hotuba yenyewe inakuwa ngumu? Sikiliza alichosema Pinda uamue mwenye kati ya hizo version tano ni NINI HASA pinda alisema? BONYEZA HAPA KUSIKILIZA
 
Damn! I'm dizzy......

Oh yeah...."wakati mwingine" Kuhani huwa ana pointi kama ilivyo watu wengi...
 
Damn! I'm dizzy......

Oh yeah...."wakati mwingine" Kuhani huwa ana pointi kama ilivyo watu wengi...

hahahaha... si unajua hata Obama alipobadilisha kauli yake ya Januari 8 aliposema kuwa ni "serikali" ndiyo itakayoondoa hali hii mbaya ya kiuchumi na na kuleta hii ya Jan 28 kuwa ni watu wenyewe wanaweza kufanya hivyo na kusound kama Reagan hata profesa alimpa kudos..
 

Nimeanza kurudisha imani yangu kwa PINDA baada ya kuanza kutetereka kufuatia matamshia yake kuhusu UNUNUZI WA MASHANGINGI na HILI LA NDUGU ZETU MAALBINO...

Kwa wale mnaovalia njuga Pinda kujiuzulu nadhani mnakuwa hamtendei haki Tanzania yetu. Ni muhimu kutambua kuwa alichokifanya Pinda kina maslahi makubwa katika mustkabali wa tamaduni za uongozi katika nchi yetu. Tutakapoendelea kushikia bango tutakuwa tunawaambia viongozi wengine wasithubutu kujirudi na kuomba radhi watanzania. Tulifanya kosa hili na Zakia Meghji. Tusirudie kosa tena. Tulinde utamaduni huu wa kukubalia makosa na kuomba radhi ambao bado unachipukia katika psych ya utamaduni wa kisiasa katika nchi yetu....

Tanzanianjema
 
Pinda alisema ni wananchi ndio watakaoamuwa...Sasa serikali inasubiri maoni ya wananchi ama ina maana wakati wa kupiga kura?

 
Steve, my brother from another mother. Naomba nikusahihishe kidogo. Mimi sio hasimu mkuu wa Kuhani. Hajawahi kunifanyia lolote baya maishani mwangu na mimi as far as I'm concerned, sijawahi kumfanyia lolote baya maishani mwake. Sidhani kama namjua au yeye kunijua. Kwa hiyo basi, in all seriousness siwezi kuwa adui yake. Alivyo yeye ni ndivyo alivyo. Sijui kama in real life yuko hivyo au vipi. Hilo sijali sana kwani kama nisemavyo mara kwa mara, hapa ni mtandaoni tu. Ukianza kuyachukulia mambo ya hapa serious kihivyo utakuwa huna maisha. Kwa hiyo basi, mimi binafsi huwa sichukulii mambo mengi yaandikwayo hapa kuhusu mimi au niandikayo kuhusu watu wengine kuwa na umuhimu na maana hivyo. Hakuna mtu aitwaye Nyani Ngabu in real life. Nyani Ngabu is just a mythical figure. Anybody can be Nyani Ngabu. So be easy my brother....
 
Hapa naona wachawi wameingia. Hivi mapambano ya kuwalinda Albino yatapata mafanikio kweli?
 
Naamini itabidi ifike kipindi tutofautishe "symphathy na sheria" tunaendekeza sana sentiments katika swala ambalo liko straight forward.

Wengi wetu humu tunamtetea Pinda kwa sababu "kaomba msamaha". Lakini jamani tunaelewa mtu kama Pinda nafasi yake katika jamii yetu? Tunajua kwamba Pinda ni Waziri Mkuu? Tunajua kwamba ni huyu aliyeapa kuilinda na kuitetea katiba ya nchi yetu? unajua kwamba Katiba inawalinda wahalifu na wasio waharifu? What message are you sending unaposema kwamba watu wauawe?

Lets go back, tunaposema utawala wa sheria tunakuwa na maana gani? au ni yale yale..tunakuwa na double standards. Kwamba fulani kaomba msamaha kwa hiyo aachwe apumzike? By the way..wengi mnalichukulia hili kama utani..lakini Prime Minister kusimama jukwaani na kusema fulani akiua auawe..somthing is wrong . very wrong. Implication yake ni kubwa. Jiulize watu watamfikiriaje akiongelea kitu kama Human Rights au Death Penalty? kesho Pinda akienda Umoja wa mataifa atasimama kwenye podium kulaani matumi ya nguvu dhidi ya watu fulani? media za zinaweka kumbukumbu. I mean..implications ya kauli kama za akina Pinda ni kubwa mno. Hatuwezi kukaa na kusema kwamba jamaa "aachwe kwa sababu kaomba msamaha"

Accountability demands consequences. Leo Lowassa, Yona, Mramba et al..wakisema tunaomba msamaha..tulifanya makosa..tutawasamehe? au Pinda anasamehewa kwa sababu alitoa kauli tuu ambayo "haidhuru"

Personally I respect and admire Pinda.

