TANESCO: Bwawa la Mwalimu Nyerere (JNHPP) kuhusishwa na athari za mafuriko ya Kibiti na Rufiji ni kupotosha Umma

TANESCO: Bwawa la Mwalimu Nyerere (JNHPP) kuhusishwa na athari za mafuriko ya Kibiti na Rufiji ni kupotosha Umma


UFAFANUZI KUHUSU ATHARI ZA MAFURIKO YA KIBITI NA RUFIJI KUHUSISHWA NA UJENZI WA BWAWA LA JULIUS NYERERE (JNHPP)

Alhamisi, 11 Aprili 2024
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linapenda kutoa ufafanuzi kwa Umma kuhusu athari za mafuriko yanayoendelea katika maeneo ya Wilaya za Rufiji na Kibiti ambayo yanahusishwa na ujenzi wa Bwawa la Kufua Umeme la Julius Nyerere (JNHPP).

Tunapenda kuujulisha umma kwamba uwepo wa Mradi wa Bwawa la kufua umeme la Julius Nyerere umesaidia kwa sehemu kubwa kupunguza athari ya mafuriko katika Wilaya za Rufiji na Kibiti ukilinganisha na miaka ya nyuma kabla mradi haujajengwa.

Imetolewa Na;
KURUGENZI YA MAWASILIANO NA UHUSIANO KWA UMMA
TANESCO-MAKAO MAKUU
DODOMA
Na sisi hapa JF tunapenda kuufahamisha umma kwamba, uongozi wa CCM unajaribu kutumia kila njia kuonyesha hili tatizo halijasababishwa na Bwawa la Nyerere, pamoja na kuwapa TANESCO maagizo waseme hivi.

Tunaukumbusha umma kwamba wanasiasa sasa ndio wamekuwa mainjinia wa kutoa ufafanuzi, na mainjinia wako kimya. Wenye akili wote wanajua kwamba tatizo ni kwamba Bwawa la Nyerere lilijazwa maji kupita kiasi na bila mpangilio, na walipogundua hili wakaamua kufungulia maji mengi kulinusuru bwawa na kuepuka mafuriko makubwa hata zaidi ambayo yangeleta maafa makubwa sana ikiwa Bwawa lingepata madhara. Hii ingekuwa habari ya ulimwengu na aibu kubwa kwa Tanzania, kashfa mbaya kwa uongozi wa Tanzania. Lakini hawataki kukiri hili na kusema ukweli. Mbaya zaidi, wanawalaumu wananchi ambao wamewasababishia haya matatizo.

Tunajua kuwa TANESCO inabidi wakubali maelekezo toka juu kuhusu kutoa maelezo juu ya mafuriko ya Rufiji kwa sababu tu ya kulinda ugali wao na ule wa chama tawala. Tunawaelewa, lakini wanapaswa pia kuelewa wanashiriki dhambi ya wanasiasa. Tunatumaini dhamiri zao zitawishitaki.

Tungenda Tanesco wajibu ndio au hapana kwa maswali haya mawili;

  1. Je, ni kweli kwamba maji yalipofunguliwa Bwawa la Nyerere yalifunguliwa katika flow rate ambayo ilijulikana ingepeleka maji mengi downstream ambayo yangesababisha mafuriko?
  2. Je, ni kweli kwamba katika kipindi cha mwaka mzima cha masika na kiangazi, ikiwa maji yangeruhusiwa kupita kwa kiwango cha wastani unaokubalika, mafuriko yasingetokea kwa sababu ya dry and wet season flow rates balancing effect lakini hilo halikufanyika kwa kutaka Bwawa la Nyerere lijae haraka?
TANESCO tayari hatuwaheshimu, sasa msitake kutupa sababu nyingine ya kutowaheshimu.

Ushauri wetu kwenu ni kwamba, badala ya kutumia ubongo wa wanasiasa ku-manage maji ya bwawa la Nyerere, tumieni computer programe kama inavyotakiwa - flow in rate-retention-flow out rate. Mngefanya hivi, angalau mngewapa tahadhari wananchi miezi minne hata mitano kabla ya mafuriko, kama kweli tatizo lilikuwa ni natural weather issue. Lakini mkaamua kuwa watu wenye macho mnaokubali kuongozwa na vipofu.
 

UFAFANUZI KUHUSU ATHARI ZA MAFURIKO YA KIBITI NA RUFIJI KUHUSISHWA NA UJENZI WA BWAWA LA JULIUS NYERERE (JNHPP)

Alhamisi, 11 Aprili 2024
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linapenda kutoa ufafanuzi kwa Umma kuhusu athari za mafuriko yanayoendelea katika maeneo ya Wilaya za Rufiji na Kibiti ambayo yanahusishwa na ujenzi wa Bwawa la Kufua Umeme la Julius Nyerere (JNHPP).

