TANESCO yasaini mkataba wa kuzalisha Umeme Jua MW 150 Kwa Bilioni 275. Waziri Makamba apiga marufuku mauziano ya Umeme kwa Dola

TANESCO yasaini mkataba wa kuzalisha Umeme Jua MW 150 Kwa Bilioni 275. Waziri Makamba apiga marufuku mauziano ya Umeme kwa Dola

Hivi ni Kwa nini nguvu moja isielekezwe sehemu moja ili ikikamilika ianze sehemu nyingine? Hata uangalizi unakuwa makini kwa hao contractors. Bwawa la Nyerere na Umeme wake wa maji na size ya source ya Umeme tuliambiwa shida ya Umeme itakuwa ni history likikamilika percent % sasa hizi source nyingine mpya za nini wakati ili bado? Anyway labda uelewa wangu ni mdogo.
Diversification mfano gesi tunaitegemea kwa umeme 70% hivi umewahi jiuliza siku ikitokea hitilafu kwenye Bomba la gesi au pale Kinyerezi 1 and 2 si nchi nzima tutakaa gizani miezi kibao. Ila ukiwa na energy mix inasaidia ku complement Bwawa la Nyerere na Gesi
 
Gharama za kuzalisha umeme wa jua ni kubwa ukilinganisha na gharama za kuzalisha umeme wa maji. Huu u.eme wa jua / upepo ni miradi ya kifisadi
Kakono.hydro 14 mgwt gharama Dola mil.100
Kishapu solar 150 megawatt gharama bil.275

 
Umemjibu kwa akili kubwa sana. Hizo Panel za Kichina zikimaliza mwaka nendeni mkatambike yani. Baada ya miezi 12 zoote zitahitaji repair ya 270Bil
Hiyo ni hasara ya mkandarasi sio Tanesco
 
Inaweza mbona, kamamna water fall yenye uwezo wa kuzungusha turbine yenye kufua kiwango hko cha umeme
Taja hiyo sehemu,kwanza mnajua gharama za bwawa la Nyerere Dola bil.3.5 ni Nje ya gharama zingine za miundombinu,njia za kusafirisha umeme nk?
 
Walijinasibu Nyerere dam soon litakuwa tayari na litatatua na kumaliza kabisa shida ya umeme.
Sasa why urukie huko kwenye solar au kuna 10% yako huko na hisa kiasi kadhaa..?
Halafu umeme wa solar gharama yake ipo kwenye maintenance yaani kubadili panels, wiring, batteries.
 
Ni mpango mzuri hasa kwa hilo lengo la chanzo mbadala badala ya kutegemea maji ambayo wakati fulani kuna ukame.

Tunahitaji ubunifu Ili umeme uwe unapatikana kwa urahisi,uhakika na unafuu. Hii ni hatua nzuri. Makamba ni kiongozi mbunifu. Kipindi alipokuwa Wizara ya Mawasiliano tulipata vifurushi na bando kwa bei nafuu baada ya kuwakomalia wamiiki wa makampuni ya Simu.
 
Issue sio kuzalisha hata Jangwani wanaweza kuzalisha kuzalisha ma_gigawatt let alone Megawatt issue ni tunazitunza vipi hizo megawatt ili wakati hakuna jua tuzitumie ? (Storage bado ni bottleneck kwenye solar)

Kwanini wanunue ili wauze ?, Kwanini wazimalize Bwawa la JKN haraka na lianze kazi ili badala ya kununua wao ndio wauze ?
Huo sio mradi wa nchi, ni mradi binafsi
 
Waziri Makamba katika hili amefanya jambo kubwa lenye kustahili pongezi. Kuwa na sera katika eneo la uzalishaji wa umeme kwa kutumia nishati jadidifu ni kitu cha msingi sana kwa wakati huu, hasa ikizingatia nchi yetu ipo katika ukanda wa kijografia wa kitropiki, basi hata uvunaji wa nishati hii utakuwa na ufanisi mkubwa sana.
Serikali Kupitia Tanesco imeandika Historia ya kusaini mkataba wa Kuzalisha Umeme wa Juna na kampuni ya China wenye thamani ya Shilingi Bilioni 275 ambao utazalisha megawatt 150 Kishapu ,Shinyanga na Kwa awamu ya kwanza Wataanza na megawatt 50.

