Pre GE2025 Tanga: CCM yachangia madawati Shule ya Sekondari Mgwashi

Pre GE2025 Tanga: CCM yachangia madawati Shule ya Sekondari Mgwashi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Katika kusherehekea miaka 48 ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga na Mjumbe wa Kamati Kuu, Rajabu Abdulrahaman, ametembelea katika Shule ya Sekondari Mgwashi iliyopo Korogwe Vijijini Kata ya Mngwashi na kutoa mchango wa shilingi milioni saba (7,000,000) kwa ajili ya kununua madawati 100.
Snapinst.app_476114256_18478916458052562_6972919992401237745_n_1080.jpg
Naye Mbunge wa jimbo hilo, Timotheo Mzava, alichangia shilingi milioni saba (7,000,000) ili kukamilisha ununuzi wa madawati mengine 100.

Mwenyekiti Abdulrahaman alisisitiza kuwa CCM inatekeleza kwa vitendo kutatua changamoto za wananchi, huku akiwataka viongozi wa vyama vingine kuacha malalamiko na badala yake wachukue hatua stahiki.

Kuhusu kero ya ucheleweshaji wa ujenzi wa zahanati, Mwenyekiti Rajabu ametoa maagizo kwa uongozi wa halmashauri kuhakikisha kuwa ifikapo tarehe 1 Aprili 2025, zahanati hiyo iwe imeanza kutoa huduma kwa wananchi.
 
Back
Top Bottom