Tunapenda kuujulisha umma kwamba uwepo wa Mradi wa Bwawa la kufua umeme la Julius Nyerere umesaidia kwa sehemu kubwa kupunguza athari ya mafuriko katika Wilaya za Rufiji na Kibiti ukilinganisha na miaka ya nyuma kabla mradi haujajengwa.

Historia ya kitakwimu inaonesha kuwa maeneo ya Rufiji na Kibiti yamekuwa yakikumbwa na mafuriko kwa miaka mingi ya nyuma kwa kiwango kikubwa kuliko hali ilivyo hivi sasa. Mwezi Mei, 1974 kiwango cha juu cha mafuriko katika mto Rufiji kilifikia mita za ujazo 13,200 kwa sekunde.

Mwaka 1988 kiwango cha mafuriko kilifikia mita za ujazo 8,383.9, mwaka 2016 kiwango cha mafuriko kilifikia mita za ujazo 8,974,7, mwaka 2020 kiwango cha mafuriko kilifikia mita za ujazo 7158.5 na tarehe 15 Februari 2024 kabla ya Bwawa la Julius Nyerere kujaa maji, kiwango cha mafuriko ya maji kilichokuwa kinaingia kwenye Bwawa kilifikia mita za ujazo 8,444 kwa sekunde.

Hata hivyo mafuriko hayo hayakufikia maeneo ya Kibiti na Rufiji kwa sababu Bwawa halikuwa limejaa, kiufupi ni kwamba Bwawa liliendelea kuhimili maji ya mafuriko tokea mwezi Disemba 2022 lilipoanza kujazwa maji mpaka mwishoni mwa mwezi Februari 2024 lilipojaa.

Baada ya Bwawa kujaa, maji ya mafuriko ya Mto Rufiji yaliendelea kupita mtoni kama ilivyo asili yake na hivyo kusababisha mafuriko katika maeneo ya Kibiti na Rufiji jambo ambalo ni la kawaida kwa kila msimu wa mvua kwa mto huu.

Hivyo, kama Mradi wa JNHPP usingejengwa basi maji haya yangefika moja kwa moja kwenye maeneo ya Rufiji na Kibiti na hivyo kusababisha athari kubwa zaidi ya mafuriko na kwa vipindi virefu kuliko tulivyoshuhudia sasa.

Lakini kwa kuwa maji hayo ya mafuriko yalikuwa yakimezwa kwanza na Bwawa la Mradi na kutunzwa kwa muda mrefu, jambo hilo lilisaidia mafuriko kutotokea au kuonekana kwa mapema katika maeneo hayo ya Kibiti na Rufiji.

Ikumbukwe kwamba moja wapo ya sababu ya kuanzishwa Mradi wa Bwawa la kuzalisha Umeme la Julius Nyerere (JNHPP) katika maeneo ya Rufiji ni kwa sababu ya uwepo wa maji ya mafuriko katika Bonde la Mto Rufiji hali iliyopelekea Serikali kuamua kuyatumia mafuriko hayo ya maji kwa ajili ya kuzalisha umeme.

Kama eneo hilo la Bonde la Mto Rufiji lisingeonekana kuwa na maji mengi ya mafuriko kila mwaka basi hata Serikali isingeamua kuwekeza mradi wa Bwawa katika eneo hilo.

Tunapenda Umma ufahamu kwamba mwaka huu (2024) kumekuwepo na mvua kubwa za El-nino ambazo zimepelekea kuwepo kwa mafuriko makubwa katika maeneo mengi ya nchi yetu ikiwemo maeneo yanayopeleka mtiririko wa maji ya mvua kwenye Bonde la Mto Rufiji.
Hivyo, kiwango kikubwa cha mafuriko katika maeneo hayo ya Kibiti na Rufiji kimesababishwa na mvua kubwa za El-nino zinazoendelea kunyesha.

Sehemu nyingine kumesababishwa na madhara ya mabadiliko ya tabia nchi ambapo kutokana na kupanda kwa vina vya bahari, kumekuwepo na upungufu wa spidi ya maji ya mito kuingia baharini hasa wakati maji ya bahari yanapokuwa yamejaa yaani "High Tide".

