TANESCO yatoa tamko kuzimika kwa taa za uwanjani mechi ya Shirikisho

DullyJr

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2011
Posts
13,983
Reaction score
11,857
Uwanja wa Taifa una hudumiwa na vyanzo viwili vya Umeme. TANESCO na Majenereta ya uwanja.

Mechi ya leo uwanja ulikuwa unahudumiwa na Majenereta ya uwanja.

Baada Majenereta kushindwa kufanya Kazi katikati ya mchezo na taa kuzimika uwanja uliamua kutumia chanzo cha TANESCO na mchezo ukaendelea.

Tunasikitika kwa kadhia iliyo iliyo jitokeza na tutashirikiana na wenzetu kwa siku za usoni jambo hili lisijirudie.

 
Tukisema NAPE na MAKAMBA ni watu wa hovyo na vilaza tunaonekana sisi ni Sukuma gang haya endeleeni. KAZI iendelee
 
Kwanini uwanja utumie majenereta mwanzoni? Umeme wa TANESCO ulikuwaje mpaka ikabidi watumie jenereta
 
Kwa ninavyojua mimi mtu mmoja muungwana kaangalia boli kwa dakika 20 kaona halivutiiii akaona azime umeme akapumzike zake weekend hii

Wakati anazima akajisema kimoyomoyo timu za maana zimecheza Ijumaa na Jumamosi hawa wengine saidia fundi tuuu
 
Ujinga mtupu.

Na huku mtaani nilipo umeme ulikatika nusu saa baada ya kurudi kule taifa na huku ni majenereta?
 
Ujinga mtupu.

Na huku mtaani nilipo umeme ulikatika nusu saa baada ya kurudi kule taifa na huku ni majenereta?
Mwamba kaangalia rede dk 15 kaona haelewi ,kazima zake umeme kaenda kupumzika wikiendi[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Mechi zilichezwa ijumaa na jumamosi[emoji1787]
 
Kwanza pale uwanjani nasikia taa kati ya 15% hazifanyi kazi kabisa.
Hata jenereta nasikia kuna moja halifanyi kazi.
Hata hizo taa nasikia haziingiliania na vyanyo vya umeme. Yaani kuna baadhi zinategemea jenereta tu na nyingine tanesco.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…