Clever505
JF-Expert Member
- Jul 27, 2020
- 1,183
- 2,256
Mimi naishi Zanzibar sasa ni mwaka wa 12, nimekuja huku nikiwa mdogo sana 2012 nikiwa na miaka 19, mpaka sasa naanza kuwa mtu mzima kuna mambo nayaona huku ambayo mtanganyika ukija huku ukakaa siku mbili/tatu huwezi kuyaelewa. Adui wakubwa wa Wazanzibar ni:
1. CCM
Huku watu wote hawaitaki kabisa ccm, hata ifanye mema gani hawaitaki tuuuu, cha kushangaza ccm inashinda uchaguzi. Hapo nafikiri inajulikana kinachofanywa na maccm kushinda.
2. Ukristo
Chuki dhidi ya ukristo ni kubwa sana huku ila we Mtanganyika ukija hapa kwa siku chache sio rahisi kuona hilo ila sisi ambao tunakutana na hawa watu kwenye mikusanyiko mbalimbali mfano, masokoni, kwenye usafiri wa umma, mahospitalini, kazini ndo tunajua jinsi ukristo unasemwa vibaya kila kona.
3. Muungano
Muungano unachukiwa na kila rika la mzanzibar ambaye tayari ameshaanza kujitambua, cha kushangaza sisi watanganyika tunaupambania sana. Huku watu wanafundishwa jinsi muungano unavyowabana, unavyowakosesha uhuru na nchi Yao, why watanganyika hatufundishwi faida yake kama kweli ipo?
Inawezekana kuna faida kiserikali lakini je, wananchi wa kawaida mitaani wanaelewa faida yake? Wanachi wa Zanzibar wanajua na wanahimizana kuukataa muungano wakidai unaifanya Zanzibar isiwe huru, vipi sisi watanganyika mbona hatuna chochote cha kukizungumza mtaani ambacho ni kizuri kitakachotushawishi wananchi wa kawaida tuupambanie?
Huwezi kukuta vijana wa kitanganyika mtaani wanazungumzia uzuri wa muungano lakini ni mara nyingi sana mimi naona vijana wa kizanzibar wamekaa vijiweni wanauponda muungano na hawautaki kabisa.
Kama muungano ni mzuri tuelezeni tujue ili tuwe proud nao na tuupambanie kufanya uwe imara ila kama hamfanyi hivyo mnatufanya tusiwe na la kusema hata tunapokuta watu wanauponda. Hapa nilipo mi nipo tayari kwa chochote kwamba tuuvunje au tuendelee kwa sababu sioni faida yake kwangu ila kijana wa kizenji yeye jibu ni moja tu kwamba "hatuutaki muungano"
Kwa akili yangu huwa nawaza na kujisemea kwamba Nyerere alikuwa na wazo zuri la kutengeneza muungano ila alishindwa kabisa kuutengeneza muungano bora. Kwanza aliua jina la Tanganyika na kuliacha Zanzibar, hapo maana yake ni kwamba alitengeneza uzanzibar na utanzania wakati ilibidi atengeneze kitu kimoja tu utanzania. Pili, kufanya wazanzibar wawe huru kutawala hadi Tanganyika ila watanganyika hawana uhuru wa kutawala Zanzibar hilo ni kosa kubwa.
Kwa sasa tuna Tanzania na Zanzibar na wala si Tanganyika na Zanzibar hili ni kosa la Nyerere. Watanganyika tunalitaka sana jina la Tanzania ila wazenji hawataki kabisa kujihusisha nalo.
Wazee, tufundisheni faida ya muungano ili na sisi tufundishe vizazi vyetu, mnapoendelea kukaa kimya wasioutaka muungano hata kama ni wachache watashinda kwa hoja maana wanaoutaka muungano hawana points za msingi. Mimi hapa nilipo sina chochote cha maana cha kuja kuwafundisha kizazi changu kuhusu umuhimu wa muungano ila kijana wa kizanzibar anayo mengi ya kumueleza mwanae ili auchukie muungano.
= > Waliohoji uhalali wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar wafikia hatua gani?
= > Yajue mambo 22 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
= > Tanganyika ni lazima iendelee kuungana na Zanzibar?
= > Muungano wa Tanganyika na Zanzibar: Una faida gani na kwa manufaa ya nani?
