TANESCO wamepata wapi umeme wa kuiuzia Zanzibar Tshs 30 kwa unit?

The Phylosopher

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2015
Posts
1,968
Reaction score
2,957
Nimemsikia waziri kutoka Zanzibar akisema kwamba Kuna kero moja kubwa imeondoshwa kwa tanesco wamekubali kuiuzia Zanzibar umeme Kwa shs 30 Kwa unit.
Huu umeme wa bei hiyo umetoka wapi?
 
Amesema wanauziwa Tsh 130 na si 30
 
Nimemsikia waziri kutoka Zanzibar akisema kwamba Kuna kero moja kubwa imeondoshwa kwa tanesco wamekubali kuiuzia Zanzibar umeme Kwa shs 30 Kwa unit.
Huu umeme wa bei hiyo umetoka wapi?
Kwani umeme wa Uganda tunaununua kwa bei gani?
 
Issue sio kwanini wao wauziwe bei rafiki bali kwanini sisi tusiuziwe bei rafiki ?

Umeme ni huduma na impact yake ipo katika sekta zote..., kutoa kwa bei za kukomoana ni kujiibia mfuko wa suruali ili uweke mfuko wa shati
 
Bulyanhulu Mine na kiwanda cha Wazo Tegeta wanauziwa kwa bei hiyo hiyo
 
Nimemsikia waziri kutoka Zanzibar akisema kwamba Kuna kero moja kubwa imeondoshwa kwa tanesco wamekubali kuiuzia Zanzibar umeme Kwa shs 30 Kwa unit.
Huu umeme wa bei hiyo umetoka wapi?
Ila Wazanzibari ni wanyonyaji!! Sisi wamiliki wa mitambo, tunauziwa unit 1 kwa zaidi ya shilingi 300! Halafu wao wanauziwa kwa shilingi 30 tu!!

Mimi naona huu Muungano ufikie tu tamati. Maana inachosha kuendelea kuwalea hawa viumbe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…