Hivyo, kwa maelezo yaliyopo kwenye taarifa hii, Shirika la Umeme Tanzania linakanusha taarifa zozote za upotoshaji zinazohusisha Bwawa la Julius Nyerere na mafuriko ya Kibiti na Rufiji na linakemea upotoshaji unaofanywa na baadhi ya Watu wasio na nia njema kubeza juhudi za Serikali katika kuimarisha hali ya upatikanaji wa umeme nchini kwa ujenzi wa Bwawa la Julius Nyerere.

Shirika linaendelea kuwasihi Wananchi kuwa watulivu na kuendelea kufuatilia taarifa sahihi zinazotolewa na mamlaka husika ili kuendelea kujiweka katika hali ya usalama na kuondoa taharuki isiyo na ulazima.

Imetolewa Na;
KURUGENZI YA MAWASILIANO NA UHUSIANO KWA UMMA
TANESCO-MAKAO MAKUU
DODOMA
Rufiji mafuriko yapo toka enzi....nakumbuka wimbo wa mbaraka mwinshehe
 
UNESCO na WWF waliwashaonya juu ya hili na madhara mengne meng lakini kwakuwa NEMC na TANESCO wote ni sauti moja ya CCM mkajibariki wenyewe under the aura of a go-ahead given by the dubious Environmental Impact Assesment.

Sasa saiz tena mnataka kukwepa lawama badala ya kuleta solution mnatumia nguvu nying kushift blames..!
Shida ya wabongo tukisikia mashirika ya Umoja wa Mataifa (UNESCO na WWF n.k ) tunahisi sijui wao ni miungu. Hayo mashirika yanaongozwa na watu kama wewe tu hayo majina yasifanye muwe mnanyenyekea kila wanachosema na kuhisi wao ni Mungu.

Kwa taarifa yao tu hayo mashirika huwa yana skendo nyingi na taarifa zao zimekuwa zikigubikwa na utata rejea ile report ya DOING BUSINESS ambayo watanzania tulikuwa tunafanya reference kwa kila kitu lakini baadaye ikaja kugundulika waandaaji walikuwa wanapokea rushwa na kuzipendelea baadhi ya nchi.

Kwa hiyo tusipende sana kuamini wanacho kisema wao bila kujiridhisha huo ni utumwa wa fikira.
Asante
 

UFAFANUZI KUHUSU ATHARI ZA MAFURIKO YA KIBITI NA RUFIJI KUHUSISHWA NA UJENZI WA BWAWA LA JULIUS NYERERE (JNHPP)

Alhamisi, 11 Aprili 2024
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linapenda kutoa ufafanuzi kwa Umma kuhusu athari za mafuriko yanayoendelea katika maeneo ya Wilaya za Rufiji na Kibiti ambayo yanahusishwa na ujenzi wa Bwawa la Kufua Umeme la Julius Nyerere (JNHPP).

Tunapenda kuujulisha umma kwamba uwepo wa Mradi wa Bwawa la kufua umeme la Julius Nyerere umesaidia kwa sehemu kubwa kupunguza athari ya mafuriko katika Wilaya za Rufiji na Kibiti ukilinganisha na miaka ya nyuma kabla mradi haujajengwa.

Historia ya kitakwimu inaonesha kuwa maeneo ya Rufiji na Kibiti yamekuwa yakikumbwa na mafuriko kwa miaka mingi ya nyuma kwa kiwango kikubwa kuliko hali ilivyo hivi sasa. Mwezi Mei, 1974 kiwango cha juu cha mafuriko katika mto Rufiji kilifikia mita za ujazo 13,200 kwa sekunde.

Mwaka 1988 kiwango cha mafuriko kilifikia mita za ujazo 8,383.9, mwaka 2016 kiwango cha mafuriko kilifikia mita za ujazo 8,974,7, mwaka 2020 kiwango cha mafuriko kilifikia mita za ujazo 7158.5 na tarehe 15 Februari 2024 kabla ya Bwawa la Julius Nyerere kujaa maji, kiwango cha mafuriko ya maji kilichokuwa kinaingia kwenye Bwawa kilifikia mita za ujazo 8,444 kwa sekunde.

Hata hivyo mafuriko hayo hayakufikia maeneo ya Kibiti na Rufiji kwa sababu Bwawa halikuwa limejaa, kiufupi ni kwamba Bwawa liliendelea kuhimili maji ya mafuriko tokea mwezi Disemba 2022 lilipoanza kujazwa maji mpaka mwishoni mwa mwezi Februari 2024 lilipojaa.

Baada ya Bwawa kujaa, maji ya mafuriko ya Mto Rufiji yaliendelea kupita mtoni kama ilivyo asili yake na hivyo kusababisha mafuriko katika maeneo ya Kibiti na Rufiji jambo ambalo ni la kawaida kwa kila msimu wa mvua kwa mto huu.

