TANESCO: Mvua zikiendelea kunyesha katika mabwawa, changamoto ya upungufu wa umeme itapungua

bagamoyo

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
24,941
Reaction score
28,869

Changamoto za Upungufu wa umeme Kupatiwa Ufumbuzi

Mkurugenzi mkuu wa TANESCO Bw. Maharage Chande akizungumza na waandishi wa habari leo December 2, 2022 kuhusu hatua za muda mfupi na muda mrefu kumaliza upungufu wa umeme .

Mkurugenzi ameongeza kuwa mvua zinazonyesha muda huu nchini bado hazijaweza kutiririka katika mito ya maji inayoingia katika mabwawa ya umeme.

Hivyo juhudi zimeelekezwa mitambo ya gesi na kukarabati mitambo huku mvua zinazoendelea kunyesha hatimaye kujaza mito inayotiririsha maji katika mabwawa ya umeme.

---
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) ameelezea mikakati yao wanayoendelea nayo pamoja na changamoto wanazokutana nazo katika harakati zao za kurejesha huduma ya umeme.

Amesema “Tayari tumeshakamilisha matengenezo ya mtambo mmoja wa LM6000 katika kituo cha Ubungo namba III na umeshaanza kuingiza megawati 35 za umeme katika Gridi ya Taifa kuanzia tarehe 25 Novemba 2022 kama tulivyoeleza hapo awali.

“Tayari tumeshakamilisha matengenezo ya mtambo mmoja wa kituo cha Kidatu na umeshaanza kuzalisha megawati 50 za umeme katika Gridi ya Taifa kuanzia tarehe 30 Novemba 2022.

“Matengenezo ya mtambo mmoja katika kituo cha Kinyerezi namba II yameshakamilika na tayari umeshaanza kuzalisha megawati 215 za umeme kuanzia tarehe 24 Novemba 2022.”

Kuhusu juhudi zao za muda mfupi, amesema majaribio ya mitambo miwili katika kituo cha upanuzi cha Kinyerezi namba I yanaendelea, na kwa sasa mitambo hiyo inaingiza jumla ya megawati 65 za umeme katika Gridi ya Taifa. Pia wanategemea hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Disemba 2022, mitambo hii itakuwa inazalisha jumla ya megawati 90 kama tulivyoeleza hapo awali;

Ameongeza kuwa bado wanaendelea na kazi za matengenezo ya mitambo miwili ya Ubungo namba III ambapo baada ya kukamilika mwishoni mwa Disemba 2022, itazalisha jumla ya megawati 40 za umeme.


JITIHADA ZA MUDA WA KATI ZINAZOENDELEA KUFANYIKA
Ameseme “Tunategemea mitambo mingine miwili kuanza kufanya kazi katika kituo cha upanuzi cha Kinyerezi namba I kuanzia mwezi Februari 2023 ili kuingiza megawati 90 za umeme katika Gridi ya Taifa.

“Iwapo mvua zitaendelea kunyesha katika mabwawa yote ya kufua umeme na matengenezo yaliyobakia kukamilika kama yalivyopangwa, basi tunategemea hali ya umeme itaendelea kuimarika na hivyo tunatarajia kiasi cha upungufu wa umeme kwa siku kuendelea kupungua kutoka wastani wa kati ya megawati 300 hadi 350 wiki iliyopita hadi kufikia megawati 215 za umeme wiki hii.”
 
JPM akiongea bungeni akasema kuna watu wanapunguza kina cha maji ya Mtera ili mtaani pawe na mgao mkali wa umeme ili wapigaji wapate sababu ya kutajirika.

Mpaka anakufa hakuna ushahidi wowote wa maana uliowekwa wazi wa tuhuma za wizi huo wa TANESCO!, Ni shirika kubwa la umeme lenye kuingiziwa siasa na wanasiasa wanaotafuta popularity za mitandaoni.

Tukiwa wabunifu kidogo tu tunaweza kuwa na vyanzo mbalimbali vya umeme na maisha yakawa yanaendelea pasipo haja ya kuwa na migao ya umeme inayorudisha nyuma juhudi mbalimbali za kujikwamua kiuchumi.
 

Mkurugenzi mkuu wa TANESCO Ndugu Maharage Chande amesema tatizo la Ukame ambalo limepelekea upungufu wa umeme bado lipo, japokuwa ya mvua kuanza kunyesha baadhi ya maeneo nchini.

Amesema kuwa bado mvua hazijanyesha maeneo muhimu kwa uzalishaji wa umeme kwa kupitia maji na kina na cha maji kwenye mabwawa mbali mbali bado kinaendelea kushuka.

Hivyo wamejikita zaidi katika kuongeza uzalishaji wa umeme kupitia gesi. Amesema hayo akizungumza na vyombo vya habari leo tarehe 02/12/2022.
 
