Bepari2020
JF-Expert Member
- Nov 7, 2020
- 2,072
- 2,453
Wataalamu waandike basi hiyo ERP itumike kwenye mashirika ya umma na pia tuuze nje ya nchi tuingize madola. Au wewe andika yako utajirike.we jamaa pumba sana, kwani hujui kuna mifumo mingine ipo kwenye windows? kwa hiyo serikali iandike OS kisha ifuatie na utility softwares n.k issue ni kuwa huu mfumo ungeweza kutengenezwa na watanzania kama ambavyo mingine imetengenezwa na kutika mpaka sasa bila shida, hiyo kununua nje ni ishara ya upigaji,mboba watu hawajalalamika ndege kununuliwa nje??? sababu tunajua sio uwezo wetu, ila kwa hili hapana, wataalamu wa ndani ni muhimu wapewe fursa ili waweke ujuzi wao
Mikataba ya namna hii, hapana kwa kweli, dah , wangewekeza kwenye miundombinu kwanzaWatanzania naona tulisahau kabisa ajenda ya ufisadi wakati wa Magufuli, mpaka sasa kuna ufisadi umefanyika fasta fasta bila ya watu hata kushtuka.
Mkataba uliosainiwa baina ya Serikali ya Tanzania (kupitia TANESCO) na kampuni ya Tech Mahindra ya India wenye thamani ya dola milioni 30 ni wa kukodisha software ya Enterprise Resources Planning (ERP) - ambayo wahindi hawa wenyewe wanaiita Corporate Management System (CMS), kama inavyosomeka kwenye bango pichani chini.
Software ya aina hii huwa inaunganisha vitengo vyote vya taasisi katika software moja kwa ajili ya urahisi wa kuendesha taasisi. Hivyo basi kwa lugha nyingine ni kwamba Wahindi hawa watafunguliwa milango ya kuingia kila mahali ndani ya TANESCO, na hivyo kuwa na siri zote za mfumo wetu wa umeme.
Jambo kama hili ni hatari sana kwa usalama wa taifa. Hakuna njia rahisi ya kuiangusha nchi bila ya kufyatua hata kombora moja kama kuangusha mfumo wa nchi wa umeme.
Software kama hizi serikali inatakiwa iwawezeshe wataalam wa ndani kupitia Mamlaka ya Serikali Mtandao kutengeneza, kama vile mfumo wa malipo serikalini ulivyotengenezwa na wataalam wetu wa ndani kwa kuwezeshwa na serikali.
Zabuni ya kukodisha software hii ilianzaga kwenye dakika za lala salama za utawala wa Kikwete. Hivyo basi kitendo cha zabuni hii kukaa benchi kwa miaka mitano ya Magufuli kinaonesha kuwa hakuwa amekubaliana nayo. Baada ya Magufuli kufa naona wadau wa zabuni hii wameiendeleza na kuimwagia wino fasta, kama wanavyotaka kufanya kuhusu bandari ya Bagamoyo.
Halafu muda si mrefu wanaleta nyingine na kuita an updated version, hiyo iliyo nunuliwa imepitwa na wkt.Wahindi Tena Bora wangepewa hiyo tenda Korea kusini nahisi ndio nchi pekee duniani yenye kuaminika
Kwwnz sio kununua ni kukodisha wahts a shame jamaniKwahiyo shida kubwa ya Serikali yetu haipo kwenye kutokuwa na pesa ya kutosha, hapana, shida ipo kwenye matumizi ya hovyo bila kujali wala kushirikisha wananchi
Mungu atusaidie
Usisahau kupitia na hapa😁👇Mama yangu!!
jiwe ule ujuaji wake wakati mwingine ulisaidia sana Taifa maana wasaidizi walijua lolote watakalompelekea atawa challenge tuHili tatizo linaanzia kule juu kabisa, unapokuwa na kiongozi asietaka kushughulisha akili yake kwa chochote zaidi ya kusubiri kuletewa taarifa na wasaidizi wake huyo ndie chanzo.
