Tanga Cement vs Twiga Cement

Tanga Cement vs Twiga Cement

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

MBUNGE MHE. GETERE - TANGA CEMENT INA HIFADHI YA MALIGHAFI YA SARUJI HUKU TWIGA CEMENT WANA MITAMBO MIZURI YA KUZALISHA SARUJI

Mbunge wa Jimbo la Bunda Vijijini Mhe. Boniphace Mwita Getere amegusia suala la Twiga Cement na Tanga Cement huku akichangia hoja ya bajeti ya Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara wakati wa kusomwa kwa bajeti ya Wizara na Waziri mwenye dhamana Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji

"Ni lazima serikali iwaangalie watu wa Tanga wananung'unika nini? hili jambo (la Twiga Cement kutaka kuinunua Tanga Cement) lisichukuliwe kama kawaida. Ni kweli mtu anayemiliki kiwanda (Tanga Cement) hana uwezo? " Mwita Getere, mbunge wa jimbo la Bunda vijijini.

"Kiwanda cha Tanga kina hifadhi kubwa ya malighafi ya kuzalisha saruji (clinker) halafu kiwanda cha Twiga Cement kuna mitambo mizuri ya kuzalisha saruji, sasa hapa utapima mwenyewe je ni kitu gani kitahama endapo Twiga Cement itainunua Tanga Cement? Je ni clinker itahama kwenda Dar es Salaam au mitambo itahama kutoa Dar es Salaam kwenda Tanga?" Mwita Getere, mbunge wa jimbo la Bunda vijijini.

FvSt1yxX0AEGyy6.jpg
 
NILIWAHI KUGUSIA SEHEMU HILI SAKATA LA TWIGA KUNUNUA TANGA CEMENT. Nianze kusema kuwa hii sekta ya Cement ni non regulated sector japo ni sector muhimu sana kwa ujenzi wa Taifa.Cement ni moja kati ya mahitaji muhimu kwa kwa ujenzi wa nchi hii na kuna mahali haina mbadala(Substute).Unaporuhusu watu wachache watawale soko nanuzalishaji wa cement ni hatari sanaa, uuzwaji wa Tanga kwa Twiga Cement Unamaanisha kwamba unapunguza wazalishaji sokoni kuwa wachache zaidi hivyo kupelekea umiliki wa soko hulia,Maana yake ni kwamba TWiga atakua anaamua azalishe kiasi gani kwa muda gani maana viwanda ni vyake.Tanzania tunaviwanda vikubwa vinne.Dangote cement,Twiga,Mbeya na Tanga Cement.Kuruhusu Twiga kununua Tanga Cement ni shida kubwa inamaana Tanga itakua chini ya Twiga na wazalishaji watakua watatu sio wanne tena,Hatari ya Upangaji Bei itatokea.Upangaji Bei utaiweka nchi katika wakati mgumu na kuathiri shughuli za kiujenzi kwa serikari na wananchi moja mmoja.VIpi Dangote akiinunua Mbeya Cement? Ikumbukwe kuwa Tanga Cement Ndio Kiwanda pekee chenye malighafi kubwa zaidi na nyingi kuliko vyote katika ukanda wa afrika mashariki,Najiuliza Unakuaje anapata hasara?Hapa kuna harufu ya usimamizi mbovu
 
Back
Top Bottom