Kwahio makato ya umeme kila kona yapo palepale hadi kieleweke? Mwendo wa kukata tu na kugawana mafungu.
 
Huwa najiuliza kwanini hayo marekebisho makubwa ya mitambo anayodai ya lazima, wanayafanya kwa pamoja, na kwa wakati mmoja, hivyo kusababisha kuleta upungufu mkubwa wa umeme?

Kwanini wasingefanya hayo marekebisho kwa vituo vichache kwa wakati, ili vituo vingine viendelee kuzalisha umeme na kuepusha haya makali ya mgao wa umeme uliopo kwa sababu ya kufanya kwa vituo vyote kwa wakati mmoja?

Hivi kwa akili ndogo kama hii, amekosekana kabisa mtu huko serikalini wa kuwashauri hawa jamaa waache huu ujinga wao wanaotufanyia? kwa namna hii watu wakiamini huu mgao ni wakutengeneza ili wauze majenereta watakataa vipi?

Bad enough, huyo Maharage anatumia neno "endapo" marekebisho yatakwisha kwa wakati, hii maana yake hawa jamaa wanatuliwaza kwa ujinga wa makusudi wanaotufanyia, neno "endapo" linaonesha hawana uhakika na kazi zao, hawa ni matapeli na waongo, hawafai kabisa.

Huu mgao uliopo sasa Tanzania Bara sitashangaa kama utaenda kwa muda mrefu ujao, ikiwezekana mpaka mwakani, kwasababu hawa kina Maharage wanachofanya ni kutuliwaza tu kisaikolojia na hizi press zao, lakini kimsingi hawako serious, wanatuchezea tu kama watoto wadogo.
 
Wafanye wanavyofanya.. Kikubwa wasiuze Tanesco tuu maana tumewashtukia kigambo wala njama.. Wakiongozwa na yule jamaa mvaa suti alafu kichwani akili imevaa magunia
 
Wehu kweli, sisi hatuhitaji hizo bla blah zenu unatubinulia mdomo mtoto wa kiume vipi wewe bana, sisi tunataka umeme kwakuwa tunalipia na uwezo wa kulipia tunao.
 
🙄🙄🙄🙄
 
Maharage juu ya Kipara!!
Wazanzibara kazi tunayo!
 
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) ameelezea mikakati yao wanayoendelea nayo pamoja na changamoto wanazokutana nazo katika harakati zao za kurejesha huduma ya umeme.

Amesema “Tayari tumeshakamilisha matengenezo ya mtambo mmoja wa LM6000 katika kituo cha Ubungo namba III na umeshaanza kuingiza megawati 35 za umeme katika Gridi ya Taifa kuanzia tarehe 25 Novemba 2022 kama tulivyoeleza hapo awali.

“Tayari tumeshakamilisha matengenezo ya mtambo mmoja wa kituo cha Kidatu na umeshaanza kuzalisha megawati 50 za umeme katika Gridi ya Taifa kuanzia tarehe 30 Novemba 2022.

“Matengenezo ya mtambo mmoja katika kituo cha Kinyerezi namba II yameshakamilika na tayari umeshaanza kuzalisha megawati 215 za umeme kuanzia tarehe 24 Novemba 2022.”

Kuhusu juhudi zao za muda mfupi, amesema majaribio ya mitambo miwili katika kituo cha upanuzi cha Kinyerezi namba I yanaendelea, na kwa sasa mitambo hiyo inaingiza jumla ya megawati 65 za umeme katika Gridi ya Taifa. Pia wanategemea hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Disemba 2022, mitambo hii itakuwa inazalisha jumla ya megawati 90 kama tulivyoeleza hapo awali;

Ameongeza kuwa bado wanaendelea na kazi za matengenezo ya mitambo miwili ya Ubungo namba III ambapo baada ya kukamilika mwishoni mwa Disemba 2022, itazalisha jumla ya megawati 40 za umeme.

JITIHADA ZA MUDA WA KATI ZINAZOENDELEA KUFANYIKA
Ameseme “Tunategemea mitambo mingine miwili kuanza kufanya kazi katika kituo cha upanuzi cha Kinyerezi namba I kuanzia mwezi Februari 2023 ili kuingiza megawati 90 za umeme katika Gridi ya Taifa.

“Iwapo mvua zitaendelea kunyesha katika mabwawa yote ya kufua umeme na matengenezo yaliyobakia kukamilika kama yalivyopangwa, basi tunategemea hali ya umeme itaendelea kuimarika na hivyo tunatarajia kiasi cha upungufu wa umeme kwa siku kuendelea kupungua kutoka wastani wa kati ya megawati 300 hadi 350 wiki iliyopita hadi kufikia megawati 215 za umeme wiki hii.”
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…