Tamu na chungu ulizopitia wakati unaanza biashara yako

Tamu na chungu ulizopitia wakati unaanza biashara yako

Mnamo tar21 mwez wa tisa mwaka huu nlifungua wakala (mpesa, tigo, airtel, na halotel) kariakoo nakumbuka cku hyo ckufanya muamala hata mmoja. Nliwaza nkamwambia Mungu n nini hiki sasa. Daah wateja wakawa kidogo wanakuja mwanzo wa mwez wa kumi ka kamishen kakaja hakafiki hata elfu hamsini daah kweli nkavunjika moyo sana.

Leo namshukuru Mungu kidogo wateja wanakuja japo nnaamini hadi mwakani nitasmama kwa kudra za mwenyezi Mungu. Sitaki kabisa kuajiriwa kwakuwa nishaajiriwa miaka miwili skuambulia chochote zaid ya kulipa kodi na kununua vitu vya ndani bas
 
Biashara ni ngumu kwavile imeambatana na changamoto ambazo wakati mwingine ni vigumu kuziepuka.

Mfano:

1. Uzoefu
2. Uaminifu
3. Uvumilivu
4. Usimamizi n.k

Kwanza nilianza na ufugaji wa nguruwe mmoja jike. Nikaenda nae vizuri tu. Kushika mimba, kabla hajajifungua akaanza kuumwa. Akawa anakosa nguvu za miguu, kuna jamaa mfugaji mzoefu, nilipomuelezea akasema kuna sindano inabidi achomwe. Tulipomchoma ile sindano, baada ya siku mbili mimba ikatoka. Nguruwe akaja akapona. Akashika mimba nyingine na kujifungua vitoto 5,mmoja akafa. Tukaenda nao pia fresh, ila wanakula kupita maelezo. Vilipoacha kunyonya, tukauza 3 kimoja kikabaki. Baada ya kuona uelekeo sio, mama mtu nikachinja na kuuza nyama buchani. Hela haikurudi. Nikapiga chini huo mradi.


Nikasogea kwenye kilimo. Tikiti na maharage. Hudumia sana shamba. Kwenye kuvuna, tikiti ilinipiga hasara moja matata sana. Nikapiga chini. Nikahamia kwenye kusafirisha maharage toka mkoani kuleta Dar. Nilichora mchoro vizuri tu. Nikanunua mzigo wa kutosha na kuuagiza uje mjini. Huku town alikuwepo jamaa yangu mmoja, mtu wa karibu sana (alikuwa mtu wa karibu sana, maana sio wa karibu tena). Jamaa akaupokea mzigo na kuusimamia kwa wale madalali wauzaji. Daily ananipa mrejesho wa maendeleo, nikawa nafurahishwa na bidii yake. Kumbe daily anaenda kuchukua hela alaf anaweka heshima mitaani na bar (mimi sina habari). Kuja kustuka, kashakula hela 75%, huku mimi ananiongopea madalali hawajampa bado. Biashara ikafa.


Nikageukia kwenye tangawizi. Nikalima vizuri na kila kitu kikawa chini ya usimamizi wangu mwenyewe. Kwenye mavuno mambo hayakwenda vizuri, ila walau niliona mwanga fulani hivi. Ikabidi niwekeze tena kwenye ili zao. Msimu wa pili kilichotokea ni afadhali ya msimu wa kwanza. Kama sijapalaraizi shambani, basi sidhani kama ntakuja kupalaraizi maishani mwangu. Kifupi shambani kitu pekee nilichoambulia ni kuitwa bossi na wale vibarua, zaidi ya hapo niliwafaidisha wao tu mimi sikupata kingine. Nikasema kilimo kwangu bye bye, siingii shambani tena.