Hivyo, kama Mradi wa JNHPP usingejengwa basi maji haya yangefika moja kwa moja kwenye maeneo ya Rufiji na Kibiti na hivyo kusababisha athari kubwa zaidi ya mafuriko na kwa vipindi virefu kuliko tulivyoshuhudia sasa.

Lakini kwa kuwa maji hayo ya mafuriko yalikuwa yakimezwa kwanza na Bwawa la Mradi na kutunzwa kwa muda mrefu, jambo hilo lilisaidia mafuriko kutotokea au kuonekana kwa mapema katika maeneo hayo ya Kibiti na Rufiji.

Ikumbukwe kwamba moja wapo ya sababu ya kuanzishwa Mradi wa Bwawa la kuzalisha Umeme la Julius Nyerere (JNHPP) katika maeneo ya Rufiji ni kwa sababu ya uwepo wa maji ya mafuriko katika Bonde la Mto Rufiji hali iliyopelekea Serikali kuamua kuyatumia mafuriko hayo ya maji kwa ajili ya kuzalisha umeme.

Kama eneo hilo la Bonde la Mto Rufiji lisingeonekana kuwa na maji mengi ya mafuriko kila mwaka basi hata Serikali isingeamua kuwekeza mradi wa Bwawa katika eneo hilo.

Tunapenda Umma ufahamu kwamba mwaka huu (2024) kumekuwepo na mvua kubwa za El-nino ambazo zimepelekea kuwepo kwa mafuriko makubwa katika maeneo mengi ya nchi yetu ikiwemo maeneo yanayopeleka mtiririko wa maji ya mvua kwenye Bonde la Mto Rufiji.
Hivyo, kiwango kikubwa cha mafuriko katika maeneo hayo ya Kibiti na Rufiji kimesababishwa na mvua kubwa za El-nino zinazoendelea kunyesha.

Sehemu nyingine kumesababishwa na madhara ya mabadiliko ya tabia nchi ambapo kutokana na kupanda kwa vina vya bahari, kumekuwepo na upungufu wa spidi ya maji ya mito kuingia baharini hasa wakati maji ya bahari yanapokuwa yamejaa yaani "High Tide".

Hivyo, kwa maelezo yaliyopo kwenye taarifa hii, Shirika la Umeme Tanzania linakanusha taarifa zozote za upotoshaji zinazohusisha Bwawa la Julius Nyerere na mafuriko ya Kibiti na Rufiji na linakemea upotoshaji unaofanywa na baadhi ya Watu wasio na nia njema kubeza juhudi za Serikali katika kuimarisha hali ya upatikanaji wa umeme nchini kwa ujenzi wa Bwawa la Julius Nyerere.

Shirika linaendelea kuwasihi Wananchi kuwa watulivu na kuendelea kufuatilia taarifa sahihi zinazotolewa na mamlaka husika ili kuendelea kujiweka katika hali ya usalama na kuondoa taharuki isiyo na ulazima.

Imetolewa Na;
KURUGENZI YA MAWASILIANO NA UHUSIANO KWA UMMA
TANESCO-MAKAO MAKUU
DODOMA
Walivyosema wanafungulia maji kutoka kwenye bwawa, ili maanisha nini? Mafuriko ni ya maji yaliyopunguzwa kutoka kwenye bwawa, wanabisha nini?
 
Hilo lipo wazi, Bwawa limemeza maji kwa kadri ya uwezo wake, yaliyozidi lazima yapite..
 

UFAFANUZI KUHUSU ATHARI ZA MAFURIKO YA KIBITI NA RUFIJI KUHUSISHWA NA UJENZI WA BWAWA LA JULIUS NYERERE (JNHPP)

Alhamisi, 11 Aprili 2024
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linapenda kutoa ufafanuzi kwa Umma kuhusu athari za mafuriko yanayoendelea katika maeneo ya Wilaya za Rufiji na Kibiti ambayo yanahusishwa na ujenzi wa Bwawa la Kufua Umeme la Julius Nyerere (JNHPP).

Tunapenda kuujulisha umma kwamba uwepo wa Mradi wa Bwawa la kufua umeme la Julius Nyerere umesaidia kwa sehemu kubwa kupunguza athari ya mafuriko katika Wilaya za Rufiji na Kibiti ukilinganisha na miaka ya nyuma kabla mradi haujajengwa.

Historia ya kitakwimu inaonesha kuwa maeneo ya Rufiji na Kibiti yamekuwa yakikumbwa na mafuriko kwa miaka mingi ya nyuma kwa kiwango kikubwa kuliko hali ilivyo hivi sasa. Mwezi Mei, 1974 kiwango cha juu cha mafuriko katika mto Rufiji kilifikia mita za ujazo 13,200 kwa sekunde.

