Tanesco kodi ya jengo imepanda?

Tanesco kodi ya jengo imepanda?

Endelea kushabikia simba na yanga
Yaani hata uniambie nitaje wachezaji wawili kutoka Simba na Yanga sijui hata mmoja, mimi na mpira mbalimbali. Mara ya mwisho kwenda uwanja wa Taifa ni siku uwanja mpya ulipozinduliwa baada ya kujengwa na wachina. Ikatokea vurugu kubwa sana watu wakaharibu viti na vifaa mbalimbali vya uwanja mpya. Nikajiapiza kwamba sitokaa tena kuhangaika na huu ujinga ujinga, na kweli mpaka leo sina habari kabisa.
 
Mkuu unajua chama kahamia yanga? Je Joshua mutale????
 
Je mwezi uliopita ulifanya manunuzi ya umeme? Ulilipa shiling ngapi kwenye kodi ya jengo?
Tarehe 28.06.2024 Kijana wangu nilimtuma kununua umeme na details zikawa as follows:
  • VAT (18%) 4426.22
  • EWURA (1%) 244.90
  • REA (3%) 737.71
  • DEBT COLLECTED 0.0
 
Imepanda baada ya 1500 ,sasa ni 2k.hivyo wamekukata 6k sababu huenda hukununua umeme kwa miezi kadhaa.Wanatudhulumu sana hawa majitu
Nanunua umeme kila Mwezi mkuu, hata kama niko safarini au shambani. Halafu nyumba ninayokaa ni ya serikali za mitaa, nimepanga.
 
Mwezi uliopita ulilipa kodi ya jengo? Au mara ya mwisho kununua umeme ni mwezi gani?

Kodi ya jengo imepanda kutoka 1500 mwezi uliopita hadi 2000 mwezi huu ( mwaka mpya wa bajeti ya serikali ni mwezi julai).
Ngoja na wengine wachangie mada tujue shida ipo wapi..
Nimelipa na Debt collected ilisoma 0.0 which i think ni kwa sababu nalipa Luku kila mwezi bila kukosa. Sasa nilitegemea wakate basi hiyo 2000 sasa naona wamelamba 6000???
 
Mkuu unajua chama kahamia yanga? Je Joshua mutale????
Chama ni nani huyo mkuu? Ameenda kuchukua nafasi ya Haji Manara?? Au umechanganya na issue ya Msigwa wa CHADEMA kutimkia chama la wana??
 
Wanajamvi leo nimenunua umeme wa 25,000/= na makato yalikuwa kama ifuatavyo:
MAKATO

1. VAT 2,803

2. EWURA (1%) 155.74

3. REA (3%) 467.21

4. DEBT COLLECTED 6000

TOTAL 9,426

BALANCE FROM MY 25,000 = 15,574

Sasa hii 6000/= ni ile kodi ya majengo imepanda?
Juzi kati kuna kale kasystem ambao walisema wanboresha mitambo yao nkajua tuu tayar tunaelekea kupewa HEAVY LOG ON THE HEAD
 
Chama ni nani huyo mkuu? Ameenda kuchukua nafasi ya Haji Manara?? Au umechanganya na issue ya Msigwa wa CHADEMA kutimkia chama la wana??
Koz tunapenda jadili mipira wkt maisha yanatait balaa
 
Back
Top Bottom