Nikaamua kufungua duka la nafaka kwa reja reja. Ushindani niliokutana nao sio wa kawaida. Mara leo mtu aje kuulizia, then anakwambia ntarudi kuchukua kiasi kadhaa siku nyingine. Kumbe nae anafanya biashara hiyo hiyo so alikuja kunichunguza. Mara wamama watake mkopo. Kipindi mchele umekuwa hadimu mtaani, bei ya chini ilikuwaga 1500 kwa kilo, ila watu wanataka mchele wa 1300,tabu tupu. Baada ya miezi 4,nikaamua kupiga chini. Maana mzunguko ulikuwa mdogo saaana, nikawa namfaidisha mwenye fremu tu.


Kutokea hapo ndio nikaamua kuwekeza kwenye kitu kingine kabisa, tena nilianza na mtaji wa 1.5 milions. Nikaamua kusimamia mwenyewe mwanzo mwisho, hapo atleast ndio mwanga kidogo ukaonekana. Now nafikiria ni jinsi gani nitaitanua .

***** ****** ****** ******

Biashara zinahitaji kujitoa. Ukiweza kuweka hela yako sehemu, basi hakikisha unaweza kuweka na muda wako. Vinginevyo utaishia kufaidisha wengine.
Mwaka Jana nilizichanga sana kwa kusave mshahara wangu mwezi wa tatu mwaka jana nikaamua pesa yangu kuiongezea samani(kuiwekeza)nililima nyanya heka moja tukiwa na dogo baada ya kumaliza chuo cha ualimu,wazoefu wakatwambia "tutafute watu wengine 2 tuwe wa 4" Nilikataa kata kata tukijiamini kazi ya kuhudumia nyanya heka moja haitotushinda(tumekulia familia za wakulima wale wa kutumia nguvu).Tukapambana ikafika mda tukawa hatuongeleshani mpaka mda wa kula,nyanya zilikuja iva huku zingine hazijafungia fito.Mwanzoni tenga tukawa tunauza 40,000/= lakini kila kukicha bei ilizidi kushuka (mwezi wa sita mwishoni),mbaya zaidi shamba likavamiwa na vipepeo huku wateja hawapo(ukifika shambani shamba zima limekuwa jekundu) baada ya wiki mbili shamba zima wakaibuka funza wakatobowa nyanya zote.Nashukuru kila pesa niliyokuwa nauza niliandika mwisho wasiku nikapata 700,000/= baada ya kutumia 1,600,000/=.

Kumbuka mwaka huo huo nilikuwa nimelima heka 3 za pamba maana kila niamkapo asubuhi nilikuwa nakigongagonga kifua changu na kunuia "mke wangu mtarajiwa nikija kukuoa lazima ufikie kwenye nyumba yako tena nzur". Pamba ilianza kunishangaza kwenye mwezi wa NNE ikawa inarefuka tu Hata haizai kwa ufupi pamba haikuzaaa (WAZIRI WA MIFUGO NA KILIMO Mungu anakuona kwa ulichonifanyia 2017/2018).kwa ufupi mbegu tulioletewa ilikuwa mbovu.Mwisho wa siku nilipata 240,000/= baada ya kutumia 600,000/=.Huo mwaka ulikuwa mwaka wa shetani kwangu.Sahivi silimi tena huwa nawasubilia tu wakiivisha nanunua mazao naweka stock nashukuru now day pesa yangu haipotei.
 
Biashara ni ngumu kwavile imeambatana na changamoto ambazo wakati mwingine ni vigumu kuziepuka.

Mfano:

1. Uzoefu
2. Uaminifu
3. Uvumilivu
4. Usimamizi n.k

Kwanza nilianza na ufugaji wa nguruwe mmoja jike. Nikaenda nae vizuri tu. Kushika mimba, kabla hajajifungua akaanza kuumwa. Akawa anakosa nguvu za miguu, kuna jamaa mfugaji mzoefu, nilipomuelezea akasema kuna sindano inabidi achomwe. Tulipomchoma ile sindano, baada ya siku mbili mimba ikatoka. Nguruwe akaja akapona. Akashika mimba nyingine na kujifungua vitoto 5,mmoja akafa. Tukaenda nao pia fresh, ila wanakula kupita maelezo. Vilipoacha kunyonya, tukauza 3 kimoja kikabaki. Baada ya kuona uelekeo sio, mama mtu nikachinja na kuuza nyama buchani. Hela haikurudi. Nikapiga chini huo mradi.


