Tamko la Tanganyika Law Society(TLS), Juu ya Wimbi la Pili la Mlipuko wa Ugonjwa wa Korona nchini

Status
Not open for further replies.

Kutegemea Serikali iliyotufikisha hapa kubadilika kwa kuishauri tu, itakuwa kusubiria embe dodo kwenye mnazi.

Tuwape muda maalum (deadline) serikali na waliotajwa wote kwenye waraka huu kuyafanyia kazi yote yaliyomo katika waraka huu.

Yote ni mema sana, ISIPOKUWA hili la KUPIGA NYUNGU.

Hili la nyungu ni moja ya hayo yanayokosa mashiko kisayansi katika kupambana na janga hili yaliyo tufikisha hapa tulipo.
 
Hujanielewa mkuu,
kuna uwezekano kuwa kuna sheria zimevunjwa za uhujumu uchumi.

Kwa jinsi walivotuongoza kizembe zembe na wanalipwa pesa za uma huoni kuwa wametuhujumu!?

Kwa nn sasa wasisimamishwe ktk nafasi zao kwa kupisha uchunguzi na washtakiwe wakikutwa na tuhuma?
 
UVIKO HAUPO.
KILA MMOJA ACHUKUE TAHADHARI KWA KUFUATA USHAURI WA WATAALAMU WA AFYA KUHUSU KUJIEPUSHA NA MAAMBUKIZI YA UVIKO.

ZINGATIA LISHE BORA, MAZOEZI NA TIBA MBADALA ILI KUKABILIANA NA UVIKO.

Kwa maoni yangu, mwenye akili atafahamu kinachosemwa hapo.

Serikali kutamka UVIKO UPO, haitaishia hapo. Kinachofuata ni namna gani inakabiliana nao. Watanzania tulip wengi, hayo masharti ni balaa kuliko UVIKO wenyewe.

Mwenye mashaka na afya/uhai wake, aji- lockdown mwenyewe. Hawa TLS wasitake kutuletea dhahama
 
Na ambao hawana mashaka wafe tu?

Wakiendelea kufa tu, hiyo serekali itapata wapi pesa/kodi za kujengea miundombinu?

Kwenye tamko la t.l.s. limeonyesha vifungu vya sheria vinavyoielekeza serekali kulinda usalama wa raia wake.

Ni wajibu wa serekali kuongoza na kuonyesha njia ktk mapambano yeyote kama taifa.

Wewe unataka waendelee kusema haipo na wasichukue hatua yeyote?
Kwa faida ya nani?
 
Wimbi la pili la Corona ni manyunyu tu kwa sababu baada ya serekali kukataa chanjo, kirusi kimepata uwanja mzuri zaidi wa kufanya mutations ili kuzalisha variants wa wimbi la tatu na wimbi la nne ambalo litakuwa baya zaidi.

Tulivyokuwa tunamkataa Farao hawa TLS walikaa pembeni wakifikiri ya kuwa wapo salama.Wajiandae kunyang'anywa haki zao za kuishi zaidi na zaidi kwani the worst is yet to come!
 

Mkuu tuko pamoja. Niliandika kukazia ulichokuwa umeandika wewe. Bahati mbaya Android inatabia ya kiherehere kuingiza vijimaneno bila ridhaa ya mwandishi.

Nime edit na nina paste in italics hapa chini. Mkuu nina usongo sana na hawa jamaa. Kwa sababu yao, leo hii wengi ambao hayajatukuta, nasi ni marehemu tu, tunaotembea:

Kutegemea Serikali iliyotufikisha hapa kubadilika kwa kuishauri tu, itakuwa kusubiria embe dodo kwenye mnazi.

Tuwape muda maalum (deadline) serikali na waliotajwa wote kwenye waraka huu kuyafanyia kazi yote yaliyomo katika waraka huu.

Yote ni mema sana, ISIPOKUWA hili la KUPIGA NYUNGU.

Hili la nyungu ni moja ya hayo yanayokosa mashiko kisayansi katika kupambana na janga hili yaliyo tufikisha hapa tulipo.
 
Asante TLS. Mwiguru kaumbuka na uwaziri wake wa Sheria na Katiba. Watu wamesimamia profession Yao bila kuogopa vitisho vyake vya kunifurahisha stone.
 
Tukishawapa deadline alafu ikapita bila kuchukua hatua yeyote tunawafanyaje?
 

Hawajambo Lumumba?

 
Tukishawapa deadline alafu ikapita bila kuchukua hatua yeyote tunawafanyaje?

Hii nchi si ya mtu binafsi au genge fulani na hasa la wahalifu.

Deadline ya kufanyia kazi yaliyo mema namna hii ikipita, itakuwa ni lazima kuchukua hatua.

Waungwana husema, lazima tuchukue hatua kama vile tutakavyoona inafaa.
 
Too little too late,
Mmechelewa sana,au ndio mlikuwa mnasubiri uteuzi!?
Mwaka jana,watu walivaa barakoa,karantini zilifsnywa,lakini Ugonjwa ukasambaa,sasa hapa Cha muhimu tusifunge mipaka,na lockdown,tutakufa kwa njaa,huu Ugonjwa tujifunze kuishi nao,
 
Reactions: rbt
Naona TLS tayari imeanza mashambulizi,kimsingi hizi ni tuhuma za TLS kwa serikali,na sio ushauri kwa serikali. point ya ku note katika walaka wao huu ,serikari imekiuka sheria ya haki na utawala Bora.kimsingi hizi ni shutuma na sio ushauri.kuna Jambo wanalitafuta,ila naiamini serikali Ina watendaji wazalendo na weledi watakaa nao kwa hekima.TLS Wanakowlekea sio kwema kabisaaaa.
 
Mimi naona wametimiza jukumu lao la msingi kwa mujibu wa katiba
 
Tulivyokuwa tunamkataa Farao hawa TLS walikaa pembeni wakifikiri ya kuwa wapo salama.Wajiandae kunyang'anywa haki zao za kuishi zaidi na zaidi kwani the worst is yet to come![emoji848][emoji848][emoji2827][emoji2827]
 
Hii nchi si ya mtu binafsi au genge fulani na hasa la wahalifu.

Deadline ya kufanyia kazi yaliyo mema namna hii ikipita, itakuwa ni lazima kuchukua hatua.

Waungwana husema, lazima tuchukue hatua kama vile tutakavyoona inafaa.
Natamani sana kuzifahamu hizo hatua za kuichukulia serikali isiyowajibika juu ya wananchi wake kama TLS walivyoelezea.
Kama bunge linashindwa kuiwajibisha serikali ikiwa na mamlaka kamili ya kikatiba, sisi tutachukua hatua gani?!
 
Wanasheria inaonekana wanajua tatizo linalotukabili kuliko madaktari waliofuzu MUHAS na UDSM - Faculty of Medicine - Muhimbili Campus hapo kale iliyokuwa chini ya Prof. Mutabaji
Ukiwa mpumbavu usilazimishe upumbavu wako kwa wengine.

Madaktari ndio waliowapima hao marehemu na wagonjwa kuwaeleza Hali zao

Madaktari hawana forum kisheria ya kueleza umma tofauti na TLS ambao wameeleza kutekeleza jukumu lao kwa mujibu wa sheria.
 
Halafu hao MAT sina hakika kama Wana hata vifaa binga
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…