Tamu na chungu ulizopitia wakati unaanza biashara yako

Yes details ndogondogo mara nyingi tunazidharau lakini ndozenye maana kwenye biashara mkuu,haikuwa rahisi maana nilikata mpk mtaji wenyewe lakini nilisimama tena now namshukuru Mungu

Katika ufugaji

ni bora ufuge mbwa wa kisasa watakulipa haraka na hawakupi stress na siyo kuku wa kisasa masharti kibao

wahenga wanasema ujinga ni kwenda tu na siyo kurudi

pambana.
 
Mwaka jana kuna jamaa alinipa wazo labiashara yampunga. Nikazama chimbo kwakupewa maelezo2. Nikashuka stendi ndio nikazama chimbo maporini kwamguu tena kwakupewa maelezo2 njiani nasindikizwa nakelele zandege nawanyama wadogowadogo kama nyani wengine sikuwatambua, nanilikuwa natembea huku naogopa sana.

Nilitembea zaidi yamasaa matatu ndio nikawa nimefika hilo eneo nandio nadhani ilikuwa mara yangu yakwanza kutembea huo umbali kwamguu tena porini.

Wakati natembea nikawa najiwazia kumbe hela kuipata sio mchezo, acheni wenye pesa wawe wagumu kumbe kuna wengine wamepitia misoto mikali.

Nilipofika nilinunua mzigo kama wamilioni 1 na laki 5 nikasafirisha kwapunda kutwa nzima mpaka senta, Kesho yake nikapakia kwenye gari mpaka mjini. Siku hiyo hiyo nikafika nakuuza wateja wakufikia2 nikapata faida kama laki 3. Kiukweli nilijiona mjanja sana biashara ndani yasiku 3 faida laki 3 yaani wastani walaki 1 kila siku. Nikasema kumbe hii ndio biashara namkumbuke ilikuwa ndio mara yangu yakwanza so hasara ya hiyo biashara bado sikuijua.

Sikulaza damu siku yapili huyo tena, safari hii nilichukua pikipiki yahome maana njia zote nilishazijua. Nikajaza mafuta mpaka chimbo, kama kawaida nikanunua mzigo nikapakia kwenye gari, kwabahati mbaya gari ikazama njiani siku tatu gari lipo njiani siku yanne (4) kupiga simu mjini naambiwa bei yamchele imeshuka kutoka 1700 mpaka 900 kwa elfu 1000 tena hii elfu moja mchele wako unatakiwa uwe mzurii sana.

Nilichanganyikiwa, kupiga hesabu zangu hapo tayari nahasara maana trip hii nilinunua mpunga mwingi ili ile faida yalaki 3 niidable ili nipate laki 6.

Kiukweli nilipata hasara nafaida yangu ile laki 3 yakwanza ndio nikafidishia mabonde ila bado nikawa nimekula hasara.
 
Inachu

Inachukua Muda gani ili uwe kwenye mtelezooo

Juhudi zako... Networking, good customer care...

Branding yourself, usifanye biashara kwa mazoea, kubali kubadilika, jifunze vitu vipya, don't copy but learn from the best...

Uvumilivu, wenye maneno mazuri na wenye matusi wote ni wateja...



Cc: mahondaw
 
Usimkatishe tamaa inawezekana hukumfundisha namna ya kujitegemea mke ndo msimamizi na msaidizi mkuu Jaribu kumuelimisha lakini muulize yeye Anapenda kusimamia nini mfungulie asimamie
Ndugu mkewangu ni mrokole ana imani kali sana anasali karibia siku zote za week, hata chanzo cha kufilisi duka ni sababu alikuwa anafungu muda mchache muda mwingi yuko kanisani
 
Hiyo ninusu hasala kwasababu dar kuku walio kufa wanasoko lao pia
 
Ndugu mkewangu ni mrokole ana imani kali sana anasali karibia siku zote za week, hata chanzo cha kufilisi duka ni sababu alikuwa anafungu muda mchache muda mwingi yuko kanisani
Labda alikuwa anakopesha sana
 
Usimkatishe tamaa inawezekana hukumfundisha namna ya kujitegemea mke ndo msimamizi na msaidizi mkuu Jaribu kumuelimisha lakini muulize yeye Anapenda kusimamia nini mfungulie asimamie
Ni kweli kabisa inawezekana mke hakua na uzoefu wala ujuzi katika biashara
 
H

Hongera sana mkuu kwa kutoa point ya mbolea. Maana sio siri zile comments zako za
"Ngoja waje, kukupa muongozo.........
Cc: mahondaw "
zinakeraga basi tu, ni vile tu kila mtu ana uhuru wa kupost anachotaka
Ahhahah mkuu umeamua utoe la moyoni
 
Usikate tamaa kaka we endelea kuaa mvumilivu sababu hakuna kitu rahisi,ndivyo tunavyopitia hivyo sio wewe peke ako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…