Nikasogea kwenye kilimo. Tikiti na maharage. Hudumia sana shamba. Kwenye kuvuna, tikiti ilinipiga hasara moja matata sana. Nikapiga chini. Nikahamia kwenye kusafirisha maharage toka mkoani kuleta Dar. Nilichora mchoro vizuri tu. Nikanunua mzigo wa kutosha na kuuagiza uje mjini. Huku town alikuwepo jamaa yangu mmoja, mtu wa karibu sana (alikuwa mtu wa karibu sana, maana sio wa karibu tena). Jamaa akaupokea mzigo na kuusimamia kwa wale madalali wauzaji. Daily ananipa mrejesho wa maendeleo, nikawa nafurahishwa na bidii yake. Kumbe daily anaenda kuchukua hela alaf anaweka heshima mitaani na bar (mimi sina habari). Kuja kustuka, kashakula hela 75%, huku mimi ananiongopea madalali hawajampa bado. Biashara ikafa.


Nikageukia kwenye tangawizi. Nikalima vizuri na kila kitu kikawa chini ya usimamizi wangu mwenyewe. Kwenye mavuno mambo hayakwenda vizuri, ila walau niliona mwanga fulani hivi. Ikabidi niwekeze tena kwenye ili zao. Msimu wa pili kilichotokea ni afadhali ya msimu wa kwanza. Kama sijapalaraizi shambani, basi sidhani kama ntakuja kupalaraizi maishani mwangu. Kifupi shambani kitu pekee nilichoambulia ni kuitwa bossi na wale vibarua, zaidi ya hapo niliwafaidisha wao tu mimi sikupata kingine. Nikasema kilimo kwangu bye bye, siingii shambani tena.

Nikaamua kufungua duka la nafaka kwa reja reja. Ushindani niliokutana nao sio wa kawaida. Mara leo mtu aje kuulizia, then anakwambia ntarudi kuchukua kiasi kadhaa siku nyingine. Kumbe nae anafanya biashara hiyo hiyo so alikuja kunichunguza. Mara wamama watake mkopo. Kipindi mchele umekuwa hadimu mtaani, bei ya chini ilikuwaga 1500 kwa kilo, ila watu wanataka mchele wa 1300,tabu tupu. Baada ya miezi 4,nikaamua kupiga chini. Maana mzunguko ulikuwa mdogo saaana, nikawa namfaidisha mwenye fremu tu.


Kutokea hapo ndio nikaamua kuwekeza kwenye kitu kingine kabisa, tena nilianza na mtaji wa 1.5 milions. Nikaamua kusimamia mwenyewe mwanzo mwisho, hapo atleast ndio mwanga kidogo ukaonekana. Now nafikiria ni jinsi gani nitaitanua .

***** ****** ****** ******

Biashara zinahitaji kujitoa. Ukiweza kuweka hela yako sehemu, basi hakikisha unaweza kuweka na muda wako. Vinginevyo utaishia kufaidisha wengine.
Icho kitu kingne ulichoamua kukiwekeza tupe mwaga nacho nikipi
 
Kwenye kuanza biashara changamoto kubwa ni FURSA/WAZO LA BIASHARA.

Ukishaingia kwenye biashara na ukaperform vizuri unajikuta unazidi kuona FURSA NZURI NA KUBWA zaidi changamoto inakuwa MTAJI.

Ugumu wa biashara mwanzoni inachangiwa na UTAMBUZI WA FURSA, SOKO NA USIMAMIZI.

Nakumbuka biashara yangu ya kwanza nilichukua mzigo Iringa nikaupeleka maeneo ya Ukonga - Dar. Wateja wanagombania mlango wa fuso ufunguliwe wawahi magunia. Mzigo wote niliuza cash na kukawa na uhaba wa kama gunia 150 nikajilaumu ningekuwa na mtaji ningewaletea Scania Kichanja sio Fuso.
Mzigo gani huo mkuu[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Tuotee fursa
 
Mkuu Ilikuwa MKAA nikiwa Iringa naaangalia Fursa nikapata wazo la kusafirisha mkaa kwenda Dar.

