Ukiendekeza SIASA utapotea mkuu.
Kwani waliokosa umeme au wanaokaa huko ni Chadema tu,kama mmekosa basi mmekosa wote.
Hivi chama gani unafikiria kikiingia madarakani kitakuwa ni miungu watu kwamba hakuna linaloweza kutokea.
Mambo Mengine ni God`s case,unalalamika utafikiria mpemba?
Ukiendekeza kusema kila kitu kibaya ni sababu ya CCM basi utakuwa unapoteza muda wako bure na nguvu yako kimaisha.
We fanyakazi na ujitume nenda shule ujiendeleze uone kama unaonewa,hakuna chama kitakachokuletea chakula mpaka ujitume mwenyewe.
Na wanaolalamika sana ndio wanaokuwa nyuma kila siku,unaweza kujikuta unagombana na mkeo,mara unasema ahhh CCM hao.
We Angalia mfano Mama Lishe wa Dar,wao Siasa kwao ni siku ya kupiga kura tu,wakimaliza wanaingia mzigoni na hakuna habari za kuonewa wala nini.Na ndio maana Mamalishe wengi Dar wanamiliki viwanja na wengine nyumba wakati wafanyakazi wa serikali wakiishia kupanga miaka tele.
Life is how you make it,acha kulalamika issue kama hiyo eti umeme kwetu haupo kisa CCM alaa