KERO TANESCO nalia na nyie! Mmehalalisha wizi kupitia makato ya kodi ya pango

KERO TANESCO nalia na nyie! Mmehalalisha wizi kupitia makato ya kodi ya pango

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

MeVSMe

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2024
Posts
270
Reaction score
425
Jamani, Tanesco, nalia na nyie! Mtatutoa roho nyie. Yaani mtu unanunua umeme wa shilingi elfu 20, unapewa umeme wa shilingi elfu 10? Hivi nyie mna matatizo gani?

Iko hivi, juzi umeme kwangu uliisha usiku, nikasema ninunue umeme wa elfu 5, ukagoma. Nikajua labda pesa haitoshi, nikiongeza elfu 20, nikanunua wa elfu 5, bado ukagoma.

Ninawapigia simu, hampokei. Are you guys serious? Yaani mtu unalala usiku kucha bila umeme, bila sababu ya msingi. Nimeamka asubuhi, bado nikajaribu kununua, mkagoma.

Nawapigia, mnaniambia nadaiwa miezi mitatu kodi ya pango. What is kodi ya pango? Kila nilipokuwa nikinunua umeme, mnakata pesa halafu mnakuja kuniambia nadaiwa elfu 6 ya kodi ya pango?

Haya, tuseme nadaiwa. Kwanini mimi ninalala usiku kucha bila umeme? Na uzembe ni wa kwenu? Nani aliwaambia mmalize miezi mitatu mfululizo bila kukata hiyo kodi? Na hiyo kodi ya pango mnayoisema ni ipi wakati kila nikinunua umeme mnakata?

Basi haya, mkakataa kunipa umeme mkasema mpaka ninunue umeme kuanzia elfu 6 na miatano ili mkate pesa yenu. Nimenunua umeme wa elfu 20, mmenipa umeme wa elfu 11, kwanini? Hivi nyie? Oooh, mpaka nashindwa kuandika kwa sababu ya hasira nilizonazo.

Jamani wana JamiiForums, naomba muangalie hizo picha hapo, mnisaidie na nyie, mnakutana nayo haya au?Baada ya kunikata hiyo pesa, nawapigia, wananiambia ni makato, like seriously???? Yaani nimekatwa elfu 9 yote halafu Serikali inajivunia kukata makato yote haya huku sisi nyoyo zinawaka moto.

Hizo screenshots

Screenshot_20241007-094127.png
Screenshot_20241007-094232.png
 
Au ilipita miezi mitatu hujanunua umeme? Pole sana lakini, hela ya uchaguzi inatafutwa.
 
Au ilipita miezi mitatu hujanunua umeme? Pole sana lakini, hela ya uchaguzi inatafutwa.
Oooh hapana, yaani mara ya mwisho nilinunua umeme mwezi wa 9 tarehe 5umeme wa mwezi, Sasa kwanini mi wanitese Kwa kutafuta tu hela yao ya kafara,
 
Kuna mita nilinunua umeme kati ya mwezi wa 3 au 4 nimekuja kununua tena wiki iliyopita wa elf 10 wamenipa unit 1 na point 🤣🤣🤣kweli chura yupo kazini
Uuuuuuh mamaaaa, pole sana Mkuu😂😂😂😂, chura hasikii
 
Jamani, Tanesco, nalia na nyie! Mtatutoa roho nyie. Yaani mtu unanunua umeme wa shilingi elfu 20, unapewa umeme wa shilingi elfu 10? Hivi nyie mna matatizo gani?

Iko hivi, juzi umeme kwangu uliisha usiku, nikasema ninunue umeme wa elfu 5, ukagoma. Nikajua labda pesa haitoshi, nikiongeza elfu 20, nikanunua wa elfu 5, bado ukagoma.

Ninawapigia simu, hampokei. Are you guys serious? Yaani mtu unalala usiku kucha bila umeme, bila sababu ya msingi. Nimeamka asubuhi, bado nikajaribu kununua, mkagoma.