= > Fahamu A-Z kuhusu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
= > Tuna Muungano wa Tanganyika na Zanzibar tu, siyo Tanzania
1. CCM
Huku watu wote hawaitaki kabisa ccm, hata ifanye mema gani hawaitaki tuuuu, cha kushangaza ccm inashinda uchaguzi. Hapo nafikiri inajulikana kinachofanywa na maccm kushinda.
2. Ukristo
Chuki dhidi ya ukristo ni kubwa sana huku ila we Mtanganyika ukija hapa kwa siku chache sio rahisi kuona hilo ila sisi ambao tunakutana na hawa watu kwenye mikusanyiko mbalimbali mfano, masokoni, kwenye usafiri wa umma, mahospitalini, kazini ndo tunajua jinsi ukristo unasemwa vibaya kila kona.
3. Muungano
Muungano unachukiwa na kila rika la mzanzibar ambaye tayari ameshaanza kujitambua, cha kushangaza sisi watanganyika tunaupambania sana. Huku watu wanafundishwa jinsi muungano unavyowabana, unavyowakosesha uhuru na nchi Yao, why watanganyika hatufundishwi faida yake kama kweli ipo?
Inawezekana kuna faida kiserikali lakini je, wananchi wa kawaida mitaani wanaelewa faida yake? Wanachi wa Zanzibar wanajua na wanahimizana kuukataa muungano wakidai unaifanya Zanzibar isiwe huru, vipi sisi watanganyika mbona hatuna chochote cha kukizungumza mtaani ambacho ni kizuri kitakachotushawishi wananchi wa kawaida tuupambanie?
Huwezi kukuta vijana wa kitanganyika mtaani wanazungumzia uzuri wa muungano lakini ni mara nyingi sana mimi naona vijana wa kizanzibar wamekaa vijiweni wanauponda muungano na hawautaki kabisa.
Kama muungano ni mzuri tuelezeni tujue ili tuwe proud nao na tuupambanie kufanya uwe imara ila kama hamfanyi hivyo mnatufanya tusiwe na la kusema hata tunapokuta watu wanauponda. Hapa nilipo mi nipo tayari kwa chochote kwamba tuuvunje au tuendelee kwa sababu sioni faida yake kwangu ila kijana wa kizenji yeye jibu ni moja tu kwamba "hatuutaki muungano"
Kwa akili yangu huwa nawaza na kujisemea kwamba Nyerere alikuwa na wazo zuri la kutengeneza muungano ila alishindwa kabisa kuutengeneza muungano bora. Kwanza aliua jina la Tanganyika na kuliacha Zanzibar, hapo maana yake ni kwamba alitengeneza uzanzibar na utanzania wakati ilibidi atengeneze kitu kimoja tu utanzania. Pili, kufanya wazanzibar wawe huru kutawala hadi Tanganyika ila watanganyika hawana uhuru wa kutawala Zanzibar hilo ni kosa kubwa.
Kwa sasa tuna Tanzania na Zanzibar na wala si Tanganyika na Zanzibar hili ni kosa la Nyerere. Watanganyika tunalitaka sana jina la Tanzania ila wazenji hawataki kabisa kujihusisha nalo.
Wazee, tufundisheni faida ya muungano ili na sisi tufundishe vizazi vyetu, mnapoendelea kukaa kimya wasioutaka muungano hata kama ni wachache watashinda kwa hoja maana wanaoutaka muungano hawana points za msingi. Mimi hapa nilipo sina chochote cha maana cha kuja kuwafundisha kizazi changu kuhusu umuhimu wa muungano ila kijana wa kizanzibar anayo mengi ya kumueleza mwanae ili auchukie muungano.
ZAIDI UNASHAURIWA KUSOMA MADA HIZI:
= > Lipo wapi tatizo kwenye muungano wa Tanganyika na Zanzibar? Tafakari!= > Waliohoji uhalali wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar wafikia hatua gani?
= > Yajue mambo 22 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
= > Tanganyika ni lazima iendelee kuungana na Zanzibar?
= > Muungano wa Tanganyika na Zanzibar: Una faida gani na kwa manufaa ya nani?
= > Fahamu A-Z kuhusu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
= > Tuna Muungano wa Tanganyika na Zanzibar tu, siyo Tanzania