Nikampigia simu jamaa yangu Dar akaniambia huku mkaa ni mali mvua zinanyesha hataree ukileta huo mkaa unapata hela nzuri.

Kwa kweli niliingia porini nikaandaa magunia 150, nikakata vibali vyote. Jamaa yangu ananisumbua huo mkaa mbona hauji nimeshapata wateja wa mastore. Nikapata moto zaidi wa kumalizia maandalizi.

Kwa kweli safari ilipoanza kwenda dar njiani nilikuwa nawaza kama jamaa atakuwa amenidanganya huu mzigo nitaupeleka wapi na ni mara yangu ya kwanza kukanyaga dar.

Gari iliingia dar saa 12 jioni jamaa akanipokea akawapigia simu wateja aliowaandaa akawaambia kesho asubuhi gari itashusha. Nimelala guest usiku usingizi hauji bei jamaa yangu aliyokuwa ananitajia nikipiga hesabu na faida ya milioni 2 na laki 6.

Asubuhi na mapema nikaenda eneo la tukio sikuamini kuona wateja wamesimama nyuma ya gari wanahimiza mlango ufunguliwe, wengine wanapanda kwenye Bomba wanachungulia mzigo ndani wanausifia.

Mlango ukafunguliwa wakaanza kugombania wanashusha wanapanga kimafungumafungu kwa kweli nikalipwa hela cash tena kwenye ile bei nikaongeza 5000 kwa gunia baada ya kuona wanagombania.

Ilikuwa biashara yangu ya kwanza baada ya kumaliza chuo ila nilishaachana nayo now nafanya biashara nyingine.
Why uliacha mkuu??? Samahani kwa maswali lakini
 
kitu pekee nilichoambulia ni kuitwa bossi na wale vibarua,

asee huwa naumia sana moyo unakuta unaitwa boss,mkuu,mheshmiwa lakn moyon unaujua ukweli kwamba hata chai hujanyww
Hatari sana mkuu.
 
Oky niliacha kutokana na changamoto zilizokuwa zinajitokeza kila kukicha bei ya gunia la mkaa shambani bei ilipanda kwa shilingi 6,000, bei ya usafiri kwa fuso ikapanda kutoka 1M mpaka 1.4M

Bei ya mkaa kupanda ilisababishwa na uongezeko la wanunuzi shambani tunagombania mkaa, bei ya usafiri ilipanda sambamba na bei ya mafuta.

Kuna wakati pia waziri husika akawa ana discourage hii biashara, sheria mpya mpya kodi mpya mpya

Na sokoni changamoto ikawa mkaa mwingi wateja wale wale bei ikaanza kushuka ushindani ukaongezeka, kuna wateja wangu wa jumla jumla wakaanza kukopeshwa na magari yanayozunguka mtaani kwenye mastore.

Nikabadili gia angani nikaingia biashara nyingine.
Hapo sawa mkuu...!! So kwa sasa hiyo biashara huwezi mshauri mtu aifanye ausio???
 
King999 umenichekesha sana tena sana.Binafsi kwa sasa baada ya kuteleza mara kadhaa katika biashara ikabidi nitulie na niwaze kwa kina nikaibuka na hitimisho biashara/kilimo ni taaluma kama taaluma zingine za ualimu/udaktari/uanasheria n.k, hivyo ili uifanye kwa uhakika na ufanikiwe kwa unachokifanya huna budi kuisomea hiyo taaluma hata kwa mfumo usiorasmi kwa kufanya utafiti ili ukusanye taarifa za kina zenye mbivu na mbichi kabla ya kuanza.
 
Biashara ni ngumu kwavile imeambatana na changamoto ambazo wakati mwingine ni vigumu kuziepuka.