Waziri wa Nishati January Makamba akishuhudia mkataba huo amepiga marufuku Tanesco kununua Umeme kutoka Kwa wazalishaji Kwa malipo ya dola badala yake Shilingi ndio ittumika..


Aidha amewataka Tanesco kuwawezesha wazawa Ili waweze kuzalisha umeme akisema hakuna maajabu Hadi wao washindwe..


My Take
Hongera sana Makamba,majungu achilia failures wewe endelea kuchapa kazi.

=======


Wizara ya Nishati kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) imesaini mkataba wa kwanza wa uzalishaji wa umeme Jua wa kiasi cha megawati 50 utakaotekelezwa wilayani Kishapu mkoani Shinyanga.

Mkataba huo umesainiwa tarehe 29 Mei, 2023 jijini Dodoma na kushuhudiwa na Waziri wa Nishati, Mhe.January Makamba ambaye alikuwa mgeni rasmi.

Kwa ujumla mradi huo wa umeme wa Jua ni wa megawati 150 ambapo awamu kwanza itajengwa mitambo itakayozalisha megawati 50 na awamu ya pili itajengwa mitambo ya megawati 100 kwa jumla ya shilingi bilioni 275. Utekelezaji wa mradi wa Awamu ya kwanza hautazidi miezi 12.

Akizungumza katika hafla hiyo, Waziri wa Nishati amesema kuwa “kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi tunaingiza umeme wa Jua katika gridi ya Taifa, nimpomgeze Rais wetu kwa kwa muongozo na uongozi ambao umepelekea nchi kuaminiwa na washirika wa maendeleo ikiwemo Shirika la Maendeleo la Ufaransa ambalo limetoa mkopo ambao utatekeleza mradi huu.”

Ameeleza kuwa, utekelezaji wa mradi huo wa Jua ni jitihada za Serikali za kuhakikisha inatengeneza mchanganyiko wa umeme wenye afya katika gridi ya Taifa ambao utatokana na vyanzo mbalimbali kama vile maji, gesi, upepo na Jua ili hata pale chanzo moja kinapotetereka, vyanzo vingine vitaendelea kuzalisha umeme.

Waziri Makamba amesema kuwa, ili kuongeza zaidi uzalishaji wa umeme kwa kutumia nishati jadidifu, Serikali inakuja na Sera mpya ya Nishati Jadidifu (iko kwenye maandalizi) ambayo itasaidia nchi kuongeza uwekezaji kwenye eneo hilo kwani fedha nyingi duniani, masoko ya mitaji na teknolojia mpya zinajielekeza kwenye nishati jadidifu.

Ameongeza kuwa, kwa sasa kazi inayofanyika pia ni kuainisha maeneo yaliyo na rasilimali ya nishati jadidifu na kipaumbele kitakuwa kwa wazawa kuwekeza kwenye miradi kama ya Upepo na Jua na Serikali itawaunga mkono na kwamba Serikali itakuja na muongozo wa utekelezaji wa suala hilo.

Ameongeza kuwa, kwa maeneo yaliyo nje ya gridi kama vile visiwa, bado Serikali itaendelea kuwezesha jitihada za kupelewa umeme kwa kutumia miradi ya nishati jadidifu kama vile Jua na Upepo.
"Waziri Makamba amesema kuwa, ili kuongeza zaidi uzalishaji wa umeme kwa kutumia nishati jadidifu, Serikali inakuja na Sera mpya ya Nishati Jadidifu (iko kwenye maandalizi) ambayo itasaidia nchi kuongeza uwekezaji kwenye eneo hilo kwani fedha nyingi duniani, masoko ya mitaji na teknolojia mpya zinajielekeza kwenye nishati jadidifu"
 
Kiukweli umeme wa maji ni janga kwenye hili la umeme wa Jua kama siyo siasa Waziri apewe maua yake.
275 billion ni hela ndogo
Kuna vitu viwili sijui kama umeviwaza
1) Tanesco itanunua umeme kutoka kwa mwekezaji, Kama ilivyokua inanunua kwa iptl
2) gharama ya mradi, bil 270 ni hela ndogo je ni kwa megawatt ngapi? Usidhani ni kwa megawatt 1000
 
Back
Top Bottom