Wasaidizi wake wanaweza kumpelekea mawazo ya hovyo yenye malengo ya "kutupiga", na kwasababu kiongozi mwenyewe hawezi kuhoji chochote anayakubali tu mawazo hayo kutokana na namna pumba anazolishwa zitakavyokuwa zimepangiliwa.
Matokeo yake ndio haya, unaona habari ya kukodi software ya $ 30 milion, baada ya kutoka kule kwenye mradi wa LNG ambao nao naamini alipigwa sound akaukubali bila kujua chochote, wala asijue hao anaowatuma ndio wajanja wenyewe, anachofanya Rais ni sawa na kumkabidhi fisi bucha sasa tunavuna tulichopanda.
Halafu wabunge wenye uchungu na nchi yao kama Mh Mpina wakiibua bungeni kasoro hizi wanaandamwa sana na akina Msukuma, halafu mambo yanazimwa kirahisi na spika. Ndugai hangalikubali yazimwe.hii issue inaniuma sana, kwanini tusiwaamini wataalamu wetu wa ndani? mbona mfumo wa GePG umetengenezwa hapa bongo na unafanya kazi vyema tu, hizo hela tungewapa wataalamu wetu wa ndani zingewasaidia sana katika kujiimarisha kimifumo na ujuzi mwengine ambao ungezidi kuliheshimisha taifa letu kwa kuwaongezea CV na hatimae wangepata hata kazi zingine kimataifa. Hata kama nao wangesource baadhi ya vipengele kwa wataalamu wa nje ni sawa tu, hata kwenye sekta nyingine vingi vishafanyika kama hivyo na mambo yameenda vyema tu
kuna mtu anasema eti System haitokuwa stable wataalamu wa ndani hakuna wanachojua, kwanza, system kuzingua ni kitu cha kawaida na ndio maana hata wenye investment kubwa kama mitandao kijamii huwa kuna muda system inacheza lakini wana-troubleshoot na mambo yanakuwa sawa.
Very good question!!!Kwahiyo Tanesco wale ma- programmer wanafanya kazi gani?
IFM wanafundisha engineering?Tuliza puru usome uelewe!
USD 30 million ni equivalent na billion 69.5 za kitanzania! Hizo pesa ni nyingi mno kuna vichwa viko UDSM,DIT,IFM ambavyo with a fraction of that amount of money wangeweza ku develop system nzuri tu kwa msaada kidogo tu wa hao wahindi!
Haiingii akilini mtu alipe zaidi ya 70 billions kwa kukodi system mara mia angekuwa amaeinunua mazima! Hapo kuna upigaji wa kutisha sana! Hio system nauhakika haina thamani zaidi ya billion 10 kwa kuikodisha tu.
IQ ya Mama ni ndogo sana, form four failure, kaingia CCM, kafanya yake kujiendeleza vicertificate, na kupanda ngazi uko kupitia mafisi wa kiume wa uko CCM, kajikuta yuko hapo. Ni majanga kwa taifa.Hili tatizo linaanzia kule juu kabisa, unapokuwa na kiongozi asietaka kushughulisha akili yake kwa chochote zaidi ya kusubiri kuletewa taarifa na wasaidizi wake huyo ndie chanzo.
Wasaidizi wake wanaweza kumpelekea mawazo ya hovyo yenye malengo ya "kutupiga", na kwasababu kiongozi mwenyewe hawezi kuhoji chochote anayakubali tu mawazo hayo kutokana na namna pumba anazolishwa zitakavyokuwa zimepangiliwa.
Matokeo yake ndio haya, unaona habari ya kukodi software ya $ 30 milion, baada ya kutoka kule kwenye mradi wa LNG ambao nao naamini alipigwa sound akaukubali bila kujua chochote, wala asijue hao anaowatuma ndio wajanja wenyewe, anachofanya Rais ni sawa na kumkabidhi fisi bucha sasa tunavuna tulichopanda.
Si wanatoa best ICT graduates hapoIFM wanafundisha engineering?