Nchi hii ishawashinda, mwaka wa 60+ toka uhuru mpaka leo, umeme tabu, maji changamoto, afya tabu, elimu ya hovyo, barabara changamoto, ajira ndio tatizo linakuja kwa kasi, gharama za maisha zinapanda kila uchwao, pesa yetu inashuka thamani.
Hawana cha maana wanachofanya zaidi ya porojo, mara deni la taifa stahamilivu, mara uchumi wa kati, tumepata gesi umaskini bai bai, sijui madini gani, wao wanajiwahi mapema, gesi, bandari, madini, mbuga za wanyama, hazina manufaa na mtanzania zinawafaidisha wao tu.
Ikishindikana arudi tu mkoloni mzungu tujue moja.