TANESCO na Msigwa mtuambie kwanini umeme wa Tanzania kwenda Kaskazini una transmission losses kubwa kuliko wa Ethiopia kuja kwetu, mbali zaidi!

Watakovo kueleza watatumi mfano wa choo kikiwa juu mlimani si rahisi kujaa haraka
Kimsingi,huu mkataba wa kununua umemem unaweza ukawa na lojiki, japo sidhani. Jambo la msingi ni Tanzania na Samia kutoingia kichwa kichwa bila kuwa makini kuona long term implications ni nini,kama wanavyofanya siku zote. Wauweke wazi huo mkataba tuuchambue. Mkataba wa umeme Samia na Mbarawa ndio wanapitisha, unategemea nini hapo, kupigwa tu!
 
Yah. Nenda sima post ya Tibaijuka ... Ameeleza sawa na hivyo usemavyo.
Tibaijuka wamemweleza eti ni kwa ajili ya energy security. Sasa lini tena tumebadilisha objective ya kununua umemem toka Ethiopia kwa nia ya kukwepa transmission losses na kwenda kwenye supply security?

Katika vitu hivi, kila kimoja kina approach yake. Huwezi kubadili lengo moja kuwa jingine kwa mradi uleule. Ukisema ni supply security unaweza kukuta umeme wa Ethiopia ni wa mwisho kwenye list - hasa Egypt anapotishia kuwapiga kwa sababu ya hilo bwawa!
 
Kingine walitakiwa watuambie miundo mbingu ya umeme toka huko Ethiopia kuja kwetu ni wa voltage kiasi gani ? Labda uwe kuanzia 765kV au 1000kV kwenda mbele. Ambao kwa Sasa rate voltage hizo sisi hatuna haja nazo.

Lakini ukienda Arusha tu huko tayari miundo mbinu ya 400kV ipo.

Sasa sijajua wenyewe wanatumia akili gani, wengine ukiwauliza wanadai ni Grid Stability, yaani wanastabilize Grid ?
 
Hawa jamaa maelezo yao hayajitoshelezi, walitakiwa watoe maelezo ya ndani zaidi. Hili suala linahitaji mjadala wa wazi baina ya wataalamu.

Kingine, kwani Grid yetu inayofika Kaskazi ni voltage kiasi gani na hiyo inayotoka Ethiopia ni voltage kiasi ?

Sasa chanzo kimoja, ndio watu Wana hoji, vipi kwa mikoa mingine ?
 
Point nzuri. Kama wanasema transmission infrastructure ipo tayari, ni lini tathmini imefanyika kuangalia uwezo wa hiyo grid toka Ethiopia? Je wameangalia reliability yake? Wameangalia scalability yake kwa kuwa haikujengwa with transmission to Tanzania in mind? Wameangalia technological compatibility (HVDC au HVAC) na kama imetumia aluminum au copper conductors kwa hiyo ina losses za chini ukilinganisha na za kwetu? Wameangalia nini itakuwa impact kwenye grid resistance and inductive reactance watakapounganisha na Tanzania? Je itaunganishwa na na grid iliyopo ya upande wa Tanzania, na kama ndio, wameangalia connectivity? Na isipounganishwa na grid ya Tanzania, siku umeme wa Ethiopia ukifeli then hiyo mikoa ya kaskazini itakuwaje?

Ndio maana nikasema, Samia na Msigwa wasichukulie haya mambo kisiasa katika kutafuta kura za kaskazini na kuwaburuza TANESCO
 

Hapa wanatakiwa hii lugha yao ili iweleweke vizuri watumie data za wazi na nina Imani hawawezi kufanya hivyo sababu namba hazidanganyi.
 
Fact
 
Kwa wale wanaojenga na wamefikia hatua ya wiring wanafahamu bei za vifaa vya umeme kama ukiamua kuelekezwa na fundi vitu vya kununua bila kumhusisha fundi kwenye manunuzi.
Niliishawahi kununua vifaa kwa maelekezo ya fundi, nikagundua kuwa wholesalers wana bei mbili, bei ya mchekea ni vifaa duni wakati kuna bei mbaya ndio vinapaswa kuwa bora .... Lakini sio mara zote.
Tanesco watakuwa wamefanya manunuzi ya vifaa duni vinavyopoteza umeme na kuongeza gharama ambayo wanaitafsiri kuwa hasara kwa makusudi ili waje na utetezi wa program ya East Africa Power Pool.... Huu ni wizi wa kitaasisi unaohusisha nchi za nje. Hizi ni hujuma za wazi kabisa tena zinafanywa bila kuwa na soni.
 
Hata mimi nimeshindwa kushangaa nime pigwa na butwaa. Kutoka Grand renaissance dam ilipo sehemu inaitwa Guba mpaka Arusha Tanzania ni 2,292 Km. Inaweza ikapungua kidogo au ikaongezeka kidogo. Hivyo transmission loss inategemea kuwa kubwa. Mwalimu wangu wa umeme nikiwa Tanga Technical school form one alinifundisha kuwa ' The longer the wire, the bigger the resistance'. Kutoka Mwalimu Nyerere Dam mpaka Arusha city ni kama 800 Km ya weza kuwa zaidi kidogo au pungufu. Kwa mujibu wa Mwalimu wangu wa Electrical Engineering ni wazi kuwa umeme toka Ethiopia unapotea mwingi toka kwao mpaka Arusha /Moshi kuliko wa Nyerere Dam mpaka Arusha / Moshi. Labda wenzetu wanatumia 'Hardened copper'. Na Tanesco wanatumia Bronze wala siyo normal Copper.
 
Tanesco wanamzunguka mama ili wamharibie duuh !
 
Na wakumbuke walisema tanzania itakuwa na umeme wakutosha na mwingine watauza nchi nyingine jirani,hizi kauli bhana,hakika njia ya muongo huwa ni fupi.
 
Halafu huo umeme wa Wahabeshi tunaulipia kwa dollar kama petroli
 
kwamba tunanunua umeme kutoka Ethiopia kupitia Kenya
Halafu sisi Tz tunawauzia Kenya
kwmba umeme wa Ethiopia unazalishwa kwa gharama nafuu na no mwingi kuliko sisi ao megawatts 6000 sisi megawatts 2000
πŸ€”πŸ€”πŸ€”πŸ€”
Yaani mimi sijaelewa kabisa
 
Hawa watu katika kukuelewesha huwa wanakuchanganya ili uelewe! Watasema hatujasaini mkataba wa bandari ya Bagamoyo, ila tumewapa waarabu bandari, kwa hiyo msihofu hakuna mkataba mbovu umesainiwa!
 
Uzuri wa mainjinia wa Tz linapokuja swala la upigaj huwezi warudisha nyuma πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Kutoka kutaka kuuza mpaka kununua umeme Ethiopia lol!

Kama tunashindwa kuutoa umeme bwawa la mwalimu nyerere kwenda kigoma na Arusha ndio tutaweza kuutoa bwawa la mwalimu nyerere kwenda DRC au tulitaka kuuza online?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…