Lakini watanzania wenzangu tuache double standards. When we see the Prime Minister advocating for the breach of the rule of law..na sisi tunaingia mkenge na kuanza kumtetea..nadhani tunaset precedent mbaya sana.

All in all, this should be a lesson kwa wengi wetu. Tunapolilia utawala wa sheria au Rule of law..ni mambo kama haya! Sheria na huruma havina ukoo. Personally I cant take him serious when he is advocating the breach of our sacred document! Katiba.

I can ASSURE YOU, hii ingekuwa huko Europe au kwingineko..Pinda wouldnt have gone away with it!

Anyway tuliache. Ila tujifunze kitu katika hili swala zima.

Masanja,
 
Hivi alichosema Pinda kina tofauti gani na "Shoot to kill" orders zinazotolewa na viongozi wa nchi mbalimbali zinapotokea riots au looting.... Maana hizi tumeziona sehem nyingi tu including the U.S, na main reason ni kukill the malicious few, in order to protect the welfare of many.

Naomba msaada.
 
Je Pinda alisema nini katika kuomba msamaha? Wakati mwingine Kuhani anakuwaga na point yaani hata kusikiliza hotuba yenyewe inakuwa ngumu? Sikiliza alichosema Pinda uamue mwenye kati ya hizo version tano ni NINI HASA pinda alisema

Mwanakijiji,

Naona, for once, ume-appreciate baadhi ya ninavyovisema kuhusu press ya Tanzania. Ahsante.

Katika hotuba ya Pinda, kwa hisani ya media outlet yako, na kwa hapa ahsante tena, kuna makorokosho mengine ya kizushi kutoka press yenu. Classic example:

PINDA: Kiliniumiza sana mimi nilipoona Bunge la Jumuiya ya Ulaya eti ndio linatoa azimio kujaribu kulaani mauaji ya albino. Sikulipenda sana. Ingawa tulisema wamefanya jambo jema. Sikulipenda tu kwa sababu walionekana kana kwamba wao wanaelewa vizuri zaidi juu ya tatizo hili kuliko sisi wenyewe Watanzania.

MWANANCHI: Alielezea pia kuhuzunishwa zaidi na tamko la Bunge la Jumuiya ya Ulaya (EU) la kulaani mauaji hayo, kana kwamba wao wanaguswa sana na suala hilo kuliko Serikali ya Tanzania.

Tafsiri ya gazeti ukiisoma utadhani Pinda kasema wa-Ulaya wanajifanya wanaumizwa kuliko sisi na wamemhuzunisha. Kumbe kasema walichofanya European Union ni sawa, ila hapendi hii state of affairs inayooneka kana kwamba wao wanayajua haya kuliko sisi. Tatizo ni sisi! Sasa jamani mtu kweli unashindwa kutafsiri kisentesi kimoja cha Pinda hapo kweli? How kilaza can you be yani? How mtupu ?

Lakini na wewe Mwanakijiji kabla hujakosoa huo msamaha wa Pinda wa "kama nimekosea," inabidi uanze kwa kusema kwamba taarifa uliyoileta hapa kwamba kuna unconditional apology on the way inapotosha, vinginevyo usingerudi kwenye ile original sham apology.

Ile taarifa uliyoweka hapa imechota watu kibao, Pinda heko, Pinda ka-apologize, Pinda hivi na vile, halafu sasa unarudi kwenye original qualified apology ya "kama nimekosea." Na wewe unachangia confusion ama upotoshaji wa putrid news outlets za Tanzania.
 
Mwanakijiji,

Naona, for once, ume-appreciate baadhi ya ninavyovisema kuhusu press ya Tanzania. Ahsante.

I'm the most open minded person... natofautiana na wewe mara nyingi unapozungumze with haste generalizations and condemnations. Huna balance unapokosoa kitu kwako kitu ni either x or z hakuna abcde... Na hata hicho ulichokisema tumeshanyoshea kidole mara kadhaa hapo nyuma ndiyo maana nilitaka nisikie Waziri Mkuu amesema nini kuliko kusoma kwenye magazeti tu watu wakaja kunilaani kuwa nataka ninunue habari ili iwe nini.

Katika hotuba ya Pinda, na kwa hapa ahsante tena kwa hisani ya media outlet yako, kuna makorokosho mengine ya kizushi kutoka press yenu.
Huo hapo ndipo mfano ninaouzungumzia... tayari press imekuwa "yenu".. sasa kama ni yetu kwanini usiiache tu?




umeisoma ile taarifa mwanzoni na mwishoni nimeandika nini. Of course not.


kaisome tena...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…