Mfano:

1. Uzoefu
2. Uaminifu
3. Uvumilivu
4. Usimamizi n.k

Kwanza nilianza na ufugaji wa nguruwe mmoja jike. Nikaenda nae vizuri tu. Kushika mimba, kabla hajajifungua akaanza kuumwa. Akawa anakosa nguvu za miguu, kuna jamaa mfugaji mzoefu, nilipomuelezea akasema kuna sindano inabidi achomwe. Tulipomchoma ile sindano, baada ya siku mbili mimba ikatoka. Nguruwe akaja akapona. Akashika mimba nyingine na kujifungua vitoto 5,mmoja akafa. Tukaenda nao pia fresh, ila wanakula kupita maelezo. Vilipoacha kunyonya, tukauza 3 kimoja kikabaki. Baada ya kuona uelekeo sio, mama mtu nikachinja na kuuza nyama buchani. Hela haikurudi. Nikapiga chini huo mradi.


Nikasogea kwenye kilimo. Tikiti na maharage. Hudumia sana shamba. Kwenye kuvuna, tikiti ilinipiga hasara moja matata sana. Nikapiga chini. Nikahamia kwenye kusafirisha maharage toka mkoani kuleta Dar. Nilichora mchoro vizuri tu. Nikanunua mzigo wa kutosha na kuuagiza uje mjini. Huku town alikuwepo jamaa yangu mmoja, mtu wa karibu sana (alikuwa mtu wa karibu sana, maana sio wa karibu tena). Jamaa akaupokea mzigo na kuusimamia kwa wale madalali wauzaji. Daily ananipa mrejesho wa maendeleo, nikawa nafurahishwa na bidii yake. Kumbe daily anaenda kuchukua hela alaf anaweka heshima mitaani na bar (mimi sina habari). Kuja kustuka, kashakula hela 75%, huku mimi ananiongopea madalali hawajampa bado. Biashara ikafa.


Nikageukia kwenye tangawizi. Nikalima vizuri na kila kitu kikawa chini ya usimamizi wangu mwenyewe. Kwenye mavuno mambo hayakwenda vizuri, ila walau niliona mwanga fulani hivi. Ikabidi niwekeze tena kwenye ili zao. Msimu wa pili kilichotokea ni afadhali ya msimu wa kwanza. Kama sijapalaraizi shambani, basi sidhani kama ntakuja kupalaraizi maishani mwangu. Kifupi shambani kitu pekee nilichoambulia ni kuitwa bossi na wale vibarua, zaidi ya hapo niliwafaidisha wao tu mimi sikupata kingine. Nikasema kilimo kwangu bye bye, siingii shambani tena.

Nikaamua kufungua duka la nafaka kwa reja reja. Ushindani niliokutana nao sio wa kawaida. Mara leo mtu aje kuulizia, then anakwambia ntarudi kuchukua kiasi kadhaa siku nyingine. Kumbe nae anafanya biashara hiyo hiyo so alikuja kunichunguza. Mara wamama watake mkopo. Kipindi mchele umekuwa hadimu mtaani, bei ya chini ilikuwaga 1500 kwa kilo, ila watu wanataka mchele wa 1300,tabu tupu. Baada ya miezi 4,nikaamua kupiga chini. Maana mzunguko ulikuwa mdogo saaana, nikawa namfaidisha mwenye fremu tu.


Kutokea hapo ndio nikaamua kuwekeza kwenye kitu kingine kabisa, tena nilianza na mtaji wa 1.5 milions. Nikaamua kusimamia mwenyewe mwanzo mwisho, hapo atleast ndio mwanga kidogo ukaonekana. Now nafikiria ni jinsi gani nitaitanua .

