Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 2,060
- 5,648
Katika kusherehekea miaka 48 ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga na Mjumbe wa Kamati Kuu, Rajabu Abdulrahaman, ametembelea katika Shule ya Sekondari Mgwashi iliyopo Korogwe Vijijini Kata ya Mngwashi na kutoa mchango wa shilingi milioni saba (7,000,000) kwa ajili ya kununua madawati 100.
Naye Mbunge wa jimbo hilo, Timotheo Mzava, alichangia shilingi milioni saba (7,000,000) ili kukamilisha ununuzi wa madawati mengine 100.
Mwenyekiti Abdulrahaman alisisitiza kuwa CCM inatekeleza kwa vitendo kutatua changamoto za wananchi, huku akiwataka viongozi wa vyama vingine kuacha malalamiko na badala yake wachukue hatua stahiki.
Kuhusu kero ya ucheleweshaji wa ujenzi wa zahanati, Mwenyekiti Rajabu ametoa maagizo kwa uongozi wa halmashauri kuhakikisha kuwa ifikapo tarehe 1 Aprili 2025, zahanati hiyo iwe imeanza kutoa huduma kwa wananchi.
Mwenyekiti Abdulrahaman alisisitiza kuwa CCM inatekeleza kwa vitendo kutatua changamoto za wananchi, huku akiwataka viongozi wa vyama vingine kuacha malalamiko na badala yake wachukue hatua stahiki.
Kuhusu kero ya ucheleweshaji wa ujenzi wa zahanati, Mwenyekiti Rajabu ametoa maagizo kwa uongozi wa halmashauri kuhakikisha kuwa ifikapo tarehe 1 Aprili 2025, zahanati hiyo iwe imeanza kutoa huduma kwa wananchi.