Tanesco Dodoma bado hawataki tulipe 27,000 kuunganisha umeme

Tanesco Dodoma bado hawataki tulipe 27,000 kuunganisha umeme

MGOGOHALISI

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2011
Posts
3,294
Reaction score
4,920
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza.

Licha ya waziri wa nishati kuelekeza kuwa wananchi waunganishiwe umeme kwa 27,000 tanesco Dodoma bado wamekaidi agizo hili. Wameamua kuwaunganisha wateja wenye nguzo karibu na nyumba zao huku wengine wakiambiwa walipie gharama za kuwasogezea nguzo karibu. Mbaya zaidi hata nguzo walizotawanya mitaani hawataki kuzisimika kitendo kitakachofanya kila mtu kuwa karibu na nguzo, wameziacha chini zinaliwa na mchwa.

Wananchi wa Dodoma wanamuomba waziri wa nishati atembelee mitaa kama Makulu, Chidachi karibu shule ya St Marys, Iringa road na kwingineko. Nguzo zimebwagwa chini ni miezi mitatu sasa na hakuna kinachoendelea.

Yote hii ni kutaka kupata sababu ya kuwatoza wahitaji wa umeme zaidi ya kiwango alichoagiza waziri.
 
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza. Licha ya waziri wa nishati kuelekeza kuwa wananchi waunganishiwe umeme kwa 27,000 tanesco Dodoma bado wamekaidi agizo hili. Wameamua kuwaunganisha wateja wenye nguzo karibu na nyumba zao huku wengine wakiambiwa walipie gharama za kuwasogezea nguzo karibu. Mbaya zaidi hata nguzo walizotawanya mitaani hawataki kuzisimika kitendo kitakachofanya kila mtu kuwa karibu na nguzo, wameziacha chini zinaliwa na mchwa.
Wananchi wa Dodoma wanamuomba waziri wa nishati atembelee mitaa kama Makulu, Chidachi karibu shule ya St Marys, Iringa road na kwingineko. Nguzo zimebwagwa chini ni miezi mitatu sasa na hakuna kinachoendelea. Yote hii ni kutaka kupata sababu ya kuwatoza wahitaji wa umeme zaidi ya kiwango alichoagiza waziri.
REA au ?! Sijajua kama unazungumzia maeneo ya pembezoni au mjini, nadhani umefika wakati sasa umeme wa 27000 uwe ni kwa watu wote bila kujali mjini au vijijini.
 
Hii Wizara ina changamoto nyingi Sana.

Kazi za kitaalam ambazo zilipaswa zitolewe na Ewura tunaona zinatolewa tamko na Waziri.

Aina tofauti na matamko mengine kama ya Wizara ya Afya wakati wa Corona.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hamna la ukweli TANESCO waongo sana....hili shirika ni bora likabinafsishwe kama vip basi waruhusu makampuni binafsi....TANESCO HOVYO MNOOO
 
Back
Top Bottom