***** ****** ****** ******

Biashara zinahitaji kujitoa. Ukiweza kuweka hela yako sehemu, basi hakikisha unaweza kuweka na muda wako. Vinginevyo utaishia kufaidisha wengine.
Daah we jamaa mwepesi sana kupiga chini vitu
 
mwanangu ww kama mm yaan huwa znaniboha knyama mpaka nauliza huyu jamaa kama hana cha kucomment si apite kimya ???yaan kila post yy anaandika "ngoja waje" huwa ananikata maini kinyama mpakq huwa naclose app dadeq yaan nakerekaga asee yaan naboreka ase e kama huna cha kucomment uwe unapita kimya kimya mzee for sure watu huwa tunaboreka
ahahaa , nilidhani peke yangu tu
 
huenda wife sio jambaz ila matumizi yake yalizid margin/profit mana mwanamke akiona mavitu yamejaa dukan anahan kama kuna faida lundooo kumbe faida ni mia mya mbili tu
yani aliposema mkewe ni mlokole, bila shaka alikuwa anapeleka mauzo yote kanisani na sadaka mbalimbali alikuwa anatoa, mavuno, fungu la kumi, malimbuko, wajane, yatima, ujenzi wa kanisa, ahadi nk.... makanisa yetu ya siku hizi haya ni mufilisi
 
Mnamo tar21 mwez wa tisa mwaka huu nlifungua wakala (mpesa, tigo, airtel, na halotel) kariakoo nakumbuka cku hyo ckufanya muamala hata mmoja. Nliwaza nkamwambia Mungu n nini hiki sasa. Daah wateja wakawa kidogo wanakuja mwanzo wa mwez wa kumi ka kamishen kakaja hakafiki hata elfu hamsini daah kweli nkavunjika moyo sana.

Leo namshukuru Mungu kidogo wateja wanakuja japo nnaamini hadi mwakani nitasmama kwa kudra za mwenyezi Mungu. Sitaki kabisa kuajiriwa kwakuwa nishaajiriwa miaka miwili skuambulia chochote zaid ya kulipa kodi na kununua vitu vya ndani bas
safi sana mkuu, nami nafanya biashara hizo pia, na nilitamani siku moja nami nipate goli town k/,koo
 
Mnamo tar21 mwez wa tisa mwaka huu nlifungua wakala (mpesa, tigo, airtel, na halotel) kariakoo nakumbuka cku hyo ckufanya muamala hata mmoja. Nliwaza nkamwambia Mungu n nini hiki sasa. Daah wateja wakawa kidogo wanakuja mwanzo wa mwez wa kumi ka kamishen kakaja hakafiki hata elfu hamsini daah kweli nkavunjika moyo sana.

Leo namshukuru Mungu kidogo wateja wanakuja japo nnaamini hadi mwakani nitasmama kwa kudra za mwenyezi Mungu. Sitaki kabisa kuajiriwa kwakuwa nishaajiriwa miaka miwili skuambulia chochote zaid ya kulipa kodi na kununua vitu vya ndani bas
nami kuajiriwa nimekataa kabisa baada ya kupitia msoto wa ujob less, nikaona nijiajiri.
 
Mkuu Ilikuwa MKAA nikiwa Iringa naaangalia Fursa nikapata wazo la kusafirisha mkaa kwenda Dar.

Nikampigia simu jamaa yangu Dar akaniambia huku mkaa ni mali mvua zinanyesha hataree ukileta huo mkaa unapata hela nzuri.

Kwa kweli niliingia porini nikaandaa magunia 150, nikakata vibali vyote. Jamaa yangu ananisumbua huo mkaa mbona hauji nimeshapata wateja wa mastore. Nikapata moto zaidi wa kumalizia maandalizi.

Kwa kweli safari ilipoanza kwenda dar njiani nilikuwa nawaza kama jamaa atakuwa amenidanganya huu mzigo nitaupeleka wapi na ni mara yangu ya kwanza kukanyaga dar.

Gari iliingia dar saa 12 jioni jamaa akanipokea akawapigia simu wateja aliowaandaa akawaambia kesho asubuhi gari itashusha. Nimelala guest usiku usingizi hauji bei jamaa yangu aliyokuwa ananitajia nikipiga hesabu na faida ya milioni 2 na laki 6.

Asubuhi na mapema nikaenda eneo la tukio sikuamini kuona wateja wamesimama nyuma ya gari wanahimiza mlango ufunguliwe, wengine wanapanda kwenye Bomba wanachungulia mzigo ndani wanausifia.