Nawapigia, mnaniambia nadaiwa miezi mitatu kodi ya pango. What is kodi ya pango? Kila nilipokuwa nikinunua umeme, mnakata pesa halafu mnakuja kuniambia nadaiwa elfu 6 ya kodi ya pango?

Haya, tuseme nadaiwa. Kwanini mimi ninalala usiku kucha bila umeme? Na uzembe ni wa kwenu? Nani aliwaambia mmalize miezi mitatu mfululizo bila kukata hiyo kodi? Na hiyo kodi ya pango mnayoisema ni ipi wakati kila nikinunua umeme mnakata?

Basi haya, mkakataa kunipa umeme mkasema mpaka ninunue umeme kuanzia elfu 6 na miatano ili mkate pesa yenu. Nimenunua umeme wa elfu 20, mmenipa umeme wa elfu 11, kwanini? Hivi nyie? Oooh, mpaka nashindwa kuandika kwa sababu ya hasira nilizonazo.

Jamani wana JamiiForums, naomba muangalie hizo picha hapo, mnisaidie na nyie, mnakutana nayo haya au?Baada ya kunikata hiyo pesa, nawapigia, wananiambia ni makato, like seriously???? Yaani nimekatwa elfu 9 yote halafu Serikali inajivunia kukata makato yote haya huku sisi nyoyo zinawaka moto.

Hizo screenshots

View attachment 3117487View attachment 3117489
Sote ni vile vile ila hapo pa kudaiwa miezi mitatu kama ulikuwa wanunua kila mwezi hapo ndipo sipaelewi. huko kwingine sijui rea sijui nini sote maumivu ni yale yale
 
du hatari kila mwezi nanunua umeme wananiambia nadaiwa 18000
 
Sote ni vile vile ila hapo pa kudaiwa miezi mitatu kama ulikuwa wanunua kila mwezi hapo ndipo sipaelewi. huko kwingine sijui rea sijui nini sote maumivu ni yale yale
Ndio, nilikuwa nanunua Kila mwezi na Kwa mwezi ningeweza kununua kama mara 5 hivi, yaani kuanzia mwezi wa 9 tu ndo niliweka umeme wa mwezi, huku kwingine nilikuwa nanunua wa alfu5 tano Kila wiki Tena na makato walikuwa wanakata. Na niliwauliza maswali lakini kama unavojua watajitetea vyovyote vile kwenye simu, uongo na ukweli
 
Waweke option ya mtu kulipa pango la mwaka mzima in advance ili tusisumbuane
Umeona!!! Na niliwauliza mnaniambiaje nadaiwa miezi mitatu? Wakati Kwa mwezi mi nanunua umeme hata mara 5 na mnakata??? Eti oooh mfumo, yakaenda yakarudi kwanini wasikate mipesa yao huko wanasubiri kutugomea😞😞😞
 
Huwa najiuliza uhusiano wa Kodi ya jengo vs kununua umeme.

Basi tu ila SI sawa....
 
Kwa nini usiende mahakamani ndugu, huu wizi wa TANESCO kuna namna ya kuukomesha. Na ni pamoja na kutuambia hiyo ela wanaipeleka wapi wakati huo huo VAT, TRA wameshakata chao. Yaani tunapigwa double taxation halafu tunaendelea kumchekea huyu CHURA KAFIRI.
 
Sina hamu na tanesco, niliwahi wekewa deni laki 6 hadi leo hii sijawahi jua lilitoka wapi. Nilienda ofisin kwao maelezo ni mengi lkn sikuwaelewa bado deni limetoka wapi.
 
Sina hamu na tanesco, niliwahi wekewa deni laki 6 hadi leo hii sijawahi jua lilitoka wapi. Nilienda ofisin kwao maelezo ni mengi lkn sikuwaelewa bado deni limetoka wapi.
*****, laki 6??????? Hawa Ng'ombe ni wezi
 
Kama uko karibu na ofisi zao waendee wakueleze shida. Nakumbuka ilitokea shida mwezi wa sita/saba. Baadae wakajitetea na Hela hazikurudishwa. Kiendacho kwa mganga!
 
Back
Top Bottom