Mwaka 1988 kiwango cha mafuriko kilifikia mita za ujazo 8,383.9, mwaka 2016 kiwango cha mafuriko kilifikia mita za ujazo 8,974,7, mwaka 2020 kiwango cha mafuriko kilifikia mita za ujazo 7158.5 na tarehe 15 Februari 2024 kabla ya Bwawa la Julius Nyerere kujaa maji, kiwango cha mafuriko ya maji kilichokuwa kinaingia kwenye Bwawa kilifikia mita za ujazo 8,444 kwa sekunde.

Hata hivyo mafuriko hayo hayakufikia maeneo ya Kibiti na Rufiji kwa sababu Bwawa halikuwa limejaa, kiufupi ni kwamba Bwawa liliendelea kuhimili maji ya mafuriko tokea mwezi Disemba 2022 lilipoanza kujazwa maji mpaka mwishoni mwa mwezi Februari 2024 lilipojaa.

Baada ya Bwawa kujaa, maji ya mafuriko ya Mto Rufiji yaliendelea kupita mtoni kama ilivyo asili yake na hivyo kusababisha mafuriko katika maeneo ya Kibiti na Rufiji jambo ambalo ni la kawaida kwa kila msimu wa mvua kwa mto huu.

Hivyo, kama Mradi wa JNHPP usingejengwa basi maji haya yangefika moja kwa moja kwenye maeneo ya Rufiji na Kibiti na hivyo kusababisha athari kubwa zaidi ya mafuriko na kwa vipindi virefu kuliko tulivyoshuhudia sasa.

Lakini kwa kuwa maji hayo ya mafuriko yalikuwa yakimezwa kwanza na Bwawa la Mradi na kutunzwa kwa muda mrefu, jambo hilo lilisaidia mafuriko kutotokea au kuonekana kwa mapema katika maeneo hayo ya Kibiti na Rufiji.

Ikumbukwe kwamba moja wapo ya sababu ya kuanzishwa Mradi wa Bwawa la kuzalisha Umeme la Julius Nyerere (JNHPP) katika maeneo ya Rufiji ni kwa sababu ya uwepo wa maji ya mafuriko katika Bonde la Mto Rufiji hali iliyopelekea Serikali kuamua kuyatumia mafuriko hayo ya maji kwa ajili ya kuzalisha umeme.

Kama eneo hilo la Bonde la Mto Rufiji lisingeonekana kuwa na maji mengi ya mafuriko kila mwaka basi hata Serikali isingeamua kuwekeza mradi wa Bwawa katika eneo hilo.

Tunapenda Umma ufahamu kwamba mwaka huu (2024) kumekuwepo na mvua kubwa za El-nino ambazo zimepelekea kuwepo kwa mafuriko makubwa katika maeneo mengi ya nchi yetu ikiwemo maeneo yanayopeleka mtiririko wa maji ya mvua kwenye Bonde la Mto Rufiji.
Hivyo, kiwango kikubwa cha mafuriko katika maeneo hayo ya Kibiti na Rufiji kimesababishwa na mvua kubwa za El-nino zinazoendelea kunyesha.

Sehemu nyingine kumesababishwa na madhara ya mabadiliko ya tabia nchi ambapo kutokana na kupanda kwa vina vya bahari, kumekuwepo na upungufu wa spidi ya maji ya mito kuingia baharini hasa wakati maji ya bahari yanapokuwa yamejaa yaani "High Tide".

Hivyo, kwa maelezo yaliyopo kwenye taarifa hii, Shirika la Umeme Tanzania linakanusha taarifa zozote za upotoshaji zinazohusisha Bwawa la Julius Nyerere na mafuriko ya Kibiti na Rufiji na linakemea upotoshaji unaofanywa na baadhi ya Watu wasio na nia njema kubeza juhudi za Serikali katika kuimarisha hali ya upatikanaji wa umeme nchini kwa ujenzi wa Bwawa la Julius Nyerere.

Shirika linaendelea kuwasihi Wananchi kuwa watulivu na kuendelea kufuatilia taarifa sahihi zinazotolewa na mamlaka husika ili kuendelea kujiweka katika hali ya usalama na kuondoa taharuki isiyo na ulazima.

Imetolewa Na;
KURUGENZI YA MAWASILIANO NA UHUSIANO KWA UMMA
TANESCO-MAKAO MAKUU
DODOMA
T14 Armata
 
Back
Top Bottom