Sipendi kuamini ya kwamba mtawala wa kuteuliwa anayo mamlaka hata kuwazidi wasomi. Japo kwa nadra sanaaaaa napenda huhisi ya kwamba uongozi wa chuo unaweza kutumia sababu zitakazotolewa na wanafunzi ili kuwahukumu.
Kila mwanafunzi anapaswa kuwa makini na atakachoandika, la sivyo atakuwa ameandaa mafuta ya kumkaanga, hususani wale walio mrengwa hasi na uongozi (ikiwa kama uongozi ni dhalimu).
Ikiwa kama takribani kila mwanafunzi ataandika barua hivi
"...........wakati wa tukio nilikuwa mjini katika hali ya kupunguza uchovu uliotokana na majaribio. Nilipata habari juu ya kungwa chuo nikiwa hukohuko mjini. Nasikitika sana kwa kuwa matarajio yangu na ya jamii yangu yamevurugika baada ya kufunga chuo, pia sijui nitapata wapi hela za kujikimu, kodi, maji, umeme ikiwa kama muda wa semesta utaongezwa. Nawasihi sana msiongeze siku za masomo......". Je uongozi utabatilisha barua zote???