Mlango ukafunguliwa wakaanza kugombania wanashusha wanapanga kimafungumafungu kwa kweli nikalipwa hela cash tena kwenye ile bei nikaongeza 5000 kwa gunia baada ya kuona wanagombania.

Ilikuwa biashara yangu ya kwanza baada ya kumaliza chuo ila nilishaachana nayo now nafanya biashara nyingine.

Safi sana chief ulijua kufanya kitu kimoja kikubwa cha kujivunia (close deal) afu sasa biashara ilivyo ya ajabu unaweza leta awamu ya pili isiwe kama ulivyotegemea
 
Mkuu hao mbwa wa kisasa ni kweli wanafugwa au msemo tu?
Mkubwa salama

huwa napenda kuyasemea mambo ambayo nayaishi
fanya utafiti mtaani kwako kwa watu wanaofanya hizi mambo.

labda nikupe hints kidogo

ukiwa na dume la pure breed ya gs (giant) kupandisha majike mengine siyo chini 1m
puppies wa pure breed ya gs wanauzwa 1.5 kwa mmoja, kashuka sana bas 1.2

chotara yaani cross puppies wanauzwa 500k umeshuka sana basi 450k kwa mmoja.

kwanini nihangaike na kuku wa kisasa ambao ni stress tu.
 
Daah we jamaa mwepesi sana kupiga chini vitu
Na ndo alifeli hapo pale kwenye nguruwe angekomaa napo maana alishakuwa mzoefu maana changamoto huja ili Upate Uzoefu

japo na Mimi ninachangamoto ila sikati tamaa
 
n sahh mkuu biashara ukiivaa kichwa kichwa unaweza kuta inakupiga za uso
yaan knowledge is the basic of any bussness
King999 umenichekesha sana tena sana.Binafsi kwa sasa baada ya kuteleza mara kadhaa katika biashara ikabidi nitulie na niwaze kwa kina nikaibuka na hitimisho biashara/kilimo ni taaluma kama taaluma zingine za ualimu/udaktari/uanasheria n.k, hivyo ili uifanye kwa uhakika na ufanikiwe kwa unachokifanya huna budi kuisomea hiyo taaluma hata kwa mfumo usiorasmi kwa kufanya utafiti ili ukusanye taarifa za kina zenye mbivu na mbichi kabla ya kuanza.
 
yani aliposema mkewe ni mlokole, bila shaka alikuwa anapeleka mauzo yote kanisani na sadaka mbalimbali alikuwa anatoa, mavuno, fungu la kumi, malimbuko, wajane, yatima, ujenzi wa kanisa, ahadi nk.... makanisa yetu ya siku hizi haya ni mufilisi
na wanawake wa sku hz wanamsikiliza pastor kuliko mme wake
 
Wakati niko chuo nilipata boom kiasi cha lakhi 4. Nikaamua nikizalishe. Nikaanza biashara ya mbao. Kwa vile sikuwa na muda wa kusimamia, ilibidi tu niwaamini marafiki. Weee... kosa kubwa. Biashara ilifilisika. Nikajifunza kuwa usimamizi wa biashara ni muhimu tu kama ilivyo mtaji. Kuanzia hapo kama sina muda wa kusimamia, sifanyi biashara.
Hizo mbao gani mkuu ulikuwa unachukulia wapi
 
Kwahiyo hauna biashara/mradi wowote pembeni mbali na ajira yako kwa mantiki hiyo.
Wakati niko chuo nilipata boom kiasi cha lakhi 4. Nikaamua nikizalishe. Nikaanza biashara ya mbao. Kwa vile sikuwa na muda wa kusimamia, ilibidi tu niwaamini marafiki. Weee... kosa kubwa. Biashara ilifilisika. Nikajifunza kuwa usimamizi wa biashara ni muhimu tu kama ilivyo mtaji. Kuanzia hapo kama sina muda wa kusimamia, sifanyi biashara.
 
Back
Top Bottom