Hongera kwa jitihada zako mkuu. Hata hivyo naomba nikuweke sawa wewe, mleta mada na wasomaji wengine kuhusu mambo mawili.
Jambo la kwanza ni kwamba Togo na Kamerun hakukabidhiwa kwa Ufaransa pekee. Ukweli ni kwamba kila moja ya makoloni haya mawili iligawanywa katika pande mbili yaani mashariki na magharibi. Sehemu ya mashariki ya kila koloni walipewa Wafaransa huku sehemu ya Magharibi wakipewa Waingereza (kama kumbukumbu zangu zipo sahihi). Hapa sitaelezea jinsi makoloni haya mapya yalivyotawaliwa.
Jambo la pili ni kwamba Namibia haikubaki kwa Wajerumani bali ilikuwa chini ya uangalizi wa League of Nations ambapo baadae wakaiweka chini ya uangalizi wa serikali ya Umoja wa Afrika ya Kusini ( South African Union government) ambayo ilianza mwaka 1910. Hatua ya kuikamilisha Namibia kwa serikali ya Afrika ya Kusini iliambatana na masharti kadhaa. Hapa pia sitaendelea zaidi.
Asante.
Mkuu, umejaribu kuelezea lakini naomba nikuweke sawa hapo kwenye mgawo.
Mimi sitasahau historia maana wengine humu kama mmeisoma vizuri huwezi kusahahu huu mkataba wa Varsailles.
Pia nakumbuka kulikuwa na suali katika A level la kuhusu kufafanua mkataba huu wa Versailles.
Ni mkataba mreefu unaojumuisha sehemu mbalimbali duniani lakini ntaelezea kwa Afrika.
Huu ulikuwa ni mkataba baina ya Ujerumani na nchi za magharibi wakiongozwa na Uingereza katika kuhakikisha vita haitokei tena.
Hivyo ukasainiwa tarehe 19 juni mwaka 1919 na mwezi October mwaka huohuo wa 1919 mkataba huu ukarekodiwa na League of Nations ambayo baadae (1945) ilikuja kuwa United nations.
Sasa mkataba ulikuaje?
Kipengele cha 119 kilitaka Ujerumani itangaze kwamba inaachia makoloni yake yaliyokuwa yakitunzwa na kampuni yake ya Germany East Afrika.
Baada ya hapo kipengele cha 22 kikatangaza kuwa makoloni hayo sasa yatakuwa chini ya jumuiya ya kimataifa au league of nations.
Hapa Uingereza akajitwalia kampuni ya Germany East Afrika (Tanganyika) ambayo mwanzo ilijumuisha koloni lililounda Tanganyika, Rwanda na Urundi, lakini sasa Rwanda na Urundi akapewa Ubelgiji.
Mfaransa akapewa Togo (Togoland) na Cameroon (Germany Kamerun)
Germany South West Afrika ambayo leo ni Namibia akapewa Afrika Kusini.
Pia katika kulipa fidia kwa Ujerumani kuivamia ardhi ya Ureno ambayo ilikuwa ikiitwa Portugese Afrika, Wajerumani wakany'ang'anywa sehemu moja ya Msumbiji inaitwa Kionga Triangle ambayo ipo kaskazini kwa msumbiji na ilikuwa pia chini ya kampuni ya Gremany East Afrika.
Wamakonde wa hapo Kionga wengi wao wanazunguza kireno lakini kuna makabila mengine kama ya Wamakua na Wamwani.
Sehemu hiyo ilikuwa kubadilishwa jina na kuwa inaitwa Cabo Delgado na makao yake makuu yanaitwa Pemba ambao ndio mji mkuu.
Wakuu historia ipo na ni sisi tu watanzania kuendelea kuelewa khasa hizi historia kwani historia inahusu jana, leo na kesho.
Nikurudi kwa mleta mada kuhusu kama leo tungekuwa wapi ni kwamba ilitegemea na malengo ya mkoloni lakini leo hii ukifika Windhoek Namibia utashangaa jinsi ilivyopangwa na haina tofauti sana na mji wa Tanga.
Wajerumani bado wapo pale na wanajihesabu kama ni wanamibia.