Tanga: Zaidi ya wananchi 2000 wa Bondo waliochomewa nyumba zao, waishi chini ya miti

Tanga: Zaidi ya wananchi 2000 wa Bondo waliochomewa nyumba zao, waishi chini ya miti

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Ikiwa siku chache zimepita tangu tulivyoripoti taarifa kuhusu wananchi wa Bondo, Wilaya ya Kilindi Mkoani Tanga kulia kukosa makazi baada ya nyumba zao kuchomwa moto na kubomolewa kwa kuambiwa wamevamia hifadhi.

Inakadiriwa kuwa zaidi ya kaya 2,600 zimeachwa bila makazi, mali zao kuharibiwa, na familia zao kutawanyika, huku wengine wakiwa hawajui walipo wapendwa wao, ikiwemo watoto wadogo.

Tukio hili linahusishwa na operesheni ya kuwaondoa wananchi hao kwa madai ya kuvamia eneo la hifadhi ya msitu. Kwa mujibu wa mashuhuda, usiku wa tarehe 3 Januari ulikuwa wa mateso yasiyosahaulika, baada ya vikosi vya ulinzi vilivyojihami kwa silaha kuingia eneo hilo na kuanza kuwafurusha kwa nguvu. Inadaiwa kuwa mabomu ya machozi, risasi na moto vilitumika katika kuwaondoa wakazi hao, huku wengine wakidai kupigwa, kuteswa na hata wanawake kubakwa mbele ya watoto wao.

 
usiku wa tarehe 3 Januari ulikuwa wa mateso yasiyosahaulika, baada ya vikosi vya ulinzi vilivyojihami kwa silaha kuingia eneo hilo na kuanza kuwafurusha kwa nguvu. Inadaiwa kuwa mabomu ya machozi, risasi na moto vilitumika katika kuwaondoa wakazi hao, huku wengine wakidai kupigwa, kuteswa na hata wanawake kubakwa
Askari wa wanyama pori na misitu Tanzania ni makatili kwa binadamu wenzao kuliko wanyama, sijui kwa nini !!
 
Ikiwa siku chache zimepita tangu tulivyoripoti taarifa kuhusu wananchi wa Bondo, Wilaya ya Kilindi Mkoani Tanga kulia kukosa makazi baada ya nyumba zao kuchomwa moto na kubomolewa kwa kuambiwa wamevamia hifadhi.

Inakadiriwa kuwa zaidi ya kaya 2,600 zimeachwa bila makazi, mali zao kuharibiwa, na familia zao kutawanyika, huku wengine wakiwa hawajui walipo wapendwa wao, ikiwemo watoto wadogo.

Tukio hili linahusishwa na operesheni ya kuwaondoa wananchi hao kwa madai ya kuvamia eneo la hifadhi ya msitu. Kwa mujibu wa mashuhuda, usiku wa tarehe 3 Januari ulikuwa wa mateso yasiyosahaulika, baada ya vikosi vya ulinzi vilivyojihami kwa silaha kuingia eneo hilo na kuanza kuwafurusha kwa nguvu. Inadaiwa kuwa mabomu ya machozi, risasi na moto vilitumika katika kuwaondoa wakazi hao, huku wengine wakidai kupigwa, kuteswa na hata wanawake kubakwa mbele ya watoto wao.

ni muhimu sana wananchi kua na tabia ya kujigovern wenyewe kistaarabu bila shuruti na bila kupotoshana.

ni jambo la maana zaidi kutii, kuheshimu na kuzingatia sheria tunapojenga makazi ya kuishi ili kuepuka usumbufu baadae.

Pole sana wahusika licha ya taarifa hiyo kuja na porojo na chumvi nyingi kwa lengo la kupata huruma kwenye uvunjifu wa sheria 🐒
 
Duh,
Hatari sana hii..
Mwananchi anabomolewa nyumba/ anachomewa moto na kupigwa miti kwa shuruti halafu anafurushwa..
Mi-5 tena!
Tlaatlaah Lucas Mwashambwa
Gentleman,
ni muhimu kuzingatia sheria katika kuandaa makazi yako ili kuepuka usumbufu baadae.

Tunafuatilia kwa ukaribu zaidi jambo hilo ili kupata ukweli na kujiridhisha na hatimae kuona hatua muhimu za kuchukua 🐒
 
UNAJUA CCM INAPATA KURA KWA WAJINGA WA VIJIJINI, SASA NGOJA WAGEUKWE
 
Back
Top Bottom