Tanga: Baada ya mke kuuawa, mwili wa mume nao waokotwa

Tanga: Baada ya mke kuuawa, mwili wa mume nao waokotwa

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Snapinsta.app_462182813_956561473162840_3011162439420272966_n_1080.jpg

Baba wa familia na mkazi wa barabara ya nne jijini Tanga Alii Bagidad (60) mwenye asili ya Kiasia ambaye mke wake pamoja na dada wa kazi walikutwa wamenyongwa pamoja na kutobolewa macho yao wiki iliyopita na yeye amekutwa amekufa baada ya mwili wake kuokotwa katika eneo la Nguvumali B jijini Tanga.

Mwili wa mtu huyo umekutwa katika eneo hilo lenye pori ambapo mpaka sasa bado haijajulikana chanzo cha kifo chake.

Mashuhuda wa tukio hilo wamesema waligundua tukio hilo baada ya kusikia harufu kali iliyokuwa ikitokea eneo ambalo amekutwa amekufa na hivyo kuwalazimu kujua ni kitu gani kilichopelekea harufu hiyo na ndipo walipokutana na mwili huo.
Snapinsta.app_462305999_956561746496146_6516304653791328427_n_1080.jpg

Snapinsta.app_462136366_956561753162812_458392467806980030_n_1080.jpg
Mjumbe wa mtaa wa Nguvumali B amesema ndani ya siku mbili mfululizo alikuwa akikutana na harufu hiyo akiamini ni mizoga ya wanyama ambayo imekuwa ikitupwa na wafugaji.

"Polisi walikuja wakaangalia wakawapigia simu ndugu zao wamekuja kuhakikisha kama kweli huu mwili ni wa ndugu yao wakakiri kuwa ni ndugu yao na ndipo taratibu nyingine zikaendelea kwa ajili ya kuuhifadhi mwili huo," amesema mjumbe huyo wa serikali ya mtaa.

Soma Pia: Tanga: Mume atuhumiwa kumuua mkewe, dada wa kazi kwa kuwanyonga na kuwatoboa macho

Katika taarifa ya awali jeshi la polisi lilimuhusisha marehemu na kifo cha mke wake pamoja na mfanyakazi waliokutwa wamenyongwa na kutobolewa macho nyumbani kwao barabara ya nne jijini Tanga.

Chanzo: EastAfricaTV
 

Baba wa familia na mkazi wa barabara ya nne jijini Tanga Alii Bagidad (60) mwenye asili ya Kiasia ambaye mke wake pamoja na dada wa kazi walikutwa wamenyongwa pamoja na kutobolewa macho...
Ingawa habari hii ina kama week hivi lakini MAPENZI MABAYA MAPENZI MABAYA in Banana's voice.
 

Baba wa familia na mkazi wa barabara ya nne jijini Tanga Alii Bagidad (60) mwenye asili ya Kiasia ambaye mke wake pamoja na dada wa kazi walikutwa wamenyongwa pamoja na kutobolewa....
Kesho ni fumbo kwetu Binadamu, ila tusisahau kumwomba sana Mungu kutupatia hekima kimaisha.

Ubinadamu ni kazi/The humanity is a work.
 
Mi naishi Tanga ,hyo stori ipo hivi mume aliwadhulumu wasomali pesa/madini baada ya kuwa wanafanya biashara.
Hovyo wasomali waliamua kumuua na unaambiwa wasomali ukiwadhulumu wanadhuru mpak familia yako Mana wamaamini mmekula wote.
Jamaa Ni muhindi alouliwa
 
Back
Top Bottom